Thursday, May 6, 2010

ODINGA ATEMA CHECHE!!!

Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amesema ili Bara la Afrika lipate maendelea lazima liepuke utegemezi kutoka kwa mataifa ya magharibi.

Waziri Mkuu Odinga amesema imefika wakati kwa Bara la Afrika kuanzisha vitegauchumi vyake kwa kutegemea rasilimali zilizopo barani humu.

Aidha Waziri Mkuu Odinga amesema licha ya changamoto ya miundombinu katika bara la Afrika bado inayonafasi ya kutengeneza miundombinu ili kujiletea maendeleo ya haraka.

Amesema moja ya nyenzo muhimu katika maendeleo ni miundombinu ambapo wawekezaji wengi wamekuwa wakiogopa kuwekeza katika Bara la Afrika kwa kuhofia ubovu wa miundombinu.

"Tukiwekeza kwenye miundombinu ya barabara,umeme,reli,mawasiliano tutakuwa tumepiga hatua kubwa kimaendeleo kwani hakuna mwekezaji anayewekeza kwenye miundombinu mibovu."

Odinga amesema kwa zaidi ya miaka 40 ya uhuru wa bara la Afrika nchi nyingi hazijapiga hatua ya maendeleo kutokana na uongozi mbovu na kusema kuwa kwa sasa demokrasia inachukiua mkondo wake.

Ametolea mfano wa Kenya katika suala la demokrasia kuimarika amesema nchi yake imekuwa mfano wa kuigwa kwa kufanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo na amesema kuanzia siku 90 katiba hiyo mpya itakuwa imekamilika na kutawanywa kwa wananchi.

"Hivi sasa demokrasia katika nchi nyingi za Afrika ni nzuri japo kwa mfano Kenya marekebisho ya katiba yatakamilika siku tisini kuanzia leo na kutawanya kwa wananchi".

No comments:

Post a Comment