Thursday, May 6, 2010

CUF YATOA SALAM ZA RAMBIRAMBI KWA NIGERIA!!

CUF- Chama Cha Wananchi, tumepokea kwa masikitiko makubwa habari za msiba wa Rais wa Nigeria Umar Yar'Adua hivyo tunatoa pole kwa Wananchi wa Nigeria.

Rais Umar Yar' Adua alikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Wanaigeria wanafikia malengo yao ya Maendeleo na kuwa na Amani ya Kudumu katika nchi yao. Pia alihakikisha anayafanyia kazi mambo matatu muhimu kwa Wanaigeria ambayo ni kushughulikia Rushwa na Ufisadi uliokithiri nchini humo, pili kuhakikisha Nigeria inakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi itakayo tenda haki kwa watu wote na jambo la tatu ni kuhakikisha Nigeria inakuwa na amani ya kudumu kwa kukubaliana na Waasi hasa katika maeneo ya mafuta.

CUF - Pamoja na kumtakia kila la kheri Rais mpya aliyeapishwa Goodluck Jonathan ambaye alikuwa ni Makamo wa Rais, lakini pia ni matarajio yetu kuwa atahakikisha anaifanyia kazi na kuiendeleza mipango na malengo mazuri aliyoyaacha Marehemu Umar Yar' Adua, na kuhakikisha anaondoa ubaguzi wa aina yoyote na kuleta umoja na mshikamano kwa Wanigeria.

CUF- tunatarajia kuwa Wanaigeria watakuwa na utulivu wa hali ya juu katika kipindi hiki cha majonzi hasa kwa kuzingatia Nigeria ni nchi yenye watu wengi Barani Afrika hivyo kuwa ni mojawapo ya Nchi yenye Uchumi ulio juu ikilinganishwa na baadhi ya nchi nyingine.

Mungu amlaze mahali pema peponi Marehemu Umar Yar' Adua, Amin!!

No comments:

Post a Comment