Thursday, December 24, 2009

MSIMBAZI HOI TUSKER

YANGA 2-1 SIMBA
Mabingwa Watetezi wa Tanzania Bara Yanga wamefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya Kombe la Tusker mara baada ya kumbanjua Mnyama mkali kuliko wote mwituni Simba kwa Magoli 2-1. Magoli ya Yanga yamefungwa na Jerryson Tegete (68) huku la pili likifungwa na Shamte Ally (117). Goli la Simba lilifungwa na Hillary Echesa (80). Yanga kucheza fainali na Sofapaka wakati Simba wanasaka nafasi ya tatu na Tusker.

No comments:

Post a Comment