Tuesday, January 26, 2010

MURRAY, HENIN WATINGA NUSU FAINAL AUSTRALIA OPEN!!!




Mchezaji ambaye anaorodheshwa katika nafasi ya mbili kwa ubora wa Mchezo wa Tennis Duniani upande wa wanaume Roger Federer ameondolewa katika Michuano ya Wazi ya Australia baada ya kupata kichapo kutoka kwa Andy Murray.

Federer ameondoshwa katika mashindano ya Tennis ya Australia katika hatua ya robo fainali baada ya kukubali kichapo cha seti mbili kwa bila kabla ya kupata maumivu ya goti na kushindwa kuendelea na seti ya tatu.

Katika seti ya kwanza Murray aliweza kushinda kwa sita tatu kabla ya kushinda katika seti ya pili kwa saba sita na ndipo kunako seti ya tatu wakati akiongoza kwa tatu bila ndipo Federer alishindwa kuendelea na mchezo baada ya kuumia.

Naye Andy Roddick amefungishwa virago katika hatua ya robo fainali baada ya kukubalia kichapo cha seti tatu kwa mbili huku akifanikiwa kutoka nyuma na kusawazisha seti mbili na mchezo kuwa droo kabla ya kufungwa seti ya mwisho.

Roddick amechapwa na Marin Cilic kutoka Croatia na sasa kijana huyo atakuwa na kirabua dhidi ya Andy Murray katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo inayoendelea nchini Australia.

Kwa upande wa wanawake Justine Henin ametinga hatua ya nusu fainali baada ya kuvuna ushindi wa seti mbili kwa buyu dhidi ya Nadia Petrova katika mchezo uliokuwa mkali.

Henin ameshinda seti ya kwanza kwa saba sita kabla ya kuja katika seti ya pili na kushinda kwa saba tano na hivyo kujikatia tiketi yake ya kutinga hatua ya nusu fainali ya Mixhezo hiyo ya Wazi inatimua vumbi huko Australia.

No comments:

Post a Comment