Monday, January 18, 2010

ESSIEN AONDOLEWA KIKOSI CHA GHANA!!!!


Kiungo wa Kimataifa wa Ghana ambaye anakipiga katika Klabu ya Chelsea, Michael Essien ameondolewa katika Kikosi cha timu hiyo kutokana na kuumia goti katika mzoezi ya Timu hiyo. Kiungo huyo wa Black Stars amepata maumivu hayo akiwa katika Mji wa Cabinda kwenye mazoezi ya kawaida. Essien kuumia kwake kutakuwa pigo kwa timu hiyo kutokana na mchezaji huyo kucheza kipindi kimoja katika mechi na Ivory Coast.
Kwa sasa Ghana itamkosa Essien katika mchezo wake wa mwisho dhidi ya Burkina Faso.

No comments:

Post a Comment