Monday, May 3, 2010

MAMBO YA ARDHI!!

Wataalamu wa udongo wa kituo cha Utafiti UYOLE wamebaini kuwa ardhi ya Mkoa wa RUVUMA inakabiliwa na tatizo la upungufu wa madini ya Salfa hali inayochangia kuzorota kwa ustawi wa mazao hususani mahindi.

Matokeo ya Uchunguzi wa ardhi ya Mkoa wa RUVUMA yanakuja ikiwa ni miaka kumi tangu Mkoa huo upige marufuku matumizi ya Mbolea aina ya SA ambayo ina kiasi kikubwa cha madini ya salfa.

Athari za ardhi ya Mkoa wa Ruvuma kupungukiwa madini ya Salfa zimeathiri zaidi uzalishaji wa Zao la Mahindi, ambapo sasa wakulima wanashindwa kufikia rekodi ya kuzalisha magunia 25 hadi 30 ya mahindi, hali iliyowalazimu wataalamu kutoka kituo cha Utafiti wa Udongo Uyole kuendesha utifiti shirikishi katika vijiji vitatu vya wilaya ya Mbinga Mkoani Humo.

Afisa kilimo wa Mkoa wa RUVUMA amekiri kuwepo malalamiko ya wakulima juu ya kupigwa marufuku matumizi ya Mbolea ya SA, lakini akajitetea kuwa Mkoa ulishaagiza wilaya zipime ardhi upya na kutoa ushauri, agizo ambalo utekelezaji wake unasuasua

Pamoja ardhi ya Ruvuma kupungukiwa madini ya Salfa, Utifiti wa Uyole pia umebaini kuwa kuna upungufu wa Madini ya Nitrogen, Phosphoras, na Calcium (Habari kwa Hisani ya Gerson Msigwa)

No comments:

Post a Comment