Thursday, February 25, 2010

ANDERSON WA MAN UTD NJE MSIMU MZIMA!!!



Kiungo wa Kimatifa wa Brazil ambaye anakipiga katika Klabu ya Manchester United Anderson anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa kipindi chote cha msimu kilichosalia kutokana na maumivu ya mguu aliyoyapata. Kocha wa Man Utd Sir Alex Ferguson amesema maumivu aliyoyapata Anderson katika mchezo dhidi ya West Ham United ni makubwa na inawezekana akakosa Mchuano wa Kombe la Dunia baadaye mwaka huu.

No comments:

Post a Comment