Tuesday, January 26, 2010

JK APAA KWENDA USWISI!!!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameondoka nchini leo tarehe 26, mchana kuelekea Davos, Uswiss kuhudhuria kikao cha kila mwaka kuhusu uchumi, World Economic Forum.

Kikao hicho kinachoanza tarehe 28 hadi 30 Januari, kinahudhuriwa na Viongozi Wakuu wa nchi, Wachumi, Viongozi wa Mashirika mbalimbali, Wanataaluma, Viongozi wa Dini na Wanaharakati mbalimbali duniani.

Mara baada ya kikao cha Davos, Rais Kikwete ataelekea Addis Ababa Ethiopia kuhudhuria Kikao cha kila mwaka cha Wakuu wa Nchi za Afrika, kitakachoanza tarehe 31Januari hadi tarehe 2, Februari mwaka huu.

Mara baada ya kikao cha Viongozi wa Afrika Rais Kikwete anatarajia kurudi Dar-es-Salaam.

No comments:

Post a Comment