Thursday, February 25, 2010

MKUTANO WA MAAFISA WAKUU WA JESHI LA POLISI WAFUNGWA!!!

Serikali imeliagiza Jeshi la Polisi kuhakikisha linadhibiti mapema wimbi la uhalifu na kuimarisha nidhamu kwa askari kuondokana na vitendo vya rushwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani Mbarak Abdulwakili ametoa rai hiyo wakati akifunga mkutano wa Maafisa Wakuu wa Jeshi la Polisi uliokuwa ukifanyika kwenye ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa, Mjini Dodoma.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Inspekta Jenerali Saidi Mwema, amesema mkutano huo ambao ulikuwa ukiwashirikisha Makamanda wa Polisi wa Mikoa na Vikosi, umejadili na kuweka mikakati ya kukabiliana na uhalifu ukiwemo wa vitendo vya kudai na kupokea rushwa.

Akizungumzia matarajio ya taifa kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwishoni mwa mwaka huu, IGP Mwema amewaondolea hofu wananchi kuwa jeshi la polisi litahakikisha kuwa uchaguzi huo unakuwa huru na wa haki.

Katika maazimio yao makamanda hao wamesema kuwa, watatoa elimu kwa wamiliki binafsi wa Mbwa na Farasi ili watumike kama walinzi wasaidizi.

No comments:

Post a Comment