Wednesday, December 23, 2009

SOFAPAKA YATINGA FAINALI TUSKER

SOFAPAKA 4-0 TUSKER
Mabingwa wa Kabumbu nchini Kenya, Klabu ya Sofapaka imefanikiwa kutinga katika hatua ya fainali ya michuano ya Kombe la Tusker baada ya kuifyatua Tusker kwa jumla ya magoli manne kwa buyu. Sofapaka kwa sasa inasubiri mshindi kati ya watani wa jadi Simba na Yanga ili acheze naye fainali ya kuska mwali wa Tusker Mwaka huu. Simba na Yanga wanatarajiwa kusaka nafasi moja ya Fainali kesho kwenye Uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment