Tuesday, December 22, 2009

ZANZIBAR GIZANI MPAKA MWAKANI

MIUNGURUMO YA JENERETA MAPAKA MWAKANI ZANZIBAR
Taarifa kutoka Kisiwani Zanzibar zimethibitisha kuwa umeme ambao ilibidi uwake leo umeshindikana na sasa huenda hali ya stima ikatengamaa hapo mwakani. Habari ambazo zimethibitishwa na Waziri mwenye dhamana ya Umeme Zanzibar imeeleza kuwa kifaa ambacho kilikuwa kinashughulikiwa katika kijiji cha Fumba kimeharibika tena na kinatakiwa kipelekwe Afrika Kusini ili kichongwe. Na kutokana na hiki kuwa kipindi cha sikukuu ya X-mass mafundi wamepumzika. Kwa hiyo ni lazima kifaa hicho kitapelekwa mwakani kwa ukarabati kabla ya kuletwa kwa majaribio.

No comments:

Post a Comment