Sunday, May 23, 2010

VITA YA INTER MILAN vs BAYERN MUNICH!!!














Mambo yalivyokuwa katika Uga wa Santiago Bernabeu wakati wa Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya. Inter Milan walifanikiwa kubeba mwali baada ya kuifunga Bayern Munich magoli 2-0!!!

MOURINHO SAFARI REAL DE MADRID!!


Kocha mwenye mbwembwe na tambo nyingi Jose Antonio Mourinho maarufuf kama Special One ametangaza nia yake ya kutaka kukinoa kikosi cha Real De Madrid baada ya kuipa ndoo tatu Inter Milan ikiwepo na ile ya Champions League. Mourinho amesema kama haujafundisha Real De Madrid utakuwa haujakamilika. Mourinho amesema ana uchungu sana kuona mechi dhidi ya Bayern Munich imekuwa ya mwihso kwake akiwa Inter Milan. Special One amesema kwa sasa ananyumba Stanford Bridge na San Siro na sasa anataka kuongeza Santiago Bernabeu.

Saturday, May 22, 2010

CHAMAKH ATUA RASMI ARSENAL!!


Klabu ya Arsenal imethibitisha kumsajili Mshambuliaji wa kimataifa wa Morocco Marouane Chamakh kwa mkataba wa muda mrefu baada ya kumalizana na timu yake ya Bordeuax ya Ufaransa. Huu ni usajili wa kwanza Arsene Wenger kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi!!!

SAA CHACHE ZIMESALIA KABLA YA KUPATIKANA BINGWA!!!


Saa chache zimesalia kabla ya Bingwa wa mwaka huu wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya hajapatikana. Miamba Inter Milan inatarajiwa kuumana na Bayern Munich. Na tayari Kocha wa Inter Milan Jose Mourinho ameendelea kukataa kuongelea future yake hasa kutokana na kuhusishwa na kujiunga na Real Madrid!!!

AJALI YA NDEGE INDIA!!!



Takriban watu 158 ambao ni abiria wa Air India wamefariki dunia baada ya ndege waliyokuwa wanasafiria kuanguka katika Mji wa Mangalore wakati taarifa zikisema watu nane wamenusurika!!!

Friday, May 21, 2010

VITA YA DUNIA INTER MILAN vs BAYERN MUNICH!!



Vita ya Dunia inasubiri kwenye Fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya ambayo kwa mara ya kwanza inachezwa siku ya jumamosi tofauti na ilivyozoeleka huwa usiku wa Jumatano. Mchezo huo unawakutanisha Inter Milan wanaonolewa na Jose Antonio Mourinho dhidi ya Bayern Munich iliyochini ya Louis Van Gaal. J e nani kuibuka mbabe kati ya Special One Mourinho au Van Gaal??

SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA CCM WILAYANI KYELA!!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Mbeya, Bwana Nawab Mullah kutokana na kifo cha Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya ya Kyela, Marehemu Japhet Mwakasumi, aliyefariki tarehe 19 Mei, 2010 Jijini Dar es Salaam.

Katika salamu zake hizo, Rais Jakaya Kikwete amesema amesikitishwa na kuhuzunishwa sana na taarifa za kifo cha Marehemu Mwakasumi kilichotokea nyumbani kwake Ukonga – Banana, Jijini Dar es Salaam.

“Ninatambua vema mchango wa Marehemu Mwakasumi wakati wa uhai wake katika Wilaya ya Kyela hususan katika Chama Cha Mapinduzi kutokana na uhodari na uchapakazi wake ambao umeiwezesha CCM kuimarika zaidi, “amesema Rais Kikwete na kuongeza, “Kwa hakika kifo chake ni pigo kubwa kwa familia yake, wana – CCM na wananchi wote wa Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya na Taifa kwa ujumla”

Katika rambirambi zake kwa familia ya Marehemu Japhet Mwakasumi, Rais Kikwete amesema familia hiyo imepoteza kiongozi muhimu. Amewataka ndugu, jamaa na marafiki wa Marehemu Mwakasumi kuwa na moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo, na amemuomba Mwenyezi Mungu ailaze mahali pema peponi roho ya Marehemu Japhet Mwakasumi.

KIKOSI CHA SPAIN WORLD CUP!!

Goalkeepers: Iker Casillas (Real Madrid), Jose Manuel 'Pepe' Reina (Liverpool), Victor Valdes (Barcelona).

Defenders: Raul Albiol (Real Madrid), Alvaro Arbeloa (Real Madrid), Joan Capdevila (Villarreal), Carlos Marchena (Valencia), Gerard Pique (Barcelona), Carles Puyol (Barcelona), Sergio Ramos (Real Madrid).

Midfielders: Xabier Alonso (Real Madrid), Sergio Busquets (Barcelona), Cesc Fabregas (Arsenal), Andres Iniesta (Barcelona), Javier Martinez (Athletic Bilbao), David Silva (Valencia), Xavi Hernandez (Barcelona).

Forwards: Jesus Navas (Sevilla), Juan Manuel Mata (Valencia), Pedro Rodriguez (Barcelona), Fernando Llorente (Athletic Bilbao), Fernando Torres (Liverpool), David Villa (Valencia).

GRANT ABWAGA MANYANGA PORTSMOUTH!!



Kocha Mkuu wa Klabu ya Portsmouth Avram Grant ambaye ni raia wa Israel ametangaza kujiuzulu nafasi yake baada ya kushindwa kuibakisha Timu huyo Ligi Kuu Nchini England. Grant amethibitisha kubwaga kwake manyanga baada ya hapo awali kuwepo uvumi!!

CUF WATOA KAULI MAUAJI YA KATIBU CCM MWANZA!!

CUF – Chama cha Wananchi tunawasihi Wagombea na Viongozi wa Vyama vya Siasa vya upinzani kwa ngazi zote kuwa makini juu ya usalama wao kuelekea uchaguzi mkuu ujao kutokana na dalili mbaya ya mauaji ya Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Kata ya Isamilo mkoani Mwanza, Bahati Stephano yaliyofanyika wiki iliyopita,.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari mauaji hayo yanahusishwa na tetesi za kisiasa na tayari watu wanne wanaotuhumiwa kuhusika na mauaji hayo wamekamatwa akiwemo Meya wa Jiji la Mwanza ambaye pia ni Diwani wa Kata hiyohiyo ya Isamilo, Bandiho Bihondo (64).

CUF – Chama cha Wananchi tumeshitushwa na mauaji hayo kufanyika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu, na hasa ikizingatiwa kuwa aliyeuliwa alikuwa ni kiongozi wa chama cha siasa kilichoko madarakani na wanaotuhumiwa wanahusika kwa njia moja au nyingine ni wanachama wa chama hicho.

CUF – Kutokana na mazingira ya kifo hicho tunazidi kusisitiza na kuwaasa Wagombea na Viongozi wa vyama vya Siasa vya upinzani kwa ngazi zote kuwa macho na maisha yao, na waichukulie kuwa hii ni dalili ya hali ya hatari, kwa wale wagombea wa upinzani wanaokubalika katika maeneo yao, na viongozi waliomstari wa mbele katika ujenzi wa chama kiasi cha kuwa tishio katika maeneo yatakayogombewa hususani kwa wanaotaka kutetea nafasi zao.

CUF – Tunawasihi Wananchi wa Tanzania hususani wapiga kura wote kuwa makini na wagombea ambao wanaona nafasi walizonazo wanahati miliki nazo, kutoa fundisho kwa wagombea hao na chama chao cha CCM ili watambue kuwa nchi hii ni yetu sote na wananchi (wapiga kura) ndio wenye hati miliki ya nani ndie mstahiki wa kuongoza nchi kwa kipindi husika.

VILLA AKAMILISHA USAJILI BARCELONA!!



Mshambuliaji wa Kimataifa wa Spain David Villa amekamilisha usajili wake wa kujiunga na Mabingwa wa La Liga Barcelona kitokea Valencia! Villa amesajiliwa kwa kitita cha pauni 34.2 na kusaini mkataba wa miaka minne kwa vijana hao wa Catalan!!!

Sunday, May 16, 2010

BAYERN MUNICH YATWAA TAJI LA PILI!!!


Klabu ya Bayern Munich imefanikiwa kutwaa ubingwa wake wa pili mwaka huu baada ya kushinda taji la Chama Cha Soka nchini Ujerumani kwa kuichakaza Werder Bremen kwa magoli manne bila ya jibu!! Magoli ya washindi wamefungwa na Arjen Robben, Ivica Olic, Franck Ribery na Bastian Schweinsteiger. Bayern wametinga pia fainali ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya wakiwa na kibarua dhidi ya Inter Milan!!

BALLACK KUFANYIWA SCAN YA ENKA!!



Nahodha wa timu ya taifa ya Ujerumani Michael Ballack anafanyiwa scan ya kifundo chake cha mguu ambacho ameumia kwenye mchezo wa fainali ya FA dhidi ya Portsmouth. Ballack alipigwa daruga na Kevin Prince Boateng na hivyo yupo mashakani kushiriki fainali za Kombe la Dunia zinazoanza mwezi ujao nchini Afrika Kusini!!!

CHELSEA BINGWA FA!!








Klabu ya Chelsea maarufu kama The Blues wamefanikiwa kutwaa taji lao la pili msimu huu baada ya kuifunga Portsmouth maarufu The Pompey kwenye fainali ya FA kwa goli moja kwa nunge!! Hongereni Wazee wa Darajani kwa kuwa na mwaka wa mafanikio!!

Wednesday, May 12, 2010

NDEGE YA ABIRIA YAANGUKA LIBYA!!


Watu zaidi ya mia moja wamepoteza maisha baada ya ndege ya Afriqiyah ya nchini Libya kuanguka katika Mji wa Tripoli! Mtoto wa miaka minane pekee ndiye ambaye amesalimika kwenye ajali hiyo! Ajali hiyo imetokea wakati ndege hiyo ikitokea nchini Afrika Kusini!!

Sunday, May 9, 2010

SHERIA YA WALEMAVU YALILIWA!!!

Mkuu wa Kitengo Cha Walimu wenye ulemavu wa Chama Cha Walimu Tanzania CWT Peter Mlimahadala amemuomba Rais Jakaya Kikwete kusaini haraka sheria ya Walemavu iliyopitishwa na Bunge hivi karibuni ili ianze kutumika na kuwanusuru walemavu wengi ambao haki zao zinapotea.

Mwalimu Peter Mlimahadala ambaye alikuwa akikabidhi Msaada Baiskeli Mbili za walemavu kwa wanafunzi Wilayani Songea Mkoani Ruvuma pia ametaka Serikali ichukue hatua za haraka kuondoa kodi na kuweka ruzuku kwa vifaa vya walemavu ambavyo kwa sasa havinunuliki kutokana na kuuzwa bei kubwa.

Pamoja na kuomba kusainiwa haraka kwa sheria ya Walemavu ya mwaka 2010, Mlimahadala pia ameomba serikali kutafuta ufumbuzi wa tatizo la vifaa vya walemavu kuuzwa kwa bei ya juu akipendekeza Serikali itoe ruzuku kwa vifaa hivyo.

Aidha Amependkeza Vifaa vya walemavu ambavyo huingizwa hapa nchini kutoka nje ya nchi visitozwe kodi, ili viwafikie walemavu kwa bei nafuu.

Akiwa Mjini Songea Mwalimu Peter Mlimahadala amekabidhi Baiskeli mbili za walemavu zenye thamani ya zaidi shilingi milioni moja zilizotolewa na CWT ambacho ni chama pekee cha wafanyakazi chenye kitengo cha Walemavu. (Habari kwa Hisani ya Gerson Msigwa)

Saturday, May 8, 2010

KIKOSI CHA GHANA KWA WORLD CUP!!!


Goalkeepers: Richard Kingston (Wigan, England) Daniel Adjei (Liberty Professionals), Stephen Ahorlu (Hearts of Lions) , Stephen Adams (Aduana Stars)

Defenders: Samuel Inkoom (Basle, Switzerland), Hans Sarpei (Bayer Leverkusen, Germnay) Lee Addy (Bechem Chelsea), John Mensah (Sunderland, England), Rahim Ayew (Zamalek, Egypt), Isaac Vorsah (Hoffenheim, Germany), John Pantsil (Fulham, England), Jonathan Mensah (Granada, Spain) Eric Addo (Roda JC, Holland)

Midfielders: Dede Ayew (Arlese Avignon, France) Michael Essien (Chelsea, England) Kwadwo Asamoah (Udinese, Italy) Agyemang Badu (Udinese, Italy) Stephen Appiah (Bologna, Italy) Anthony Annan (Rosenborg, Norway) Haminu Dramani (Lokomotiv Moscow, Russia), Sulley Muntari (Inter Milan, Italy) Quincy Owusu-Abeyie (Al Sadd, Qatar), Derek Boateng (Getafe, Spain) Bernard Kumordzi (Panionios, Greece) , Laryea Kingston (Hearts, Scotland), Kevin-Prince Boateng (Portsmouth, England)

Strikers: Prince Tagoe (Hoffenheim, Germany) Asamoah Gyan (Rennes, France), Dominic Adiyiah (AC Milan, Italy), Matthew Amoah (NAC Breda, Holland)

MAGARI YA MASTAA WA ULAYA NA MAREKANI!!!








Haya ni baadhi ya magari ambayo yanatumiwa na Mastaa wa Ulaya na hata Marekani ambao wanayanunua kwa fedha nyingi sana. Sijui lini Mastaa wa hapa kwetu nao watafikia hapa na kuachana na kutamba na Vinadia vyao!!

Thursday, May 6, 2010

MAZISHI YA RAIS YAR'ADUA!!!!






Wakuu wa Jeshi la Nigeria wakiwa wameubeba mwili wa Marehemu Rais Alhaj Umar Yar'Adua ambaye amezikwa katika eneo la Katsina nchini humo!! Mwili huo ulisafirishwa kwa ndege baada ya watu kupata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa Kiongozi huyo!!!

RAIS GOODLUCK JONATHAN AKIAPISHWA!!


Rais mpya wa Nigeria Goodluck Jonathan akiapishwa rasmi kushika madaraka ya kuliongoza taifa hilo kufuatia kifo cha Rais Umar Yar'Adua!!

RAIS MPYA WA NIGERIA GOODLUCK JONATHAN!!!


Rais mpya wa Nigeria ameapishwa rasmi saa kadhaa kabla ya kuzikwa kwa Alhaj Umar Yar'Adua. Kaimu Rais wa Taifa hilo Jonathan Goodluck ameapishwa kuchukua nafasi ya marehemu Yar'Adua!!!

CUF YATOA SALAM ZA RAMBIRAMBI KWA NIGERIA!!

CUF- Chama Cha Wananchi, tumepokea kwa masikitiko makubwa habari za msiba wa Rais wa Nigeria Umar Yar'Adua hivyo tunatoa pole kwa Wananchi wa Nigeria.

Rais Umar Yar' Adua alikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Wanaigeria wanafikia malengo yao ya Maendeleo na kuwa na Amani ya Kudumu katika nchi yao. Pia alihakikisha anayafanyia kazi mambo matatu muhimu kwa Wanaigeria ambayo ni kushughulikia Rushwa na Ufisadi uliokithiri nchini humo, pili kuhakikisha Nigeria inakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi itakayo tenda haki kwa watu wote na jambo la tatu ni kuhakikisha Nigeria inakuwa na amani ya kudumu kwa kukubaliana na Waasi hasa katika maeneo ya mafuta.

CUF - Pamoja na kumtakia kila la kheri Rais mpya aliyeapishwa Goodluck Jonathan ambaye alikuwa ni Makamo wa Rais, lakini pia ni matarajio yetu kuwa atahakikisha anaifanyia kazi na kuiendeleza mipango na malengo mazuri aliyoyaacha Marehemu Umar Yar' Adua, na kuhakikisha anaondoa ubaguzi wa aina yoyote na kuleta umoja na mshikamano kwa Wanigeria.

CUF- tunatarajia kuwa Wanaigeria watakuwa na utulivu wa hali ya juu katika kipindi hiki cha majonzi hasa kwa kuzingatia Nigeria ni nchi yenye watu wengi Barani Afrika hivyo kuwa ni mojawapo ya Nchi yenye Uchumi ulio juu ikilinganishwa na baadhi ya nchi nyingine.

Mungu amlaze mahali pema peponi Marehemu Umar Yar' Adua, Amin!!

RAIS YAR'ADUA AFARIKI DUNIA!!!


Rais wa Nigeria Alhaj Umar Yar'Adua amefariki na kuzikwa kijijini kwake baada ya kuwa mgonjwa kwa muda wa miezi karibu saba! Kiongozi huyo amefariki akiwa na umri wa miaka 59 alikuwa anasumbuliwa na Ugonjwa wa Moyo na Ini! Mwenyezimungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi!!!

ODINGA ATEMA CHECHE!!!

Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga amesema ili Bara la Afrika lipate maendelea lazima liepuke utegemezi kutoka kwa mataifa ya magharibi.

Waziri Mkuu Odinga amesema imefika wakati kwa Bara la Afrika kuanzisha vitegauchumi vyake kwa kutegemea rasilimali zilizopo barani humu.

Aidha Waziri Mkuu Odinga amesema licha ya changamoto ya miundombinu katika bara la Afrika bado inayonafasi ya kutengeneza miundombinu ili kujiletea maendeleo ya haraka.

Amesema moja ya nyenzo muhimu katika maendeleo ni miundombinu ambapo wawekezaji wengi wamekuwa wakiogopa kuwekeza katika Bara la Afrika kwa kuhofia ubovu wa miundombinu.

"Tukiwekeza kwenye miundombinu ya barabara,umeme,reli,mawasiliano tutakuwa tumepiga hatua kubwa kimaendeleo kwani hakuna mwekezaji anayewekeza kwenye miundombinu mibovu."

Odinga amesema kwa zaidi ya miaka 40 ya uhuru wa bara la Afrika nchi nyingi hazijapiga hatua ya maendeleo kutokana na uongozi mbovu na kusema kuwa kwa sasa demokrasia inachukiua mkondo wake.

Ametolea mfano wa Kenya katika suala la demokrasia kuimarika amesema nchi yake imekuwa mfano wa kuigwa kwa kufanyia marekebisho katiba ya nchi hiyo na amesema kuanzia siku 90 katiba hiyo mpya itakuwa imekamilika na kutawanywa kwa wananchi.

"Hivi sasa demokrasia katika nchi nyingi za Afrika ni nzuri japo kwa mfano Kenya marekebisho ya katiba yatakamilika siku tisini kuanzia leo na kutawanya kwa wananchi".

Wednesday, May 5, 2010

SILVA AITAMANI MAN UTD!!!!


Mshambuliaji wa Kimataifa wa Spain ambaye anasukuma gozi katika Klabu ya Valencia David Silva ameweka bayana anaitamani Klabu ya Manchester United na kama itaweza kumudu dau lake hawezi kukataa kujiunga nao! Mshambuliaji huyo amesema ni wazi duniani kwa sasa kila mchezaji anatamani kucheza Ligi ya England na hasa Klabu kama Manchester United!!!!

WENGER BADO YUPO YUPO SAANAAA!!!!


Kocha Mkuu wa Klabu ya Arsenal Arsene Wenger amesaini mkataba ambao utamuwezesha kuendelea kukinoa kikosi hicho kilichosheheni Ndama hadi mwaka 2013. Wenger ambaye amekuwa akilaumiwa kutokana na kuendekeza sera yake ya kutumia wachezaji chipukizi atakuwa na jukumu la kuhakikisha timu hiyo inatwaa ubingwa ambao umekuwa historia kwa miaka zaidi ya mitatu sasa!!!!

CUF WAMGEUKIA WAZIRI GHASIA!!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeshangazwa na kauli aliyoitoa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia katika moja ya chombo cha habari nchini, kuwa chama chetu ndio chanzo cha kushawishi “Sakata lililoandaliwa la Mgomo wa Wafanyakazi nchini”.

Akizungumza na chombo hicho cha habari, ambacho jina lake tunalo alisema kuwa Chama cha CUF ndio chanzo cha uchochezi kwa Wafanyakazi kupitia taasisi yao ya TUCTA kupanga mgomo ambao Rais Jakaya Kikwete ameshautolea Tamko kuwa ameupiga marufuku, atakegoma atafukuzwa kazi, na atakaeandamana kukiona cha moto.

CUF – Chama cha Wananchi tunamuelimisha Waziri Hawa Ghasia kuwa Chama chetu ni cha siasa na kipo kwa ajili ya kutetea maslahi ya wananchi wote Tanzania na kukemea vitendo vyovyote vya udhalilishaji, ukiukaji wa haki za binadamu, ubakaji wa demokrasia nchini, ubadhirifu, ufisadi na vitendo vyovyote vinavyoashiria uvunjifu wa amani na uchochezi nchini.

CUF – Tunawatanabahisha Watanzania kuwa makini na Viongozi wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwamba wapo kwa ajili ya maslahi yao na kulindana, badala ya kuwatumikia wananchi waliowachagua wakiwemo Wakulima, Wafanyabiashara na Wafanyakazi.

MADIWANI WAGEUKA MBOGO!!!

Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wameilalamikia kamati ya idara ya mipango miji katika Manispaa hiyo kwa kushindwa kusimamia kazi zake vizuri.

Madiwani hao wametoa lawama hizo huku wakilitaka pia baraza la madiwani wa Manispaa hiyo kutoa tamko rasmi la kumuondoa mkuu wa Idara ya Mipango miji katika manispaa hiyo, Christian Mkude na kumtafuta mtu mwingine wa kushika nafasi hiyo kwa madai kuwa aliyopo sasa anashindwa kufanya kazi yake ipasavyo.

Hatua hiyo imefikiwa jana na Madiwani hao katika baraza lao la madiwani mara baada ya kumtaka Mwenyekiti wa kamati ya idara ya mipango miji, Christian Matembo kutoa maelezo ya kushindwa kusimamia vyema mpango wa ujengaji wa barabara kwa kiwango cha lami unaoendelea kufanyika mjini hapa.

Madiwani hao wamedai kuwa barabara zinazoendelea kujengwa mjini hapa kwa kiwango cha lami zipo katika kiwango duni licha ya kutumika fedha nyingi hali ambayo imepelekea kuwepo kwa malalamiko mengi ya wananchi kuhusu barabara hizo.

Golden Sanga Diwani wa Kata ya Bombambili Mjini ameishia kuishutumu kamati pamoja na idara hiyo ya mipango miji kwa kushindwa kusimamia kazi yake ipasavyo huku akiwatupia lawama moja kwa moja watalaamu kwa madai kuwa kazi wanayoifanya haikidhi mahitaji.

Amesema watalaamu wameshindwa kufanya kazi yao kwa ufanisi hali ambayo imesababisha pia barabara zingine mifereji kujengwa juu na barabara ipo chini hali ambayo inasababisha wakati wa mvua maji kupita juu ya barabara badala ya kwenye mifereji.

Akitoa hoja za kujitetea Mwenyekiti wa Kamati ya Idara ya Mipango Miji, Matembo amedai kuwa wanashindwa kufanya kazi yao vizuri kutokana na Mkuu wa Idara hiyo Bwana Mkude kutoshiriki katika mikutano ya baraza hilo la madiwani hivyo kushindwa kushauriana na kufikia muafaka.

Bwana Matembo amesema kila mkutano unapofika mkuu huyo wa idara ya mipango miji amekuwa akimtuma mwakilishi hivyo akaliomba baraza hilo kutamka rasmi kumtafuta mtu mwingine wa kushika nafasi hiyo.

Awali Mhandisi wa Manispaa ya SONGEA, Maximillian Kabairuka amekiri kuwepo kwa mapungufu katika kusimamia miradi hiyo ya barabara huku akilihakikishia baraza hilo kuwa barabara zinazojengwa ni bora na kwamba zitatumika bila kuharibika kwa muda wa zaidi ya miaka 10 hadi 15.

Akifunga baraza hilo la Madiwani, Meya wa Manispaa ya Songea, Gerald Ndimbo amesema baraza hilo linaagiza kuwa barabara hizo zifanyiwe marekebisho ya haraka hadi ifikapo Juni mwaka huu ili ziwe katika kiwango kinachotakiwa vinginevyo itamyang’anya kazi mkandarasi na kumchukulia hatua zaidi.( Habari kwa Hisani ya Emmanuel Msingwa)

Tuesday, May 4, 2010

TORRES KUKOSA MECHI ZA MWANZO ZA WORLD CUP!!!



Mshambuliaji wa Kimataifa wa Spain ambaye anasukuma gozi katika Klabu ya Liverpool Fernando Torres El Nino yupo mashakani iwapo ataweza kucheza mchezo wa kwanza wa Kombe la Dunia. Torres ambaye amefanyiwa operesheni imeelezwa kuwa uwezekano wa yeye kucheza ni mdogo sasa!!

KIKOSI CHA ALGERIA CHA WORLD CUP!!!


Goalkeepers: Lounes Gaouaoui (ASO Chlef), Faouzi Chaouchi (Entente Setif), Mohamed Lamine Zemmamouche (MC Alger), M'bohi Rais Ouheb (Slavia Sofia, Bulgaria)

Defenders: Abdelkader Laifaoui (Entente Setif), Madjid Bougherra (Rangers, Scotland), Carl Medjani (Ajaccio, France), Rafik Halliche (Nacional Madeira, Portugal), Anther Yahia (Bochum, Germany), Habib Belaid (Boulogne-sur-Mer, France), Nadir Belhadj (Portsmouth, England), Djamel Mesbah (Lecce, Italy)

Midfielders: Hassan Yebda (Portsmouth, England), Medhi Lacen (Racing Santander, Spain), Yazid Mansouri (Lorient, France), Adlene Guedioura (on loan at Wolverhampton, England from Charleroi, Belgium), Riad Boudebouz (Sochaux, France), Djamel Abdoun (Nantes, France), Fouad Kadir (Valenciennes, France), Mourad Meghni (Lazio, Italy), Karim Ziani (Wolfsburg, Germany), Karim Matmour (Borussia Moenchengladbach, Germany)

Strikers: Abdelkader Ghezzal (Siena, Italy), Rafik Djebbour (AEK Athens, Greece), Rafik Saifi (Istres, France)

HOTUBA YA RAIS KIKWETE KWA WAZEE!!!

HOTUBA YA MHE. JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, WAKATI AKIZUNGUMZA NA WAZEE WA MKOA WA
DAR ES SALAAM, TAREHE 3 MEI 2010

Mhe. Makamu wa Rais,
Mhe. Waziri Mkuu,
Waheshimiwa Mawaziri,
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa,
Mstahiki Meya,
Viongozi wa Serikali,
Wazee wangu,
Ndugu Wananchi,

Nianze kwa kumshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kuniandalia fursa ya kukutana na Wazee wa Dar es Salaam. Nawashukuru wazee wangu kwa kuitikia wito wangu huu wa kukutana nanyi na nimefarijika sana kwa mahudhurio yenu makubwa. Asanteni sana.

Nimewaiteni wazee wangu nizungumze nanyi mambo mawili na kupitia kwenu nizungumze na wananchi wote wa Tanzania. Jambo la kwanza, linahusu mkutano mkubwa wa kimataifa kuhusu masuala ya uchumi utakaofanyika hapa Dar es Salaam kuanzia keshokutwa tarehe 5 Mei mpaka tarehe 7 Mei. Mkutano huo ulioandaliwa na shirika moja la kimataifa lijukanalo kama World Economic Forum, lenye makao yake makuu nchini Uswisi, unafanyika hapa nchini kwa mara ya kwanza katika historia ya miaka 20 ya mikutano hiyo kufanyika Barani Afrika. Pia ni mara ya kwanza kwa mikutano hiyo kufanyika nje ya Cape Town, Afrika Kusini.

Ndugu zangu, Watanzania Wenzangu,

Hii ni heshima kubwa sana ambayo taifa letu limepewa. Ni kielelezo cha imani kubwa waliyokuwa nayo kwetu, wenzetu kwingineko duniani, kwani zilikuwepo nchi nyingine zilizotaka kuwa wenyeji wa mkutano huu lakini wakaiteua Tanzania. Ni jambo la fahari kwetu lakini ni jambo ambalo pia lina wajibu mkubwa kwetu. Wajibu wenyewe si mwingine bali ni ule wa kuwapokea vizuri na kuwa wakarimu kwa wageni wetu kama ilivyo desturi yetu na sifa yetu Watanzania. Lazima tuhakikishe kuwa wageni wetu wanaondoka nchini wakiwa na kumbukumbu nzuri ya nchi yetu na sisi watu wake.
Ndugu Wananchi,

Mwitikio wa watu kushiriki katika mkutano huu wa Dar es Salaam umekuwa mkubwa sana hata kuwashangaza waandaaji. Wanasema wameshaandaa mikutano hii kwa zaidi ya miaka 50 sasa, lakini hawajapata mwitikio kama huu wa mkutano wa Tanzania. Walikuwa na lengo la kupata washiriki 750, lakini mpaka tarehe 29 Aprili, 2010 washiriki 959 walikuwa wamethibitisha kushiriki na wengine kadhaa wamekosa nafasi. Haya yote ni kielelezo cha kukubalika na kuheshimika kwa nchi yetu kimataifa.

Ndugu Wananchi;

Tunatarajia kupokea Wakuu wa Nchi na Serikali wapatao, 11 na Mawaziri 23 wa kutoka nchi mbalimbali duniani. Aidha, wajumbe kutoka mashirika makubwa ya kimataifa, kama Umoja wa Kimataifa, Benki ya Dunia, WTO n.k. Kuna washiriki kutoka makampuni makubwa, ya kati na madogo ya kimataia na watu binafsi wakiwemo watu mashuhuri duniani. Washiriki wa mkutano huu kwa ujumla wao wanatoka katika mataifa 85 duniani. Katika mikutano hii hufanyika mikutano ya Viongozi Vijana wanaoongozwa na Mwana wa Mfalme wa Norway, Prince Magnus Haakon. Mkutano huo nao umevunja rekodi ya ushiriki, awali walitegemea washiriki 200 lakini washiriki waliothibitisha mpaka sasa ni 350. Kwa sababu ya ugeni mkubwa kiasi hiki, kutatokea usumbufu wa magari kusimamishwa ili kuruhusu misafara ya wageni wetu kupita. Naomba ndugu zangu muelewe hilo na kuwa wavumilivu. Natanguliza kuwataka radhi kwa usumbufu mtakaoupata katika siku tatu za mkutano huu.

Agenda kubwa ya mkutano wa mwaka huu ni kuangalia jinsi ya kurekebisha na kukuza uchumi wa nchi za Afrika baada ya kutikiswa na hali mbaya ya uchumi duniani. Masuala yatakayoongelewa ni pamoja na jinsi ya kuongeza uwekezaji; kukuza uzalishaji na tija kwenye kilimo; uwekezaji kwenye viwanda na uongezaji wa thamani kwenye bidhaa za kilimo; kuendeleza sekta binafsi ili iweze kuchangia kwenye ukuzaji wa uchumi; kuboresha miundombinu; kuendeleza elimu n.k.

Kwa ujumla mkutano huu ambao miaka ya nyuma umekuwa unafanyika Cape Town, Afrika Kusini una faida kwa nchi yetu. Faida kubwa ni kuitangaza nchi yetu na vivutio vyake duniani na hivyo kuwafanya wawekezaji na watalii watambue uwepo wetu. Wapo watakaoijua Tanzania kwa kufika na kujionea wenyewe na wapo watakaoijua nchi yetu kupitia vyombo vya habari ambavyo vitawakilishwa kwa wingi sana. Faida itakayopatikana haraka sana wakati na baada ya mkutano huu ni mahoteli na vyombo vya uchukuzi na maduka nchini kupata kipato kutokana na wageni watakaohudhuria mkutano huu kutumia huduma hizo. Naambiwa karibu wageni wetu wote wa nje watatembelea mbuga za wanyama na visiwa vya Zanzibar baada ya mkutano.


Ndugu Wazee na Viongozi,

Jambo la pili linahusu TUCTA na mgomo. Sikupenda kulizingumzia suala hili, lakini nimelazimika kuzungumza baada ya kuwasikiliza viongozi wa TUCTA wakati wa Maadhimisho ya Sherehe ya Mei Mosi hivi majuzi. Nimewasikia wakirudia kuwashawishi wafanyakazi kugomo kuanzia tarehe 5 Mei, 2010 kwa sababu ati sisi katika Serikali hatusikii wala hatujali maslahi ya wafanyakazi.

Katika hotuba yangu niliyoitoa mwishoni mwa mwezi Machi, 2010, nilielezea kwa kirefu jinsi gani Serikali inavyowathamini na kuwajali wafanyakazi. Nilitaja na kufafanua kwa kina hatua mbalimbali ambazo Serikali imechukua na inazoendelea kuchukua katika kuboresha maslahi ya mfanyakazi. Nilisema kuwa madai ya viongozi wa TUCTA kuwa Serikali hii siyo sikivu na haiwajali wafanyakazi si kweli kwani mema yote tuliyoyafanya kwa wafanyakazi hayangefanyika kama sisi hatusikii wala kujali.

Kadhalika nimeelezea dhamira yetu ya kuongeza mishahara ya wafanyakazi katika bajeti ijayo. Ukweli ni kwamba tangu tuingie madarakani, tumeongeza kima cha chini kwa watumishi wa umma kwa asilimia 62.5 kutoka shilingi 65,000 hadi kufikia shilingi 104,000 hivi sasa.

Nilielezea pia mambo mazuri yaliyofanywa na Serikali kuendeleza maslahi ya wafanyakazi wa sekta binafsi. Taliziunda Bodi nane za kisekta ambazo hazikuwepo kabla ili ziweze kushughulikia kupanga viwango vya mishahara ya kima cha chini kwa wafanyakazi wa sekta binafsi. Kwa ajili hiyo, wafanyakazi wa sekta binafsi wameanza kunufaika kwa mishahara kupanda tangu wale wa mashambani na majumbani mpaka viwandani na kwingineko. Hivi majuzi tena kumetolewa nyongeza nyingine, wapo ambao wametoka kwenye shilingi 45,000 mpaka shilingi 80,000 au hata 150,000, wapo waliotoka kwenye mshahara wa shilingi 48,000 kwa mwezi hadi shilingi 350,000 kwa mwezi mwaka 2009. Bodi hizi zinafikia maamuzi haya kwa kuzingatia uwezo wa sekta binafsi kumudu gharama hizo.

Ndugu Wananchi;

Jambo kubwa nililowaomba viongozi wa TUCTA ni kwamba, katika hotuba ya Machi, 2010 niliwasihi viongozi wa vyama vya wafanyakazi na wafanyakazi kutumia njia ya mazungumzo kwa sababu ilikuwa bado haijatumika na kushindikana. Aidha, nilikumbusha kuwa hata kama watagoma mwishowe watalazimika kurudi mezani kuzungumza, ndipo wapate wanayoyataka. Niliwatahadharisha pia kwamba ni bora kuzungumza sasa kuliko kufanya hivyo baada ya mgomo kwani hujui katika kipindi cha mgomo mambo yatakuwaje. Inawezekana hata mazingira ya kuzungumza yakawa mabaya.

Wazee Wangu;

Napenda kueleza furaha yangu na shukrani zangu kuwa maombi yangu yalikubaliwa na pande zetu tatu zimekuwa zinazungumza tangu wakati ule kwa mujibu wa sheria ya Mahusiano Kazini na Sheria ya Taasisi Kazi. Napenda kusema pia kuwa, mazungumzo yamekwenda vizuri, yapo mambo yaliyokamilika na yapo yanayoendelea kuzungumzwa na naamini nayo yatakamilika. Nadhani mnashangaa kuelezea furaha na kusema yapo mambo yaliyokamilika na kuonesha matumaini kuwa yaliyobakia nayo yatakamailika. Hii ni sahihi kabisa .

Naomba nifafanue kidogo. Tarehe 6 Aprili, 2010 kulifanyika kikao cha Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ambapo TUCTA iliwasilisha rasmi hoja zao zinazowafanya waitishe mgomo wa wafanyakazi wote nchi nzima kuanzia tarehe 5 Mei, 2010. Hoja hizo ziliwasilishwa na kuzungumzwa na kuamuliwa ipasavyo.

a. Madai kuwa Bodi za Kisekta zilikuwa zimemaliza muda wake yalifutwa na TUCTA baada ya kugundua kuwa walikosea tarehe.
b. Kuhusu madai ya kuchelewa kutangazwa kima cha chini nalo halikuwa tatizo la Serikali bali ni LESCO kupata mamlaka ya Bunge.
c. LESCO kutokukutana kwa sababu ya mazungumzo kuchelewa kumalizika ndani ya siku 60, hivyo kibali cha Bunge kilihitajika ambacho kilipatikana Februari, 2010. Kinachosubiriwa sasa ni tarehe ya mazungumzo kupangwa.
d. Ripoti ya Tume ya Ntukamazina kupewa TUCTA; wakaambiwa Tume aliunda Rais imshauri yeye kama wanahitaji ripoti wakamuombe yeye.
e. Kima cha chini kiwe shilingi 315,000/=; wakaambiwa lizungumzwe kwenye baraza husika.
f. Kodi kuwa kubwa mno; wapeleke kwenye Mamlala husika.
g. Ukokotoaji wa malipo ya uzeeni uhuishwe ili ufanane katika mifuko yote. Waliambiwa ili nalo likazungumzwe.

Tarehe 14 Aprili, 2010, LESCO ilikutana kujadili taarifa ya CMA na kuelekeza ipasavyo. Matokeo ya uamuzi wa LESCO ni:-
a. Kukubali mapendekezo ya kima cha chini cha mishahara kwa sekta binafsi na kuelekeza Waziri wa Kazi atangaze kabla ya tarehe 30 Aprili, 2010; Waziri akafanya hivyo, lakini cha ajabu mara baada ya Waziri kutangaza, TUCTA wakamshutumu Waziri Kapuya na kudai hiyo ni danganya toto. Lakini wakati wanafanya hivyo, maamuzi hayo yamefanywa katika vikao ambavyo TUCTA wameshiriki kwa ukamilifu. Waziri si mjumbe wa vikao vyote hivyo, bali yeye ndiye mtanganzaji.
b. Ikaafiki uamuzi wa CMA kuwa suala la kima cha chini cha mshahara wa watumishi wa umma lipelekwe kwenye Baraza la Majadiliano la Pamoja la Utumishi wa Umma kuzungumzwa.

Tarehe 27 Aprili, 2010, kikao cha Baraza hilo kikaitishwa na mazungumzo kuendelea tena tarehe 30 Aprili, 2010. Baada ya kikao cha tarehe 30 Aprili, 2010 walikubaliana wakutane tena tarehe 8 Mei, 2010. Jambo la kustaajabisha, tarehe 1 Mei, wale wale waliokubaliana wakutane tarehe 8 mwezi Mei, wanatoa siku mbili kwa wenzao kutoa majibu na isipofanyika hivyo tarehe 5 mwezi Mei wafanyakazi wote wagome.

Lingine la ajabu ni la viongozi wa TUCTA kuendelea kudai hadharani kima cha chini cha shilingi 315,000/= , wakati siku ya kwanza ya mazungumzo walielezwa ugumu wake, nao wakakubali na kupendekeza kiwango kingine cha chini, ambacho nacho Serikali iliona hakitekelezeki. Hivyo tarehe 30 Aprili, viongozi wa TUCTA wakapendekeza kiwango kipya cha chini zaidi. Upande wa Serikali nao walipendekeza kiwango wanachoamini kuwa mapato yetu yanaweza kumudu. Licha ya mwenendo mzuri wa mazungumzo, bado hakujawa na muafaka kati ya kiwango kipya cha chini walichopendekeza viongozi wa TUCTA na kiwango kilichopendekezwa na Serikali. Kutokana na hali hiyo walikubaliana wakutane tarehe 8 Mei, 2010 kuendelea na mazungumzo.

Ndugu Wananchi;

Iweje tena tarehe 1 Mei, 2010 mtu yule yule anageuka na kuzungumzia kima kile kila cha mwanzo wa mazungumzo na iamuliwe ndani ya siku mbili? Tunayo kila sababu ya kuhoji dhamira zao, wana nia njema kweli wenzetu hawa? Wana hili hili au wana lao jambo lingine?

Kima cha Shilingi 315,000/=

Kima cha chini cha shilingi 315,000/= hakitekelezeki kwa sababu Serikali haitakuwa nazo pesa hizo. Kwa kima hicho, Serikali itatakiwa kutumia shilingi bilioni 6,852.93 kwa mishahara peke yake wakati mapato yanayotarajiwa katika bajeti ijayo ni shilingi bilioni 5,773.1, ambazo zinapaswa kutumika kwa mishahara pamoja na shughuli zingine za kuendesha Serikali na maendeleo. Hivyo basi, italazimika kukopa shilingi bilioni 1,233.52 zaidi ili zitosheleze mahitaji ya mishahara peke yake. Hii haiwezekani kwa sababu Serikali itakuwa haifanyi shughuli nyingine ila kulipa mishahara. Tutakuwa ni watu wa ajabu sana. Huko tutakapokwenda kukopa watatushangaa na tutaonekana kichekezo. Na viongozi wa TUCTA tumewaambia hivyo.

Hata kama ningetaka kuwafurahisha akina mzee Mgaya, kwa jambo hili haiwezekani. Na, kama wanavyodai kwamba watampigia kura kiongozi na chama atakayewapa fedha hizo, kura hizo sisi tunahesabu tumeshazikosa. Ni afadhali kuzikosa kura za akina Mgaya kuliko kuwaumiza wananchi walio wengi kwa kutumia fedha zote za nchi kuwapa akina Mgaya wagawane na kuwakosesha wananchi huduma muhimu. Jambo hili sitalifanya.

Hatutafanya hivyo, kwa vile fedha za Serikali ni za Watanzania wote milioni 40 na siyo kwa ajili ya mishahara ya wafanyakazi 350,000 tu. Ni kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wote kwa ajili ya maendeleo yao. Kuwalipa mishahara wanayodai viongozi wa TUCTA inamaanisha kwamba serikali isitishe kutoa huduma yoyote ile kwa wananchi; madawa hospitalini yasiwepo, ruzuku za mbegu, mbolea na madawa ya kuulia wadudu visiwepo, ujenzi wa majosho, barabara, zahanati, mashule, maji na umemenk usitishwe, shuguli za ulinzi na usalama wa raia pia zisimamishwe. Na wafanyakazi wenyewe wakifika maofisini mwao watakuwa ni watu wa kupiga gumzo tu bila kufanya kazi yoyote kwa sababu hakutakuwapo fedha za kununulia vitendea kazi. Hii haiwezekani. Hii ni sawa na kusema serikali iwe imekufa. Hakuna serikali inaweza kufanya hivyo. Hata hao ambao wanawapigia debe hivi sasa kama wangebahatika kuwa madarakani wasingeweza na hawataweza kamwe kukubali miujiza hii.

Wazee Wangu, Wananchi Wenzangu;

Naomba muelewe ugumu tulionao katika mazungumzo na viongozi wa TUCTA. Hawataki kuwaambia wafanyakazi na wanachama wao ukweli. Viongozi hawa hawana muamana, kwenye majadiliano wanakubaliana jambo moja, wakitoka nje wanasema jingine. Viongozi hawa wanakosa moja ya nguzo muhimu ya uongozi bora. Nguzo ya uongozi bora ni kuwaambia watu unaowaongoza ukweli hata kwa yale mambo wasiyopenda kuyasikia. Hawana sababu ya kuacha kuwaeleza wanachama wao ukweli. Tayari viongozi hao wamekubaliana na Serikali kukutana tarehe 8 Mei. Hawana sababu tena ya kuipa Serikali siku mbili kutekeleza mambo yale yale yaliyopangwa kujadiliwa baina yao na Serikali tarehe 8 Mei.

Uhalali wa Mgomo

Ndugu Wananchi;

Mgomo unaoshinikizhwa na viongozi wa TUCTA ni batili na kinyume cha sheria. Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini (Employment and Labour Relations Act,) No. 6 ya 2004 inaainisha pamoja na mambo mengine utaratibu wa kutatua mizozo na migogoro kazini na haki za mwajiri na mwajiriwa. Utaratibu wa mgomo ulioainishwa katika sheria hiyo, unazingatia maslahi ya wafanyakazi, waajiri pamoja na wananchi. Unatambua umuhimu wa kufanya majadiliano na unasisitiza kwamba huduma muhimu hazipaswi kuathirika kutokana na migomo. Aidha, imetamka kuwapo kiwango fulani cha huduma wakati wa mgomo. Uratatibu huo unaelekeza kwamba mgomo wenyewe utekelezwe kwa kiwango ambacho kitasaidia kutatua tatizo mahsusi lililopo kati ya mwajiri na mwajiriwa. Mambo ya msingi ya kuzingatia ni kwamba kabla mfanyakazi hajagoma, au mwajiri hajaamua kufunga eneo la kazi (lock out) kuwe na majadiliano yatakayofanyika kwa nia njema kati ya mwajiri na mwajiriwa na kwamba majadiliano hayo yawe yameshindwa kutoa suluhisho. Kamishna wa Kazi awe amearifiwa hiyo. Wafanyakazi wasilazimishwe kugoma, badala yake wao wenyewe wawe wameamua kwa ridhaa yao kwa kura, kushiriki katika mgomo.

Bahati mbaya sana mgomo huu uliotangazwa na Chama cha Wafanyakazi siyo halali kabisa. Umeitishwa wakati ambao majadiliano bado yanaendelea. Hawaonyeshi kuwa na nia njema katika majadiliano kwani mambo yanayokubalika kwenye majadiliano ni tofauti na yale wanayowaambia wafanyakazi wao. Pili, wanawalazimisha wafanyakazi wote kushiriki katika mgomo, hata wale ambao sheria inasema kwamba huduma zao ni muhimu hivyo hawatakiwi kugoma. Tatu mgomo wenyewe hauna muda. Nne, viongozi wamejitwalia mamlaka ya kisheria kutangaza mgomo bila kuzihusisha mamlaka za kazi jambo ambalo kwa kweli siyo zuri wala la kistaarabu. Kutokana na kushindwa kutekeleza masharti haya ya Sheria ya Ajira na mahusiano kazini mgomo huu ni kuvunja Sheria za nchi, ni haramu. Hatuwezi kukubali jeuri ya watu wanaovunja sheria za nchi.

Ndugu Wananchi;

Nimalize kwa kutoa ushauri wangu kwa wafanyakazi wa Serikali, wafanyakazi wa sekta binafsi na viongozi wa TUCTA. Kwa wafanyakazi wa Serikali hakuna sababu ya msingi kugoma kwa madai yasiyotekelezeka ya kulipwa kima cha chini cha shilingi 315,000/=. Kwa vile mazungumzo baina ya Serikali na TUCTA bado yanaendelea, hakuna sababu za msingi za kugoma. Kwa vile ni dhahiri kuwa siyo halali. Atakayegoma atakuwa amekiuka taratibu na kanuni za ajira na atachukuliwa hatua kwa mujibu wa taratibu na kanuni za utumishi Serikalini. Na yule ambaye atakwenda kazini lakini ataacha kufanya kazi atachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa taratibu zilizopo.

Kwa wafanyakazi wa sekta binafsi, tumeunda Bodi za kisekta zimeshafanya kazi yake na Waziri wa Kazi ameshatangaza tuzo stahiki kisheria. Tangazo la TUCTA nyie mgome ili mlipwe shilingi 315,000/= linavunja sheria. Msiwasikilize. Mtapoteza ajira zenu na Mgaya hamtamwona. Ndugu zangu mshahara unategemea uwezo wa mwajiri kulipa, usidai kiasi ambacho hawezi kukulipa. Bodi ya Kisekta ndiyo muamuzi kwa mujibu wa sheria. Madai mengine yote nje ya utaratibu huu ni batili.
Changamoto kwa viongozi wa TUCTA, ni kuwa wakweli kwa watu wanaowaongoza na wawe tayari kusema hata yale mambo magumu ambayo wafuasi wao hawapendi kuyasikia.

Ahsanteni Sana kwa Kunisikiliza!
Mungu Ibariki Afrika!
Mungu Ibariki Tanzania!

MANUMBA AGEUKIA MASUALA YA MAZINGIRA!!!

Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai Nchini, Robert Manumba amesema kwamba udhibiti mkubwa wa kisheria unahitajika kutoka vyombo husika katika kupambana na vitendo vya uharibifu wa mazingira.

Kauli hiyo ilitolewa na Manumba jana wakati akizundua ripoti ya utafiti wa uharibifu wa mazingira Tanzania katika warsha ya siku moja uliyofanyika jijini Dar es Salaam.

“Tunahitaji udhibiti mkubwa wa sheria kutoka vyombo husika mfano polisi Takukuru katika kuhakikisha watu wanaovunja sheria za zinazodhibiti utunzaji wa mazingira kuhakikisha kuwa wanakamatwa na kuhukumiwa, ikiwemo upepelezi na uendeshaji mzuri wa kesi,” alisema Manumba.

Mkurungezi huyo amesema hayo baada ya utafiti huo kubaini kwamba vyombo vya kisheria vina upungufu wa uwezo wa kutambua, kuchunguza na kuendesha kesi zinazohusiana makosa ya mazingira.

Manumba ameongeza sekta zinazohusika kupambana na vitendo vya uharibifu wa mazingira, ambavyo ni vyombo vya kisheria,sekta binafsi na jamii zinapaswa kuweka kipaumbele utamaduni wa uratibu na ushirikiano ili kuweza kukabiliana na tatizo hilo.

Ameongeza kwamba binadamu wanapaswa kuyalinda mazingira kwa kuwa ndio yanayowafanya waishi.

Akizungumzia kuhusu warsha hiyo ambayo imeshirikisha wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha DarSalaam(USDM),taasisi zisizo za kiserikali , Ushirikiano wa Polisi Duniani Tawi la Nairobi, wizara za mazingira na idara za serikali alisema itasaidia kutoa mapendekezo na mikakati ya udhibiti wa suala hilo.

Naye Dk. Wilson Kipkore kutoka Taasisi ya Mafunzo ya Usalama,(ISS) alisema utafiti huo umefanyika katika nchi za Tanzania, Kenya,Uganda, Rwanda, Burundi, Sudan, Ehtiopia na Schely, ambapo kila nchi ina ripoti yake, umebaini kuwa ukuaji wa idadi ya watu ni changamoto kubwa katika kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

Amezitaja changamoto nyingine kuwa ni mabadiliko ya hali ya juu ya teknolojia mfano utumiaji wa machine zenye nguvu kubwa na mabadiliko ya hali ya hewa yanayosababishwa na vitendo mbalimbali vya binadamu kama vile uchomaji misitu.

Ameshauri serikali kutoa kuelekeza rasimali za kutosha,ikiwemo rasilimali watu ili kuweza kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

Utafiti huo kwa sasa umefanyika kwa muda wa miaka miwili, lakini unatakiwa kukamilishwa kwa kipindi cha miaka mitatu.

TANGAZO LA TIGO MATATANI!!!

Wajumbe wa kikao cha Bodi ya Barabara wameitaka Kampuni ya simu za Mkononi ya Tigo kusitisha matumizi ya tangazo linalomuonesha mtu anayejisaidia vichakani wakati wa safari ya kwenda Songea wakidai tangazo hilo linaudharirisha Mkoa wa Ruvuma.

Wajumbe hao, wameilaumu kampuni ya tigo kwa kutengenza tangazo lisiloeleza hali halisi kwa kuwa eneo lililowekewa kibao cha Songea halipo Mkoani Ruvuma, wala basi lilitumika halitoi huduma Mkoani Ruvuma.

Pamoja na kuitaka kampuni ya Tigo kusitisha matumizi ya Tangazo hilo, wajumbe hao waliokuwa chini ya Mkuu wa Mkoa Dr Christin Ishengoma wametishia kudai fidia kutoka kampuni ya Tigo endapo itaendelea kulitumia tangazo hilo katika vyombo vya habari vya Luninga.

Tangazo la Kampuni ya simu ya tigo linalolalamikiwa, linaonesha kilometa 250 kabla kufika SONGEA mtu mmoja anaingia vichakani kwa ajili ya kujisaidia, na kisha anaachwa na baada ya kulisimamisha basi hilo kwa kutumia simu.

Aidha wajumbe wa Bodi ya barabara Mkoani Ruvuma wameridhia mpango wa wakala wa barabara Mkoani humo, wa kujenga vituo viwili vya vyoo kati ya Njombe na Songea kwa ajili ya kujisaidia abiria wanaosafiri kutoka na kuingia Mkoani Ruvuma.

Monday, May 3, 2010

MAMBO YA ARDHI!!

Wataalamu wa udongo wa kituo cha Utafiti UYOLE wamebaini kuwa ardhi ya Mkoa wa RUVUMA inakabiliwa na tatizo la upungufu wa madini ya Salfa hali inayochangia kuzorota kwa ustawi wa mazao hususani mahindi.

Matokeo ya Uchunguzi wa ardhi ya Mkoa wa RUVUMA yanakuja ikiwa ni miaka kumi tangu Mkoa huo upige marufuku matumizi ya Mbolea aina ya SA ambayo ina kiasi kikubwa cha madini ya salfa.

Athari za ardhi ya Mkoa wa Ruvuma kupungukiwa madini ya Salfa zimeathiri zaidi uzalishaji wa Zao la Mahindi, ambapo sasa wakulima wanashindwa kufikia rekodi ya kuzalisha magunia 25 hadi 30 ya mahindi, hali iliyowalazimu wataalamu kutoka kituo cha Utafiti wa Udongo Uyole kuendesha utifiti shirikishi katika vijiji vitatu vya wilaya ya Mbinga Mkoani Humo.

Afisa kilimo wa Mkoa wa RUVUMA amekiri kuwepo malalamiko ya wakulima juu ya kupigwa marufuku matumizi ya Mbolea ya SA, lakini akajitetea kuwa Mkoa ulishaagiza wilaya zipime ardhi upya na kutoa ushauri, agizo ambalo utekelezaji wake unasuasua

Pamoja ardhi ya Ruvuma kupungukiwa madini ya Salfa, Utifiti wa Uyole pia umebaini kuwa kuna upungufu wa Madini ya Nitrogen, Phosphoras, na Calcium (Habari kwa Hisani ya Gerson Msigwa)

WAAFRIKA AMBAO WANATAMBA INTER MILAN!!




Hawa ni wachezaji ambao wanambeba Jose Antonio Mourinho katika Klabu ya Inter Milan ambayo inausaka Ubingwa wa Italy pamoja na Kombe la Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya. Wachezaji hawa ni Mshambuliaji wa Kimataifa wa Cameroon Samuel Etoo Fils,Kiungo wa Kimataifa wa Ghana (Black Stars) Sulley Ally Muntari na Kiungo wa Kenya McDonald Mariga.

Sunday, May 2, 2010

UBINGWA ENGLAND BADOOO!!!



Chelsea wakati ikiifunga kwa urahisi Liverpool kwa magoli 2-0, Manchester United nayo yashinda kwa 1-0 mbele ya Sunderland. Haya yetu macho na masikio tu!!!

Saturday, May 1, 2010

SOUTH KOREA WATAJA KIKOSI CHA WORLD CUP!!!

Kim Young-Kwang (Ulsan), Lee Woon-Jae (Suwon), Jung Sung-Ryong (Seongnam); Kang Min-Soo (Suwon), Kwak Tae-Hwi (Kyoto), Kim Dong-Jin (Ulsan), Kim Hyung-Il (Pohang), Oh Beom-Seok (Ulsan), Lee Young-Pyo (Al Hilal), Lee Jung-Soo (Kashima Antlers), Hwang Jae-Won (Pohang), Cho Won-Hee (Suwon Bluewings - on loan from Wigan), Cha Du-Ri (SC Freiburg), Cho Yong-Hyung (Jeju); Koo Ja-Cheol (Jeju), Ki Sung-Yong (Celtic), Kim Bo-Kyung (Oita), Kim Nam-Il (Tom Tomsk), Shin Hung-Min (Pohang), Kim Jae-Sung (Pohang), Kim Jung-Woo (Gwangju), Lee Chung-Yong (Bolton), Kim Chi-Woo (Seoul), Park Ji-Sung (Manchester United); Park Ju-Young (AS Monaco), Ahn Jung-Hwan (Dalian Shide), Lee Seung-Ryul (Seoul), Yeom Ki-Hun (Suwon), Lee Keun-Ho (Jubilo Iwata), Lee Dong-Guk (Jeonbuk)

KIKOSI CHA BAFANA BAFANA WORLD CUP!!!

Goal Keepers: Itumeleng Khune (Kaizer Chiefs), Shu-Aib Walters (Maritzburg United), Rowen Fernandez (Arminia Bielefeld, Germany), Moeneeb Joseph (Orlando Pirates).

Defenders: Matthew Booth (Mamelodi Sundowns), Siboniso Gaxa (Mamelodi Sundowns), Innocent Mdledle (Mamelodi Sundowns), Bongani Khumalo (Supersport United), Tsepo Masilela (Maccabi Haifa, Israel), Aaron Mokoena (Portsmouth, England), Bryce Moon (PAOK, Greece), Anele Ngcongca (Racing Genk, Belgium), Siyabonga Sangweni (Golden Arrows Lucas Thwala (Orlando Pirates).

Midfielders: Surprise Moriri (Mamelodi Sundowns), Franklin Cale (Mamelodi Sundowns), Lance Davids (Ajax Cape Town), Kagisho Dikgacoi (Fulham, England), Andile Jali (Orlando Pirates), Teko Modise (Orlando Pirates), Reneilwe Letsholonyane (Kaizer Chiefs), Siphiwe Tshabalala (Kaizer Chiefs), Thanduyise Khuboni (Golden Arrows), (Steven Pienaar (Everton, England), Macbeth Sibaya (Rubin Kazan, Russia).

Strikers: Benni McCarthy (West Ham United, England), Katlego Mphela (Mamelodi Sundowns), Siyabonga Nomvete (Moroka Swallows), Bernard Parker (FC Twente, Holland).

WAKULIMA TUNDURU WALILIA SOKO!!

WAKULIMA wa Halmashauri ya wilaya ya TUNDURU, Mkoa wa RUVUMA, wameiomba serikali wilayani humo kuhakikisha inawafungulia maghulio kwa ajili ya kuuzia mazao yao ili kuepukana na wafanyabiashara matapeli ambao huwanyonya.

Wamesema kumeibuka wimbi kubwa la wafanyabiashara matapeli ambao huzunguka vijijini kuwarubuni wakulima na kisha kuununua mazao yao kwa bei ya chini tofauti na jasho wanalotumia katika kilimo chao.

Wakulima hao wamelazimika kutoa kilio chao hicho kwa mkuu wa mkoa wa RUVUMA , Bi CHRISTINE ISHENGOMA, wakati akiwakabidhi wakulima hao trekta ndogo za kulimia 62 zenye thamani ya zaidi ya milioni 360.

Bi ISHENGOMA amekabidhi trekta hizo kwa wakulima hao tayari kwa shughuli za kilimo ikiwa ni mkakati wa halmashauri hiyo kuondokana na kilimo cha jembe la mkono kutoka asilimia 0.8 sasa hadi kufikia ailimia 15 ifikapo Juni 2011 ili kuongeza tija ya uzalishaji mazao na kukuza kipato chao.

Pamoja na kuwatoa hofu wakulima hao kuondoa mashaka kuhusu uhakika wa kuuza mazao yao , Bi ISHENGOMA amewataka wakulima wilayani humo kuhakikisha wanazitumia trekta hizo katika shughuli za kilimo pekee na siyo kubebea abiria.

Amesema trekta hizo zitasaidia katika kuongeza tija ya uzalishaji mazao na kwamba mkoa huo katika kipindi cha mwaka 2009/2010 imevuna mazao ya chakula na biashara tani 983,883 sawa na asilimia 93.6 ya matarajio ya kuzalisha mazao tani 1,506,520.

Awali kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya TUNDURU, Bi MARY DING’HOI amesema gharama ya trekta moja dukani ni milioni 6.5 lakini halmashauri inamchangia mkulima asilimia 80 na hivyo mkulima anapaswa kuchangia asilimia 20 iluyobakia ambayo ni sawa na sh. milioni 1.3.

Amebainisha kuwa msimu huu wameagiza trekta 64 na kwamba zingine 75 zimeshapata mzabuni wa kuzifikisha hadi Tunduru tayari kwa kugawiwa kwa wakulima. ( Habari kwa Hisani ya Emmanuel Msigwa)