Wednesday, May 5, 2010

CUF WAMGEUKIA WAZIRI GHASIA!!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeshangazwa na kauli aliyoitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia katika moja ya chombo cha habari nchini, kuwa chama chetu ndio chanzo cha kushawishi “Sakata lililoandaliwa la Mgomo wa Wafanyakazi nchini”.

Akizungumza na chombo hicho cha habari, ambacho jina lake tunalo alisema kuwa Chama cha CUF ndio chanzo cha uchochezi kwa Wafanyakazi kupitia taasisi yao ya TUCTA kupanga mgomo ambao Rais Jakaya Kikwete ameshautolea Tamko kuwa ameupiga marufuku, atakegoma atafukuzwa kazi, na atakaeandamana kukiona cha moto.

CUF – Chama cha Wananchi tunamuelimisha Waziri Hawa Ghasia kuwa Chama chetu ni cha siasa na kipo kwa ajili ya kutetea maslahi ya wananchi wote Tanzania na kukemea vitendo vyovyote vya udhalilishaji, ukiukaji wa haki za binadamu, ubakaji wa demokrasia nchini, ubadhirifu, ufisadi na vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani na uchochezi nchini.

CUF – Tunawatanabahisha Watanzania kuwa makini na Viongozi wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwamba wapo kwa ajili ya maslahi yao na kulindana, badala ya kuwatumikia wananchi waliowachagua wakiwemo Wakulima, Wafanyabiashara na Wafanyakazi.

No comments:

Post a Comment