Wednesday, February 24, 2010

MADAI YA PENSHENI KWA WAZEE WA MBINGA!!!

Wazee wa Wilaya ya MBINGA Mkoani RUVUMA wameanza harakati za kuishinikiza serikali kutoa Pensheni kwa wazee wote wa Tanzania bila kujali kama waliajiriwa katika sekta ya umma ama hawakuajiriwa.

Katika harakati hizo wazee hao wameunda kikundi kazi ambacho kitawatembelea wazee wote wa wilaya hiyo, na baadaye kuunda Mtandao wa Mkoa Mzima wa RUVUMA ambao pamoja na kuwaunganisha wazee wote, utatoa shinikizo kwa serikali ili wazee wote wapate Pensheni.

Akizungumza na Baadaya ya warsha ya siku mbili iliyofanyika katika wilaya ya MBINGA Mkoani RUVUMA, Meneja miradi wa shirika la Help Age International Bw SMART DANIEL amesema pensheni ni haki ya msingi ya kila mzee, ambaye amelitumikia taifa la Tanzania bila kujali kama ameajiriwa ama hajaajiriwa.

Amesema zaidi ya wazee milioni waliopo hapa nchini ni asilimia 4 ndio wanaopata Pensheni, huku wengine wote wakitapatapa kwa maisha ya taabu na fedheha kutokana na kukosa kipato.

Nae Mzee Maarufu wa Mkoani RUVUMA Mzee MUSTAFA SONGAMBELE amesema Serikali ikitekeleza mpango huo wa kutoa Pensheni kwa wazee wote wa Tanzania itakuwa imewasaidia watoto na wajukuu wao, yakiwemo makundi maalumu kama vile watoto yatima ambao tafiti zimeonesha kwa asilimia 50 wanalelewa na wazee.(Habari kwa hisani ya Gerson Msigwa)

No comments:

Post a Comment