Friday, January 15, 2010

MISAADA YAANZA KUWASILI NCHINI HAITI!!!!



Mashirika mbalimbali ya Misaada yameanza kupeleka misaada nchini Haiti kuwasaidia manusuru wa janga la Tetemeko la Ardhi ambalo limepiga nchi hiyo. Manusura wengi wanahitaji maji, chakula, malazi pamoja na msaada wa matibabu wa haraka.
Takwimu za Shirika la Msalaba Mwekundu zinaonesha watu zaidi ya elfu 50 wamepoteza maisha huku majeruhi wakiwa milioni 3.
Miili imeendelea kuzagaa katika mitaa ya nchi hiyo kutokana na zoezi la kuikosanya kwenda taratibu kutokana na kukosekana kwa vifaa vya kutosha na vya uhakika.

No comments:

Post a Comment