Tuesday, May 4, 2010

TANGAZO LA TIGO MATATANI!!!

Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara wameitaka Kampuni ya simu za Mkononi ya Tigo kusitisha matumizi ya tangazo linalomuonesha mtu anayejisaidia vichakani wakati wa safari ya kwenda Songea wakidai tangazo hilo linaudharirisha Mkoa wa Ruvuma.

Wajumbe hao, wameilaumu kampuni ya tigo kwa kutengenza tangazo lisiloeleza hali halisi kwa kuwa eneo lililowekewa kibao cha Songea halipo Mkoani Ruvuma, wala basi lilitumika halitoi huduma Mkoani Ruvuma.

Pamoja na kuitaka kampuni ya Tigo kusitisha matumizi ya Tangazo hilo, wajumbe hao waliokuwa chini ya Mkuu wa Mkoa Dr Christin Ishengoma wametishia kudai fidia kutoka kampuni ya Tigo endapo itaendelea kulitumia tangazo hilo katika vyombo vya habari vya Luninga.

Tangazo la Kampuni ya simu ya tigo linalolalamikiwa, linaonesha kilometa 250 kabla kufika SONGEA mtu mmoja anaingia vichakani kwa ajili ya kujisaidia, na kisha anaachwa na baada ya kulisimamisha basi hilo kwa kutumia simu.

Aidha wajumbe wa Bodi ya barabara Mkoani Ruvuma wameridhia mpango wa wakala wa barabara Mkoani humo, wa kujenga vituo viwili vya vyoo kati ya Njombe na Songea kwa ajili ya kujisaidia abiria wanaosafiri kutoka na kuingia Mkoani Ruvuma.

No comments:

Post a Comment