Monday, January 18, 2010

HENRY KUKUTANA NA RUNGU LA FIFA!!!!


Mshambuliaji wa Kimataifa wa Ufaransa na Barcelona, Thiery Henry ameitwa na Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Duniani, FIFA kwa ajili ya sakata la kushika mpira katika mechi yao ya kusaka nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia. Henry alishika mpira mara mbili katika mechi dhidi ya Jamhuri ya Ireland kabla hajapiga krosi iliyowekwa kimiani na William Gallas. Sakata la Henry kushika mpira kabla ya kufungwa kwa goli lilizua utata na kutaka kutia dosari mashindano ya mwaka yatakayofanyika nchini South Africa.

No comments:

Post a Comment