Monday, December 21, 2009

PONGEZI ZA RAIS KIKWETE KWA ANNA ABDALLAH

PONGEZI BAADA YA KUPATA NISHANI KUTOKA BONDENI.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za pongezi Mama Anna Abdallah kwa kutunukiwa Nishani ya heshima na Serikali ya Afrika ya Kusini.

“Tuzo hiyo ni chachu na changamoto kwa viongozi na utendaji wao wawapo katika nafasi za kutumikia wananchi na pia ni ishara kubwa ya kuutambua mchango wa Tanzania katika ukombozi wa Afrika ya Kusini na Watu wake” Rais amesema.

Mama Anna Abdallah alipewa Tuzo ya Order of the Grand Companions of O.R Tambo, Silver na Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini.

Rais Kikwete amesema Mama Abdallah ameiwakilisha nchi na watu wake vyema na hivyo kuleta heshima kwa Taifa kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment