Thursday, February 9, 2012

ZAMBIA NA IVORY COAST USO KWA USO FAINALI AFCON!!!



Timu ya Taifa Zambia maarufu kama Chipolopolo inatarajiwa kupambana na Ivory Coast maarufu kama Tembo baada ya timu hizo kushinda michezo yake ya Nusu Fainali!! Zambia walifanikiwa kuiondosha Ghana maarufu kama Black Stars kwa goli moja kwa nunge goli la kwake Emmanuel Mayuka!! Ivory Coast wakawaondosha Mali maarufu kama Eagles kwa goli moja la kwake Gervais Yao Kouassi Gervinho!!! Mchezo wa kusaka nafasi ya Mshindi wa Tatu ni kati ya Mali dhidi ya Ghana siku ya jumamosi!! Fainali itapigwa siku ya jumapili!!!

No comments:

Post a Comment