Sunday, January 1, 2012

MANCHESTER CITY YAAMBULIA KICHAPO STADIUM OF LIGHT!!!



Vinara wa Ligi Kuu Nchini Uingereza Klabu ya Manchester City imeambulia kichapo cha goli 1-0 mbele ya Sunderland katika mchezo uliopigwa huko Stadium Of Light!! Goli la Ji Dong-Won ndilo lilipeleka kilio kwa Klabu ya Man City na hivyo kushindwa kuongeza tofauti ya pointi kileleni!!

MWADHAMA POLYCARP KARDINALI PENGO AKANUSHA KUFANYA BIASHARA YA MIHADARATI!!!


Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, amesema yeye si mfanyabiashara wa dawa za kulevya ila anatajwa kwa nia ya kunyamazishwa asizungumze ukweli.

Kardinali Pengo akizungumza na vijana katika ufukwe wa Bahari ya Hindi eneo la Kawe jana alisema hajapata kuona wala kujua dawa za kulevya, lakini anajua anatajwa hivyo na wanaotaka anyamaze.

“Mimi mwenyewe nimewekwa katika orodha ya dawa za kulevya, naona kwenye vyombo vya habari, dawa zenyewe wala zisijui, lakini naendelea kuzungumza kwa sababu najua yanafanywa na wanaotaka kuninyamazisha … sitanyamaza ng’o,” alisema Pengo.

Alikuwa akiwaeleza vijana kuhusu utandawazi na kuwataka waache kuyumbishwa na kuamini kila wanachoona kimeandikwa kwenye mtandao.

Alisema mambo mengi ya ajabu yamekuwa yakiandikwa na kusemwa, lengo ikiwa ni kunyamazisha maaskofu na mapadri wasiendelee kufundisha ukweli, ili watu wachache wafaidike.

“Ni uzushi unaofanywa na watu kuharibu na kuchimbachimba Kanisa tusiseme ukweli, wachache waendelee kufaidika, naomba vijana msisombwe na hali hii, kwani watu hawa hawana woga ili mradi lengo lao la kuharibu Kanisa lifanikiwe … vijana mna uhai
ndani yenu na mna uwezo kama maaskari wa kupambana na waovu wa Kanisa,” alisema.

“Silaha ya vijana ni maisha yanayojua mnaamini kitu gani, msikubali kuyumbishwa na watu wanaotoa mambo vichwani mwao. Kama mnasikia natajwa, njooni mniulize, Baba mbona nimesikia habari fulani, badala ya kuyabeba na kushabikia…imani yenu si ya kutetereka, endeleeni kuwa imara watetereke wanaotaka tutetereke,” alisema.

Alisema vijana pia wamekuwa wakitumika kama vyombo katika biashara ya kulevya huku watu wachache wakitajirika na kwamba baadhi yao wanaokemea au kuzungumzia, wanapuuzwa au kuambiwa ndio wafanyabiashara wa dawa hizo, jambo ambalo nyuma yake halina ukweli wowote.

Kardinali Pengo alisema lengo ni kutaka kuwanyamazisha watu wanaosema ukweli ili wachache waendelee kutajirika na biashara hiyo kwa kuwatia hasara vijana.

Naye Mhashamu Askofu Salutaris Libena, ambaye aliongoza Ibada Takatifu, alisema vijana wamekutana ili kumshukuru Mungu na kumwomba neema .

Libena ambaye pia ni Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, aliwataka vijana kuingia mwaka mpya kwa kumjua na kumtukuza Mungu.

Mbali na vijana kushiriki ibada hiyo lakini pia zilikuwapo burudani mbalimbali za kwaya na ngoma, sambamba na vijana kupima kwa hiari damu kwa ajili ya Mpango wa Taifa wa Damu Salama.

Kila mwisho wa mwaka vijana kutoka makanisa mbalimbali ya Kanisa Katoliki hukutana kwa lengo la kumtukuza Mungu na kumshukuru kwa kumaliza mwaka.

Friday, December 30, 2011

BALOZI OMBENI YOHANA SEFUE ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI!!!


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Ombeni Yohana Sefue kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Balozi Sefue anachukua nafasi inayoachwa wazi na Bwana Phillemon Luhanjo ambaye anahitimisha mkataba wake wa utumishi wa umma kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011.

Kabla ya uteuzi wake, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York, Marekani. Kabla ya hapo, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada tokea Oktoba 2005.

Balozi Sefue ataapishwa kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011 saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
30 Desemba, 2011

Thursday, December 29, 2011

PIGO KWA TASNIA YA HABARI TANZANIA JOHN NGAYHOMA AFARIKI DUNIA!!!


Mtangazaji wa zamani wa ITV/Radio One na Shirika la Utanagazaji la Uingereza BBC Kiswahili John Ngahyoma amefariki dunia mapema asubuhi ya leo!! Ngahyoma amefikwa na mauti akiwa Hospital ambako alikuwa anapatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefuna hata kulazimika kupekwa nchini India kwa matibabu lakini haikusaidia!! Kifo cha Ngahyoma kimekuja wakati Tasnia ya Habari ikiwa imepata pigo kubwa la kuondokewa na mwandishi wa Tbc Halima Mchuka!! Blogu hii imepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo hicho!! Mwenyezimungu aiweke roho yake mahali panapostahili!! Ameen!!

RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA HALIMA MCHUKA!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bwana Clement Mshana, kuomboleza kifo cha mtangazaji maarufu wa shirika hilo, Bi Halima Mohammed Mchuka ambaye alifariki dunia usiku wa kuamkia leo, Alhamisi, Desemba 29, 2011 kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.

“Nimepokea kwa huzuni habari za kifo cha Halima Mohammed Mchuka. Nakutumia wewe Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) salamu za dhati ya moyo wangu kuomboleza kifo chake. Nakuomba, kupitia kwako, uniwasilishie salamu zangu kwa wafanyakazi wenzake katika TBC ambao wamempoteza mwenzao na rafiki yao.”

Ameongeza Mheshimiwa Rais katika salamu zake, “Aidha, nataka kupitia kwako niwatumie salamu zangu za rambirambi wana-familia, ndugu na jamaa wote za marehemu. Wajulishe kuwa niko nao katika wakati huu wa maombolezo na kwamba msiba wao ni msiba wangu pia. Nawaomba wawe na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu kwa sababu yote ni mapenzi ya Mungu. Naungana nao kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, ailaze pema peponi roho ya marehemu. Amen.”

Mheshimiwa Rais pia amesema kuwa Bi. Mchuka ametoa mchango mkubwa katika nyanja ya utangazaji nchini. “Sote tutaendelea kukumbuka weledi wake, uzalendo wake na ujasiri wake katika utangazaji uliomsukuma kuwa Mwanamke wa Kwanza katika Tanzania kutangaza mechi za mpira wa miguu”.

Ameongeza Rais Kikwete: “Ni dhahiri kuwa nyanja ya utangazaji imeondokewa na mtu muhimu na namna nzuri zaidi ya kumuenzi Bi. Mchuka ni kwa watangazaji waliobakia kuendelea kuiga mfano wake katika ubora wa utangazaji nchini mwetu.”

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Desemba, 2011

NGOMA MPYA YA TID INAITWA HANITAKI!!

MATUKIO YALIYOTOKEA KWENYE MAHAKAMA YA ICTR-ARUSHA!!!

Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) inaweza kusherehekea mwisho wa mwaka 2011 kwa kujivuna kutokana na hukumu nzito na nyingi zilizotolewa katika mwaka huo.

Mahakama hiyo imetoa jumla ya hukumu 10 katika ngazi zote mbili za mahakama ya awali na mahakama yake ya Rufaa zenye kuhusisha watu 21, akiwemo mwanamke pekee kuwahi kushitakiwa na mahakama hiyo, Pauline Nyiramasuhuko na mtu anayesadikiwa kuwa mpangaji mkuu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994,Kanali Theoneste Bagosora.

Hukumu za ICTR 2011

Gatete ahukumiwa kifungo cha maisha: Machi 29, 2011, ICTR ilianza mwaka mpya kwa kutoa hukumu yake ya kwanza katika kesi inayomkabili aliyekuwa afisa mwandamizi wa serikali ya Rwanda, Jean-Baptiste Gatete ambaye alitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari na kuteketeza kizazi. Alipewa adhabu ya kifungo cha maisha jela na kesi hiyo sasa iko mahakama ya Rufaa.

Aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi ahukumiwa kifungo cha miaka 30: Mei 17, 2011, Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ilitoa hukumu nyingine nzito katika kesi inayohusisha maafisa wanne wa zamani wa jeshi la Rwanda wakiwemo Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi hilo , Jenerali Augustin Bizimungu na Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Polisi, Jenerali Augustin Ndindiliyimana.Majenerali hao walitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Bizimungu alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela huku mwenzake, Ndindiliyimana alipewa adhabu ya muda aliokwisha tumikia akiwa kizuizini tangu mwaka 2000.Aliachiwa huru mara moja.

Maafisa wengine waliotiwa hatiani ni pamoja na Mkuu wa Bataliani ya Usalama Jesheni, Meja Francois-Xavier Nzuwonemeye na Kapteni Innocent Sagahutu pia wa Bataliani hiyo ambao walipewa kila mmoja wao adhabu za vifungo vya miaka 20 jela baada ya kutiwa hatiani kwa uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Pande zote mbili za mwendesha mashitaka na utetezi zimekata rufaa.

Mwanamke pekee na wengine watano watiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari: Juni 24, 2011 ilikuwa siku ya pekee katika historia ya ICTR kwa kutoa hukumu ya kesi iliyokuwa na watuhumiwa wengi zaidi kuliko kesi yoyote katika mahakama hiyo.Kesi hiyo maarufu kwa jina la Kesi ya Butare, inajumuisha watuhumiwa sita akiwemo mwanamke pekee, Pauline Nyiramasuhuko, Waziri wa zamani wa Familia na Masuala ya Wanawake na mtoto wake wa kiume, Arsene Shalom Ntahobali. Wawili hao walihukumiwa vifungo vya maisha jela baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu ukiwemo ubakaji na kuteketeza kizazi na uhalifu wa kivita.

Wengine waliotiwa hatiani katika kesi hiyo ni pamoja na Eli Ndayambaje, aliyehukumiwa pia kifungo cha maisha jela, Alphonse Nteziryayo, alipewa adhabu ya kifungo cha miaka 30, Sylvain Nsabimana atatumikia miaka 25 jela ambapo Joseph Kanyabashi alipewa adhabu ya miaka 35 jela. Wote sita wanasubiri tarehe ya kusikilizwa kwa rufaa zao.

Mawaziri wawili waachiwa huru na wengine wawili watiwa hatiani: Septemba 30, 2011, hukumu nyingine ilitolewa katika kesi inayohusisha mawaziri wanne wa zamani wa Rwanda katika serikali ya mpito ya mwaka 1994. Mahakama iliwaachia huru mawaziri wawili ikiwa ni pamoja na Casimir Bizimungu (Afya) na Jerome Bicamumpka (Mambo ya Nje). Waliotiwa hatiani ni Justin Mugenzi (Biashara) na Prosper Mugiraneza (Utumishi wa Umma) ambao kila mmoja wao alipewa adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kula njama za kufanya mauaji ya kimbari na uchohezi.Kama ilivyokuwa kwa wote waliotiwa hatiani nao wamekata rufaa kupinga hukumu hiyo.

Meya wa zamani ahukumiwa kifungo cha miaka 15 jela: Novemba 17, 2011 Mahakama pia ilitoa hukumu nyingine katika kesi ya meya wa zamani nchini Rwanda, Gregoire Ndahimana. Alitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari na ukatili dhidi ya binadamu na kuhukumiwa adhabu ya kifungio cha miaka 15.Anasubiri kupangiwa tarehe ya kusikilizwa rufaa yake.

Wanasiasa vigogo wawili wa Rwanda kutumikia jela maisha: Desemba 21, 2011 ICTR ilitoa hukumu ya mwisho kwa mwaka huu katika kesi ya wanasiasa wawili wa kilichokuwa chama tawala cha MRND wakati wa mauaji ya kimbari ikiwa ni pamoja na Rais wa chama hicho Mathieu Ngirumpatse na Makamu wake, Edouard Karemera.Walitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita. Walipatikana na hatia hususa ni kwa sababu ya nafasi yao kama viongozi wa juu wa chama hicho kwa kushindwa kuwazuia wala kuwaadhibu wanamgambo wa chama chao maarufu kama Interahamwe waliokuwa wanashiriki katika mauaji ya kimbari.

Hukumu za Mahakama ya Rufaa

Luteni Kanali Muvunyi kuendelea kutumikia miaka 15 jela: Aprili 1, 2011, Mahakama ya Rufaa ya Mahakama ya ICTR, ilithibitisha adhabu ya kifungo cha miaka 15 jela aliyopewa afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda Luteni Kanali Tharcisse Muvunyi. Afisa huyo aliyekuwa katika Chuo cha Maafisa wa Jeshi Wasiokuwa na Kamisheni (ESO) alitiwa hatiani kwa uchochezi wa mauaji ya kimbari katika hotuba yake aliyoitoa Kusini mwa Rwanda wakati wa mauaji ya kimbari mwaka 1994.

Luteni Kanali Setako kuendelea kutumikia miaka 25 jela: Septemba 28, 2011 Mahakama ya Rufaa pia ilithitisha adhabu ya kifungo cha miaka 25 jela aliyopewa aliyekuwa afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda, Luteni Kanali Ephrem Setako baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.

Maafisa wawili waandamizi wa zamani wa jeshi wanusurika vifungo vya maisha: Desemba 14, 2011, Mahakama ya Rufaa ilipunguza hadi miaka 35 jela adhabu ya kifungo cha maisha aliyopewa mtu anayesadikiwa kuwa alikuwa mpangaji mkuu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda Kanali Theoneste Bagosora baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari,uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Katika mahakama hiyo pia tarehe hiyohiyo ilimpunguzia afisa mwingine adhabu kama hiyo ya kifungo cha maisha jela hadi miaka 15, afisa mwingine wa jeshi, Luteni Kanali Anatole Nsengiyumva. Kwa kuzingatia muda aliokwishatumikia akiwa kizuizini tangu atiwe mbaroni, mahakama iliamuru kuachiwa huru mara moja.

Kesi ya mtuhumiwa wa ICTR kusikilizwa Rwanda kwa mara ya kwanza: Desemba 16, 2011, Mahakama ya Rufaa ilitoa uamuzi wa kihistoria kwa kuruhusu kesi ya mchungaji Jean Uwikinkindi kwenda kusikilizwa nchini Rwanda.Mahakama mapema ilitupilia mbali rufaa ya mtuhumiwa huyo kupinga uamuzi wa mahakama ya awali ulioamuru kesi hiyo kwenda kusikilizwa nchini Rwanda Juni 28, 2011. Umuazi huo unafungua njia kwa kesi nyingine za watuhumiwa wa ICTR kupelekwa kusikilizwa nchini Rwanda.

Matukio mengine muhimu ICTR

Uchaguzi wa Rais na Makamu wake ICTR: Jaji mwanamke, raia wa Pakistani, Khalida Rachid Khan alichanguliwa kuwa Rais wa ICTR,kuanzia Mei 27, 2011 kwa kipindi cha miaka miwili. Jaji Khan ambaye alikuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama namba III alikuwa Makamu wa Rais wa ICTR tangu Mei 29, 2007. Wakati hohuo, Rais huyo alitangaza Agosti 24, 2011 kwamba Jaji Vagn Joenson kutoka Denmark aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa ICTR. Jaji huyo alianza rasmi kazi hiyo Agosti 26, 2011.

Kuachiwa mapema mfungwa wa mauaji ya kimbari: Mfungwa wa mauaji ya kimbari, Michel Bagaragaza, aliachiwa toka gerezani nchini Sweden alikokuwa anatumikia adhabu ya kifungo cha miaka nane jela baada ya kutumikia tayari theluthi mbili ya adhabu hiyo iliyotolewa na ICTR kwa kula njama za kufanya mauaji ya kimbari.Hii ni mara ya kwanza kwa Mahakama hiyo ya Umoja wa Mtaifa kuruhusu mmoja wa wafungwa wake kutoka jela kabla ya muda wa adhabu uliotolewa kumalizika. Bagaragaza alikuwa Mkuu wa Mamlaka ya Chai nchini Rwanda.

Wito kwa mataifa kupokea wanaoachiwa huru ICTR: Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limezitaka nchi wanachama wa umoja huo kuwapokea watuhumiwa wanaoachiwa huru na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) na kuendelea kubaki chini ya uangalizi wa mahakama hiyo. Wapo watuhumiwa watano waliokwishaachiwa huru lakini bado wanatafuta nchi za kuwapokea.

TFF YATOA RAMBIRAMBI MSIBA WA MCHEZAJI WA ZAMANI WA TAIFA STARS RASHID MOYO!!!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 29, 2011

RAMBIRAMBI MSIBA WA RASHID MOYO

Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa, Rashid Moyo kilichotokea usiku wa Desemba 25 mwaka huu kwao Msambweni, Tanga.

Moyo ambaye aliichezea timu ya Taifa kwenye miaka ya 70 alizikwa Desemba 26 mwaka huu kwenye makaburi ya Mabawa mkoani Tanga. Pia alikuwa mchezaji wa timu ya Coastal Union ya mkoa wa Tanga.

Msiba huo ni pigo kwa familia ya Moyo, TFF na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango alioutoa kwa Tanzania hasa wakati akiwa mchezaji.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Moyo, Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tanga (TRFA) na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki cha msiba huo mzito. Pia TFF itatoa ubani wa sh. 100,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.

Mungu aiweke roho ya marehemu Rashid Moyo mahali pema peponi. Amina

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MTANGAZAJI WA TBC HALIMA MCHUKA AFARIKI DUNIA!!


Mtangazaji Mahiri wa Mpira katika Eneo la Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Mwanamke wa Kwanza Halima Mchuka amefariki Dunia akiwa anahudumu katika Redio Tanzania Dar es Salaam RTD na baadae Shirika la Utangazaji Tanzania (SHIUTA) amefariki Dunia.

Mchuka amefariki usiku wa kumkia leo kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda ambapo kwa sasa inaelezwa alikuwa anaanza kupata nafuu baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mtangazaji Halima Mchuka alijiunga na Radio Tanzania Dar es Salaam mwaka 1994 ambapo alifanya kazi katika Idara ya Habari na Idara ya mipango.

Mungu ailaze Roho ya BI Halima Mchuka pahala pema peponi Amina

Wednesday, December 28, 2011

KIONGOZI WA KOREA KASKAZINI KIM JONG IL AZIKWA!!


Kiongozi wa zamani wa Korea Kaskazini Kim Jong Il amezikwa leo kwenye mazishi ambayo yameongozwa na mwanaye Kim Jong Un huku kukiwa hakuna kiongozi yoyote kutoka mataifa mengine ambaye amehudhuria maziko hayo!! Maelfu ya wananchi wa Korea Kaskazini wameshiriki kwenye shughuli hizo huku weni wao wakiomboleza kwa kilio!!

Tuesday, December 27, 2011

ARSENAL YABANWA MBAVU EMIRATES NA KUAMBULIA SARE!!



Klabu ya Arsenal maarufu kama Washika Magobole waJiji la London wamebanwa mbavu katika mchezo wa Ligi Kuu Nchini England baada ya kuambulia sare ya bao 1-1 mbele ya Wolves!! Kutokana na matokeo hayo Klabu ya Arsenal imeendelea kujiweka mbali na mbio za Ubingwa msimu huu!!

JONNY EVANS KUKAA NJE KWA MAJUMA MAWILI!!


Kocha Mkuu wa Manachester United Sir Alex Ferguson amesema watamkosa Beki wao wa kati Jonny Evans kwa majuma mawili hadi matatu na hivyo kumfanya kuwa na majeruhi kumi na moja wa kikosi chake!! Evans aliumia kwenye mchezo dhidi ya Wigan Athletic uliopigwa hiyo jana!! Wachezaji wengine ambao ni majeruhi kwa sasa ni Nemanja Vidic, Darren Fletcher, Rio Ferdinand, Michael Owen, Anderson, Tom Cleverley, Fabio Da Silva, Phil Jones, Ashley Young na Chris Smalling!!

TAHADHARI YA KUIBUKA KWA MAFURIKO TENA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM!!

Monday, December 26, 2011

MAN UTD YASHINDA HUKU LIVERPOOL, CHELSEA NA MAN CITY ZIKIBANWA MBAVU!!






Ligi Kuu nchini Uingereza imeendelea na kushuhudia Manchester United ikifanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 5-0 na kuikaribia Manchester City kilele baada ya timu hiyo kulazimishwa sare ya bila kufungana na Wes Bromwich Albion!! Chelsea walikwenda sare ya goli 1-1 mbele ya Fulham wakati Liverpool walibanwa mbavu na Blackburn Rovers baada ya kutoka sare ya goli 1-1!!

Wednesday, December 21, 2011

MANCHESTER UNITED NA CITY WAKABANA KOO LIGI KUU NCHINI UINGEREZA!!





Manchester Unite imevuna ushidni wa magoli 5-0 mbele ya Fulham wakati Manchester City wakiisambaratisha Stoke City kwa magoli 3-0!! Arsenal nayo iliendelea kuvuna ushindi baada ya kuifunga Aston Villa kwa magoli 2-1!! Newcastle United imeendelea na wakati mgumu baada ya kufunga magoli 3-2 na West Bromwich Albion!! Everton ilishinda kwa goli 1-0 mbele ya Swansea huku Wigan wakitoka sare tasa na Liverpool huku QPR wakipata kichapo cha nyumbani mbele ya Sunderland!!

RAIS KIKWETE ATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA WALIOFIKWA NA VIFO KUTOKANA NA MAFURIKO DSM!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Said Meck Sadiq kuomboleza vifo vya watu 13 ambao wamepoteza maisha katika mafuriko makubwa yaliyotokana na mvua ambazo zimekuwa zinanyesha tokea Jumanne, Desemba 20, 2011.

Aidha, Rais Kikwete amempa pole Mkuu huyo wa Mkoa kutokana na uharibifu mkubwa wa nyumba, makazi na mali nyingine za wananchi uliosababishwa na mvua hizo ambazo pia zimesababisha uharibifu wa miundombinu.

Rais Kikwete pia ameuelekeza uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kusaidiana na taasisi na vyombo vyenye uzoefu wa maafa kushirikiana katika kuendelea kuokoa maisha ya watu, kusaidia waliozingirwa na mafuriko na kuwahifadhi na kuwasaidia wale wote waliopoteza nyumba na makazi kutokana na mafuriko hayo.

Katika salamu zake, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Sadiq: “Nimepokea kwa masikitiko habari za vifo vya wenzetu 13 vilivyotokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa ambayo sote tumeishuhudia katika Mkoa wa Dar es Salaam tokea jana. Nakutumia wewe rambirambi zangu kutokana na vifo hivyo, na kupitia kwako kwa familia, ndugu na jamaa waliopoteza wapendwa wao katika balaa hili la mafuriko. Wajulishe kuwa msiba wao ni msiba wangu, naelewa machungu yao na niko nao katika hali ya sasa ya maombolezo. Mungu aziweke pema peponi roho za marehemu wote.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Napenda pia kupitia kwako kutoa pole zangu nyingi kwa wote walioumia ama kupoteza mali zao katika mafuriko haya. Wajulishe kuwa moyo wangu uko nao wakati huu wa mazingira magumu.”

“Chini ya usimamizi wako, ningependa kuona uongozi wa Mkoa kwa kushirikiana na taasisi na vyombo vyenye ujuzi na uzoefu wa kupambana na majanga na dharura za namna hii, kuhakikisha kuwa tunaendelea kuokoa watu ambao bado wamezingirwa na mafuriko, tunawapa matibabu wale walioumia katika mafuriko hayo, na tunawahifadhi na kuwapa huduma za kibinadamu wote waliopoteza nyumba na makazi yao katika mafurikio hayo.”

WATU 13 WAPOTEZA MAISHA JIJINI DAR ES SALAAM KUTOKANA NA MVUA!!



Boti zikitumika kuwaokoa wananchi ambao walikumbwa na mafuriko katika Jiji la Dar Es Salaam. Boti hiyo ilitumika kuwaokoa wakazi wa Jangwani na hata Kigogo ambao walikuwa wamechukuliwa na mafuriko hayo. Mamia ya wananchi hawana makazi kutokana na mvua hizo zilizochangia kuzuka kwa mafuriko huku watu 13 wakipoteza maisha na uharibifu mwingine wa miundombinu ukishuhudiwa!!

MAFURIKO YAENDELEA KUTESA WAKAZI WA DAR ES SALAAM KWA SIKU YA PILI SASA!!





Hali ilivyo katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam baada ya mvua kali ikiambatana na radi kuendelea kutikisa Jiji hilo. Mvua hiyo imenyesha kwa saa zaidi ya nne sasa huku mawasiliano ya barabara yakikatizwa na kuchangia watu kushindwa kufika maeneo wanayokwenda!! Jeshi la Polisi nalo linaendelea na zoez la uokozi kwa wale ambao wamekwama kwenye maeneo ya mabondeni!!

Monday, December 19, 2011

RAIS KIKWETE AWAAPISHA MABALOZI WAPYA IKULU LEO!!


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaapisha Mabalozi wapya ambao amewateua kwenda kuiwakilisha nchi kwenye mataifa ya ughaibuni. Miongoni wa walioapishwa ni pamoja na Philip Marmo ambaye anakwenda nchini China, Daktari Batlida Salha Burian ambaye anakwenda nchini Kenya. Dokta Deodorus Kamala yeye anachukua nafasi ya kuwa Balozi nchini Ubelgiji. naye Dokta Ladislaus Komba anakwenda kuhudumu nchini Uganda. Mabalozi wengine ni pamoja na Bi Shamim Nyanguga ambaye amepelekwa nchini Msumbiji, Bi Grace J.E. Mujuma ambaye anakwenda nchini Zambia, Mohamed Hamza ambaye anakwenda kuiwakilisha nchi huko Misri na Ali Saleh ambaye amepelekwa Omani.

MBUNGE WA KIGOMA KUSINI DAVID KAFULILA AVULIWA UANACHAMA NCCR-MAGEUZI!!


Halmashauri Kuu ya Chama Cha NCCR-Mageuzi imemtimua uanachama Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila kwa madai ya kutaka kukiharibu chama hicho huku wanachama wengine sita wakiingia kwenye mkumbo huo.

Mgombea wa Urais kwenye uchaguzi uliopita Hashim Rungwe ni miongoni mwa waliotimuliwa kwa kosa linalofanana na Kafulila wakitajwa kutaka kukivuruga Chama.

Wanachama hao wanasiku kumi na nne za kukataa rufaa kupinga adhabu ambayo imetolewa na iwapo watashindwa kwenye rufaa yao ni wazi Kafulila atakuwa amepoteza uhalali wa kuwa Mbunge na hivyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulazimika kuitisha Uchaguzi Mdogo.

MAN CITY YAREJEA KILELENI WAKATI MAN UTD IKISHINDA DHIDI YA QPR!!




Klabu ya Manchester City imefanikiwa kurudi kileleni mwa Ligi Kuu Nchini Uingereza baada ya kuifunga Arsenal kwa goli moja kwa nunge!! Goli la David Silva ndiyo lilipeleka kilio kwa Washika Bunduki wa Jiji la London!! Manchester United ilifanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0 mbele ya Queens Park Rangers!!

BARCELONA YATWAA UBINGWA WA KLABU BINGWA DUNIANI!!


Klabu ya FC Barcelona imefanikiwa kutetea Ubingwa wake wa Klabu Bingwa ya Dunia baada ya kuifunga Santos kwa magoli 4-0!! Katika mchezo wa fainal uliopigwa nchini Japan katika Jiji la Yokohama ulishuhudia Lionel Messi akifanikiwa kufunga magoli mawili huku mengine yakifungwa na Xavi Hanandez na Cesc Fabregas!!

KIONGOZI WA KOREA KASKAZINI KIM JONG IL AFARIKI DUNIA!!


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Il amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 69 baada kuugua ugonjwa wa moyo. Kiongozi huyo ambaye aliingia madarakani mwaka 1994 baada ya kifo cha Baba yake Kim Jong Sung. Nafasi yake itachukuliwa na mwanae Kim Jong Un!! Mazishi yake yatafanyika tarehe 28 December 2011!!

Monday, May 23, 2011

CARLO ANCELOTTI ATUPIWA VIRAGO CHELSEA!!



Kocha wa Chelsea Carlo Ancelotti ametupiwa virago na Chelsea baada ya kile kinachotajwa kuwa ni kushindwa kwake kutimiza malengo ambayo yalikuwa yamewekwa na tajiri wake!! Ancelotii anaondoka na sasa kibarua kinabaki kwa Chelsea kusaka Kocha mwingine!!

Monday, May 9, 2011

HOTUBA YA RAIS KIKWETE KWENYE MAFUNZO ELEKEZI!!!

HOTUBA YA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO
WA TANZANIA AKIFUNGUA MAFUNZO ELEKEZI KWA
VIONGOZI NA WATENDAJI WAKUU WA SERIKALI
TAREHE 9 MEI, 2011

Mheshimiwa Waziri Mkuu;
Mheshimiwa Jaji Mkuu;
Wazee Wetu, Mzee Cleopa Msuya na Mzee Pius Msekwa;
Ndugu Mawaziri;
Ndugu Naibu Mawaziri;
Ndugu Makatibu Wakuu;
Ndugu Naibu Makatibu Wakuu;
Wakuu wa Vyombo vya Dola;
Wageni Waalikwa;
Mabibi na Mabwana:
Ukaribisho
Nianze kwa kuwakaribisha nyote kwenye Semina Elekezi inayojumuisha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu. Kama lilivyo jina lake, Semina hii ni ya kuelekezana juu ya namna tutakavyotimiza majukumu yetu katika Serikali. Tulikuwa na Semina kama hii mwaka 2006. Imetusaidia kupata mafanikio tuliyoyapata miaka mitano iliyopita. Naamini na Semina hii itatusaidia kupata ufanisi tunaoutarajia na ambao wananchi wanautarajia kutoka kwetu.
Ndugu Viongozi na Watendaji wa Serikali;
Niruhusuni niombe radhi kwa niaba ya Viongozi Wakuu wawili kutokuwa nasi siku ya leo. Wa kwanza ni Makamu wa Rais, Dkt. Mohamed Gharib Bilal na wa pili ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein. Makamu wa Rais yuko Uturuki kuniwakilisha katika LDC Summit. Mwanzoni nilikubali kushiriki kwenye LDC Summit, lakini baada ya tarehe za Semina yetu kubadilika na kuangukia kwenye tarehe za Mkutano huo nikawa sina namna ila kutuma mwakilishi.
Kwa uzito wa mkutano wenyewe na matumaini ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na wenyeji wetu kuhusu ushiriki wa Tanzania nikaona Makamu wa Rais atuwakilishe. Makamu wa Rais amefuatana na Mheshimiwa Prof. Anna Tibaijuka, Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mheshimiwa Mahadhi Juma Maalim. Najua watakosa uhondo, lakini tutawapatia DVD ya Semina wataona na kusikia tuliyozungumza. Mheshimiwa Rais wa Zanzibar amebanwa na vikao vya maandalizi ya bajeti.
Madhumuni ya Semina
Ndugu Viongozi,
Katika Semina hii majukumu ya msingi ya Serikali ya utawala, maendeleo na ulinzi na usalama yatafafanuliwa. Pia itaelezwa jinsi kila mmoja wetu anavyohusika nayo na anavyotegemewa kutimiza wajibu wake. Katika hotuba yangu ya kuzindua Bunge nilitaja malengo 13 ambayo yamejumuisha mambo makuu tutakayoyapa kipaumbele katika Serikali katika miaka mitano hii. Lakini nilikumbusha kuwa yale mambo 13 ni muhtasari wa maelekezo yaliyomo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.
Ndugu Mawaziri;
Mtakumbuka kuwa katika mkutano wangu wa kwanza nanyi niliwasisitizia umuhimu wa Ilani ya Uchaguzi kwa kila mmoja wenu na kwa Serikali yetu kwa jumla. Niliwaambia kuwa Ilani ndiyo mkataba mkuu baina ya Chama cha Mapinduzi na wananchi. Utekelezaji wake ndicho kipimo kikuu cha uwezo wetu wa kuongoza, mwaka 2015. Niliwataka kila mmoja wenu atambue ukweli huo na kutengeneza mkakati wa kutekekeleza Ilani kwa yale mambo yanayohusu Wizara yake. Sina shaka kuwa takriban miezi mitano baadae kila mmoja wetu atakuwa amekamilisha kazi hiyo na kuingiza katika mipango ya kazi ya Wizara itakayotekelezwa kuanzia bajeti itakayowasilishwa Bungeni mwezi ujao.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Siku ile pia nilisisitiza jambo kwa Mawaziri ambalo napenda kulirudia tena leo kwani linawahusu na Makatibu Wakuu. Ninyi kwa pamoja, Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu ndiyo timu moja ya uongozi na utawala katika Wizara. Kama viongozi mnategemewa kuonyesha njia kuhusu nini cha kufanya kutekeleza majukumu ya Wizara nilizowakabidhi kuziongoza.
Katika jukumu lenu la utawala mnategemewa kuwa makini na mahiri katika kutumia rasilimali watu, vifaa na fedha za umma mlizokabidhiwa katika kutekeleza majukumu yenu. Mnategemewa kuwa na mipango na mikakati thabiti ya kutekeleza majukumu hayo.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Katika Wizara kila kitu huanzia na kuishia kwenu. Hakuna mwingine tena kuliko nyie isipokuwa mamlaka zilizo juu yenu; yaani Waziri Mkuu, Makamu wa Rais na Rais. Kwa sababu hiyo, ili muweze kutimiza kwa ukamilifu wajibu wenu huo hamna budi kwanza kabisa kutambua vyema majukumu yenu na jinsi ya kuyatekeleza. Semina hii ina shabaha ya kusaidia katika hilo. Lakini, njia kubwa zaidi ni ile niliyowaambia siku ile, yaani ninyi wenyewe kufanya bidii ya kujua kwa kusoma, kuona na kufanya shughuli za Wizara zenu kwa makini.
Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu mnatakiwa kuyajua kwa kina mambo yote yanayohusu Wizara mnazoziongoza. Vinginevyo hamtaongoza vizuri. Mtakuwa wababaishaji. Mtashindwa kutoa malengo maana mtakuwa hamjui nini cha kuekeleza, mtashindwa kusimamia mambo, kwa vile hamjui cha kusimamia, mtakuwa hamuonekani mkifanya chochote cha maana kwa sababu hamna jambo la kufanya zaidi ya mambo ya kawaida – routine issues. Mawaziri na Makatibu Wakuu lazima mtoke. Hiyo ndiyo njia bora zaidi ya kujua mambo yahusuyo Wizara yenu na ndiyo njia bora ya kuongoza: kuona wenyewe na kutenda. Itawafanya mjiamini kuelekeza na pia mnaposimama mbele za watu na kusema. Msiwe mangimeza. Tokeni, tembeeni kuona shughuli zenu. Tembeleeni wananchi muwafahamu, wawafahamu, mjue shida zao muwatatulie.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Ili mjue mambo ya Wizara zenu vizuri lazima mtengeneze utaratibu mzuri wa kupashana habari kuhusu mambo yanayotokea Wizarani. Utaratibu utakaomwezesha kila mmoja kujua kinachoendelea Wizarani. Msipofanya hivyo kuna hatari ya ninyi wenyewe viongozi wakuu mkawa hamjiamini na hata kuwa na kauli tofauti kwa jambo hilo hilo. Mmoja anasema hivi na mwingine anasema vile. Kuna hatari ya kuzuka kutokuelewana miongoni mwenu.
Hii pia ni muhimu sana hasa kwa sababu barua huandikwa kwa Waziri au Katibu Mkuu. Msipotengeneza utaratibu wa kupashana habari Waziri anaweza asijue anachojua Katibu Mkuu na kinyume chake. Na, baya zaidi Naibu Waziri na Naibu Katibu Mkuu wanaweza kuwa gizani kabisa. Naibu Waziri hushikilia Wizara anaposafiri Waziri na ndiye msemaji wa Wizara katika Bunge asipoyajua vyema yanayotokea au mambo yanayohusu Wizara hatakuwa msemaji mzuri na wa kujiamini wa Wizara. Naibu Katibu Mkuu hushikilia ofisi ya Katibu Mkuu anapokuwa hayupo. Hatafanya kazi kwa kujiamini na atashindwa kuamua mambo kwa sababu hana habari ya mambo yanayohusu Wizara. Mambo yatakawia na mengine kukwama kwa sababu hiyo.
Pamoja na kutoa fursa kwa kila mmoja wenu kuona na kujua kinachotokea Wizarani, jengeni utaratibu wa kukutana mara kwa mara kuzungumzia shughuli za Wizara zenu. Itasaidia sana. Ndiyo maana Jeshini kuna Officers Mess kutoa fursa ya maofisa kufahamiana na kuzungumza masuala yahusuyo shughuli zao. Mnaweza kuwa na vikao vya mara kwa mara au hata kunywa chai pamoja. Hata nyie mnaweza kuwa na utaratibu kama huo.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Narudia kuwakumbusha kwamba msingi wa utendaji Serikalini ni katiba, sheria, kanuni na taratibu. Ni muhimu kwenu kama viongozi mkajielimisha juu ya Katiba, sheria, kanuni na taratibu mbalimbali zinazoongoza utendaji kazi katika sehemu zenu za kazi. Uhalali wa maamuzi mtakayoyafanya hupimwa na sheria. Ukifanya maamuzi yanayokinzana na sheria utahojiwa wewe binafsi lakini pia utaibebesha Serikali mzigo wa hasara na fedheha itakayotokana na maamuzi hayo.
Lakini pia maamuzi yasiyofuata sheria yanaweza kuwa na madhara kwa wananchi. Heshimuni Katiba na fuateni sheria, kanuni na taratibu zilizopo katika utekelezaji wa majukumu yenu. Katika semina hii masuala hayo yatafafanuliwa na kuzungumzwa. Kadhalika uhusiano wa Serikali na mihimili mingine ya dola yani Bunge na Mahakama utafafanuliwa.
Uwajibikaji wa Pamoja
Viongozi Wenzangu;
Wakati wote sisi sote tunapaswa kuzingatia kwamba Wizara ni moja, Serikali ni moja, lengo letu ni moja na hivyo wakati wote lazima tuwe na umoja, mshikamano na kauli moja. Serikali au Wizara isiyokuwa na umoja haiwezi kutimiza wajibu wake ipasavyo. Mawaziri na Makatibu Wakuu wasiokuwa na umoja hawatatimiza wajibu wao ipasavyo. Umoja ni kitu cha msingi sana. Unapokosekana kunakuwepo mifarakano na hatimaye huingia udhaifu katika kuamua na kutenda. Hali hiyo itasababisha wananchi kutohudumiwa ipasavyo na maendeleo yao kuathirika.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Hakikisheni kuwa katika Wizara zenu kuna umoja. Umoja huo uanzie kwenu nyinyi viongozi wakuu. Aghalabu ninyi mkiwa na umoja Wizara huwa na umoja, ninyi mkifarakana wafanyakazi nao hugawanyika. Kwa upande wa Serikali nako hali kadhalika, lazima Mawaziri wawe na umoja. Iwapo Mawaziri wana umoja, Serikali huwa na mshikamano na nguvu katika kuamua na kutenda. Wakati wote tuhakikishe kuwa tuna umoja na mshikamano miongini mwetu. Tuepuke kauli na matendo yatakayofarakanisha Mawaziri na hivyo kuleta mgawanyiko katika Serikali.
Lazima tukumbuke na kuzingatia dhana ya uwajibikaji wa pamoja. Lazima idhihirike katika ngazi ya Wizara na Serikali kwa jumla. Mawaziri, ninyi ndiyo viongozi wakuu katika Wizara zenu na Makatibu Wakuu ndiyo watendaji wakuu wa Wizara. Nyote mnawajibika katika nafasi zenu kwa maamuzi mnayoyafanya ya kisera na kiutendaji. Hamna budi kushirikiana, kushauriana na kuwekeana staha. Viongozi na watendaji wakuu wa Wizara hamna budi kujenga mahusiano mazuri na uwajibikaji wa pamoja. Haifurahishi kuona Waziri na Katibu Mkuu, au Waziri na Naibu Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu au Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu hawaelewani. Wanasemana na hata wakipingana hadharani, yaani mbele za wafanyakazi. Na baya zaidi pale wanapingana katika vyombo vya habari kuhusu maamuzi au utendaji wa Wizara au Serikali kwa ujumla. Hayo si maadili mema katika taasisi yoyote.
Uzoefu unaonesha kuwa jambo hili hutokea pale ambapo kunakuwa na kuingiliana katika majukumu au kwa kutozingatiwa kwa taratibu na maadili ya uongozi. Lazima ieleweke kuwa tukishaamua jambo kwa pamoja Wizarani au katika Baraza la Mawaziri ni uamuzi wetu sote hata kama wewe ulikuwa na mawazo tofauti. Wote tunao wajibu wa kuunga mkono na kuutetea. Kamwe hatutegemewi kuendelea kuupinga baada ya hapo. Kufanya hivyo ni kukiuka maadili ya uongozi na uwajibikaji wa pamoja. Kama unaona vigumu sana kuuafiki ni bora kutoka. Hairuhusiwi kupinga taasisi ambayo wewe umo ndani kama mmoja wa viongozi wake. Ni vyema hili likaeleweka vyema. Msitupe tabu ya kuulizana maswali na kuwasemea.
Kuwajibika Bungeni
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Dhana hii ya uwajibikaji wa pamoja nayo inahusu pia shughuli za Serikali Bungeni. Miswada ya Serikali ni ya Mawaziri wote mmoja mmoja na kwa umoja wao. Mswada wa Sheria ukiletwa na Waziri mmoja, kila Waziri anao wajibu wa kuunga mkono na kuutetea. Haitegemewi na ni kinyume cha maadili cha hali juu kwa Waziri kupinga mswada wa Waziri mwenzake. Kwa kweli, tabia hii haivumiliki na anayetenda hayo amejitenga mwenyewe na Serikali.
Jambo lingine muhimu kwa Mawaziri ni kutambua kuwa kuhudhuria vikao vya Bunge ni jambo la lazima kama ilivyo kwa vikao vya Baraza la Mawaziri. Si jambo la hiari. Ni lazima Waziri ahudhuria vikao vya Bunge bila ya kukosa labda awe na sababu kubwa inayoelezeka na kukubalika. Kutembelea jimbo lako la uchaguzi ni jambo la lazima lakini siyo sababu ya kukufanya ukose vikao vya Bunge au Baraza la Mawaziri.
Uwajibikaji Kikazi na Kimaadili
Ndugu Viongozi;
Tulipokutana mara ya kwanza kule Dar es Salaam baada ya kuunda Serikali, nilizungumzia uadilifu. Napenda, leo tena kusisitiza jambo hili kwa sababu ya umuhimu wake. Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu ni viongozi wakubwa sana Wizarani, Serikalini na katika jamii. Kiongozi anatakiwa kuwa mfano mwema (role model) kwa watu anaowaongoza. Watu watamani kuwa kama yeye au kuishi kama yeye. Watu watamani kumuiga kwa uchapakazi wake, kwa tabia njema na matendo mema. Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Naibu Mkuu wasinyooshewe kidole kwa uvivu, uzembe, wizi, ubadhirifu wa mali ya umma, vitendo vya utovu wa uadilifu kama vile wizi, ulevi wa kupindukia, uzinzi, majigambo, ubabe na uonevu na dhuluma. Kuwa hivyo ni kupungukiwa sifa za msingi za uongozi. Huwakatisha tamaa wananchi na kuwafanya wapoteze imani na Serikali yao.
Uwajibikaji kwa Wananchi
Ndugu Viongozi;
Lazima tukumbuke kwamba Serikali yetu imewekwa madarakani na wananchi kwa ajili yao na siyo kwa ajili ya viongozi tuliopo madarakani. Serikali ipo kwa ajili ya kuwahudumia na kutatua matatizo yanayowakabili wananchi na kuwaletea maendeleo. Wananchi wanapenda kuona Serikali yao ina viongozi na watumishi waadilifu, wachapakazi hodari, wanaowasikiliza, wanaojali shida zao na wepesi wa kushughulikia na kutekeleza maamuzi mbalimbali ya Serikali. Ni wajibu wetu kama viongozi wakuu na watendaji wakuu kutimiza matarajio hayo ya wananchi.
Kuisemea Serikali
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Moja ya mada ya semina hii inahusu mawasiliano ya Serikali. Kwa maneno mengine kuisemea Serikali. Hili ni jambo ambalo tuna udhaifu mkubwa. Sijui kwanini hatuwi wepesi kuyasemea mafanikio mengi tuliyoyapata tukaacha wasiotutakia heri wanaosema hatukufanya kitu wasikike mpaka waonekane wanasema kweli. Mwanazuoni mmoja bingwa wa habari aliwahi kusema kuwa “kufanya kitu bila kuufahamisha umma ni sawa kama kitu hicho hakijafanyika.” Mwingine anasema kuwa uongo ukisemwa mara nyingi hugeuka kuwa ukweli.
Uzoefu wa miaka mitano umeonyesha kwamba tumefanya mambo mengi lakini wananchi hawakuelezwa ipasavyo. Pia, tumeacha upotoshaji kufanywa bila ya kusahihishwa au kuchelewa sana kusahihishwa. Hivyo basi, wananchi wamekuwa wakijikuta wakiamini uongo na kulaumu au hata kuichukia Serikali kwa mambo ambayo ni potofu. Wangeambiwa ukweli mapema hawangefikia hapo. Lazima upungufu huo tuondokane nao. Lazima tuwe makini na hodari kuelezea shughuli zinazofanywa na Serikali, mafanikio yanayopatikana na changamoto zilizopo.
Aidha, tuwe wapesi kusahihisha upotoshaji wowote unaofanywa dhidi ya Serikali. Kutokufanya hivyo kumetugharimu sana. Hatuwezi kuendelea hivi wakati ninyi viongozi mpo, watu Mawizarani wapo, rasilimali zipo na vyombo vya habari vipo vinasubiri kupewa habari.
Ukuzaji Uchumi na Maendeleo
Ndugu Viongozi;
Nilieleza awali kuwa mojawapo ya majukumu ya msingi ya Serikali ni kuleta maendeleo ya nchi na watu wake. Hususan Serikali inalo jukumu la kukuza uchumi na kuwapatia wananchi huduma za msingi za kiuchumi na kijamii kwa lengo la kuongeza mapato na kuboresha hali ya maisha ya Watanzania. Hii ni kazi ya msingi sana kwa Serikali kufanya na lazima kufanikiwa. Kazi hiyo ndiyo moja ya sababu na shabaha pana ya Serikali kuwepo na sisi wote kuwapo. Kwangu mimi na ninyi wenzangu kuleta maendeleo na kukidhi matumaini ya Watanzania ni changamoto na mtihani wetu mkubwa sana.
Katika Semina hii masuala ya kukuza uchumi na kuleta maendeleo yamepewa nafasi ya kuzungumzwa kwa upana. Pamoja na watoa mada wa ndani, tunawashukuru marafiki zetu wa Benki ya Dunia kwa kutuletea mabingwa wa uchumi na maendeleo kuja kuzungumza nasi. Naamini uzoefu na mifano ya nchi mbalimbali kuhusu kufanya mageuzi ya kiuchumi na kujiletea maendeleo kutatusaidia kuimarisha na kuboresha hatua tunazochukua nchini.
Ndugu Viongozi;
Hakika tumefanya mengi na mafanikio yanaonekana, lakini tunayo kazi kubwa sana mbele yetu ya kufanya. Tanzania ni miongoni mwa nchi 49 maskini sana duniani. Shabaha yetu kubwa ni kutoka hapa tulipo sasa na kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. Yaani, tutoke kwenye pato la wastani la USD600 la sasa hadi pato la USD1,500 mpaka USD3,000 mwaka huo.
Niliamua na kuelekeza kuwa yafanyike mapitio ya Vision 2025 na tuigawe miaka 15 iliyosalia katika mafungu matatu ya miaka mitano mitano. Tuwe na mipango ya maendeleo ya miaka mitatu tukianzia na huu unaowiana na kipindi chetu cha uongozi. Hii itatuongoza vizuri zaidi kuelekea na kufikia lengo. Kazi ya mapitio inaendelea kama ilivyo ile ya matayarisho ya mpango wa kwanza wa maendeleo. Katika Semina hii tutapata maelezo ya awali ya kazi inayoendelea.
Ndugu Viongozi na Ndugu Washiriki;
Tunao pia Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) ambao tumekuwa tunautekeleza tangu mwaka 2005. Tumekamilisha MKUKUTA I na hivi sasa tupo kwenye utekelezaji wa MKUKUTA II ambao utakamilika mwaka 2015. MKUKUTA umetusaidia sana katika kuainisha maeneo ya kipaumbele katika bajeti. Kwa ajili hiyo, imesaidia katika jitihada za Serikali za kupunguza umaskini na kuinua hali ya maisha ya Watanzania. Bila ya shaka tutapata nafasi ya kuelezwa maudhui ya MKUKUTA II ili tuelewe namna ya kuwianisha shabaha zake na shughuli tunazozifanya katika Wizara zetu.
Ndugu Mawazirina Ndugu Makatibu Wakuu;
Kuinua hali ya maisha ya Watanzania kuna sura mbili: upande mmoja kuna kuongeza kipato chao. Yaani wasiokuwa na shughuli wapate shughuli za kufanya (kukuza ajira) na wale wenye shughuli zikue na kuimarika ili mapato yao yaongezeke. Mazungumzo yahusuyo kukuza uchumi yatatoa fursa ya kuyajadili mambo haya. Upande wa pili unahusu upatikanaji wa huduma za kiuchumi na huduma za kijamii zilizo bora na zinazotosheleza mahitaji. Wananchi wanataka kuona miundombinu hasa ya barabara zinajengwa na kuimarishwa, umeme wa uhakika pamoja na huduma za maji, afya na elimu zinapatikana kwa kiwango kinachokidhi mahitaji na ubora unaostahili.
Tumejitahidi kwa kiasi kikubwa kuongeza upatikanaji wa huduma hizo katika miaka mitano hii. Lakini, kazi iliyo mbele yetu bado ni kubwa. Upande mmoja bado tunayo kazi ya kuwafikia wale ambao huduma hizo hazijawafikia. Na, upande mwingine tunayo kazi ya kuhakikisha ubora na uendelevu wa huduma pale inapopatikana. Kuyafanya hayo ni wajibu wa msingi wa Serikali, kinachotakiwa ni kujipanga vyema kwa mipango na rasilimali watu, vifaa na fedha ili kutimiza wajibu huo.
Mapato na Matumizi ya Serikali
Ndugu Viongozi;
Uwezo wa Serikali kutekeleza majukumu yake unategemea sana kuwepo kwa rasilimali fedha na jinsi fedha hizo zinavyotumika. Upatikanaji wa rasilimali fedha unategemea ufanisi katika ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Serikali inapata mapato yake kupitia kodi na tozo mbalimbali. Kodi ndicho chanzo kikubwa cha mapato ya Serikali na chombo kikubwa cha ukusanyaji wa mapato hayo ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Katika miaka mitano hii mafanikio makubwa yamepatikana na mapato yameongezeka karibu mara tatu kutoka shilingi 177 bilioni kwa mwezi hadi shilingi 430 bilioni kwa mwezi hivi sasa.
Pamoja na nyongeza hiyo bado tunao uwezo wa kuongeza zaidi. Kuna watu wengi ambao bado hawajafikiwa na wigo wa kodi. Laiti wangefikiwa mapato ya Serikali yangekuwa makubwa zaidi ya ilivyo sasa. Tutafanyaje tufanikishe hilo ni changamoto yetu sote Serikalini. Tufanye nini ili tuzibe mianya inayovujisha mapato ya Serikali ni swali ambalo sote katika Serikali hatuna budi kutoa jibu muafaka. Kwa upande wa tozo mbalimbali karibu kila Wizara inazo tozo za namna hiyo. Wengi wenu hamjafikia hata theluthi moja ya malengo. Tutafanyaje ili tufikie malengo na kuyavuka ni swali ambalo kila mmoja wetu anatakiwa kujiuliza na kutoa majibu sahihi.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Sote tunajua kuwa licha ya tozo na kodi, chanzo kingine cha mapato ya Serikali ni mikopo na misaada kutoka Mabenki, Mataifa Rafiki, na Mashirika ya Fedha ya Kimataifa. Tumepata misaada na mikopo mingi ya kutoka nje katika kipindi kilichopita na muelekeo ni kuwa tutaendelea kupata zaidi katika miaka mitano ijayo. Tunatambua haja na hoja ya kupunguza utegemezi wa misaada na mikopo kutoka nje kwa kuongeza mapato yetu ya ndani. Katika miaka mitano hii tumeendelea kupunguza utegemezi lakini nia yetu sote iwe kupunguza zaidi. Naamini tutafika kwenye shabaha hiyo iwapo tutaongeza mapato ya ndani. Naomba tuzungumzie namna ya kufikia shabaha hiyo.
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Usimamizi wa matumizi ya fedha tunazokusanya kama mapato ni jukumu jingine kubwa kwetu sote. Tuna wajibu wa kuhakikisha kuwa fedha za walipa kodi zinatumika ipasavyo kuwaletea maendeleo wananchi. Katika kudhibiti matumizi ni muhimu kuelewa na kusimamia sheria, taratibu na kanuni za fedha na manunuzi ya umma kwa ufanisi wa hali ya juu. Taarifa za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali zinaonyesha kuongezeka kwa ubora lakini bado tunayo kazi ya kufanya kufikia kiwango cha kusema sasa tunapumua. Bado kuna makosa mengi katika kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za mapato na matumizi ya fedha za umma. Nataka tuzungumze kwa dhati tutafikaje kwenye ufanisi wa hali ya juu kwenye eneo hilo. Hali hii hatuwezi kuiacha iendelee kuboreka kwa kasi ndogo iliyopo sasa.
Viongozi na watendaji wakuu wa Serikali, mnatakiwa kuwa mfano kwa wafanyakazi mnaowaongoza kwa kuzingatia nidhamu ya matumizi ya fedha za umma. Hakikisheni bajeti hazikiukwi, fedha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na sheria na kanuni za fedha zinaheshimiwa. Niliagiza Kamati za Fedha ziundwe katika kila Wizara na Idara za Serikali zinayojitegemea. Je zimeundwa? Je zinafanya kazi? Hakikisheni zipo hai na zinatimiza wajibu wake. Zitasaidia sana kwa upande wa kuongeza mapato na kudhibiti matumizi katika Wizara.
Ulinzi na Usalama
Ndugu Mawaziri na Ndugu Makatibu Wakuu;
Katika semina hii tutapata nafasi ya kuzungumzia masuala ya ulinzi na usalama. Tutawasikiliza Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama kuhusu usalama wa nchi. Pia tutamsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU kuhusu mapambano dhidi ya rushwa na Kamishna wa Tume ya Maadili ya Viongozi kuhusu uadilifu wa viongozi.
Maandalizi ya Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru
Ndugu Viongozi;
Kama mnavyofahamu mwaka huu tunaadhimisha miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania Bara. Tumeazimia kusherehekea siku hii kwa uzito unaostahili. Niliagiza tufanye mambo kadhaa muhimu ambayo ni pamoja na kufanya tathmini ya kina ya mafanikio tuliyoyapata, katika juhudi zetu za kujiletea maendeleo. Aidha, niliagiza Wizara, idara na taasisi za Serikali na hata sekta binafsi zifanye tathmini ya shughuli zao na kuandika vitabu ili kuhifadhi kumbukumbu hizo muhimu kwetu na kwa vizazi vijavyo.
Vile vile niliagiza yafanyike maonesho maalum katika Uwanja wa Maonyesho wa Julius Nyerere hapa Dar es Salaam na kote mikoani kwenye viwanja vya maonesho, kuelezea mafanikio yaliyopatikana katika nyanja mbalimbali katika miaka 50 tangu Uhuru wa Tanzania Bara. Kwa kuwa tunakaribia nusu ya mwaka huu, ni vema sasa kukumbushana kuendelea na maandalizi ya sherehe hizo. Ni matumaini yangu kwamba kila Wizara inakaribia kukamilisha tathmini hiyo. Walio nyuma sana waongeze kasi. Tuliazimia pia kuwa tuanzishe mchakato wa kuipitia Katiba yetu. Tumeanza, lakini kuna upotoshaji mkubwa, lakini wajibu wetu sote tuliopo hapa kukabili hila na njama hizo chafu. Naamini tutafika salama. Kinachotakiwa ni mshikamano na umoja miongini mwetu.
Hitimisho
Ndugu Viongozi Wenzangu,
Ni matumaini yangu kwamba maneno haya ya utangulizi niliyosema, yatatupatia msingi wa tafakuri katika mijadala na mafunzo tutakayopatiwa katika siku nne zijazo hasa katika maeneo makuu ya semina ambayo ni pamoja na mfumo wa utawala na utendaji; uchumi na maendeleo; utawala bora; ulinzi na usalama; muungano; na masuala mtambuka.
Nimeambiwa kwamba semina hii itaendeshwa kwa utaratibu wa mihadhara kwa ajili ya kuwasilisha mada pamoja na majadiliano ya pamoja. Pia nimearifiwa kuwa kutakuwepo majadiliano katika vikundi ili kuchambua kwa undani zaidi mada zilizowasilishwa. Hivyo, rai yangu kwenu nyote muwe tayari kushiriki kwa ukamilifu katika majadiliano kwenye mihadhara kwa ukweli na uwazi bila kujali tofauti ya nyadhifa zenu. Wote muwe huru kutoa maoni yenu. Ndiyo maana tuko hapa.
Ndugu Viongozi,
Nawashukuru watoa mada waliokubali kuchangia ujuzi na uzoefu wao nasi. Baada ya kusema hayo sasa napenda kutamka kwamba Semina Elekezi kwa Viongozi na Watendaji Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefunguliwa rasmi.

MANCHESTER UNITED YAKARIBIA UBINGWA NCHINI UINGEREZA!!






Ushindi wa magoli 2-1 iliyoupata Manchester United mbele ya Chelsea umeifanya klabu hiyo kukaribia kutwaa taji lake la kumi na tisa la Ligi Kuu nchini Uingereza. Kwenye mchezo huo mkali uliopigwa Old Trafford umeshuhudia Manchester ikipata magoli yake kupitia Javier Hernandez na Nemanja Vidic huku Frank Lampard akifunga goli la Chelsea!! Kwa sasa Manchester United iliyobakiwa na michezo miwili inahitaji pointi moja kutwaa Ubingwa!!

Thursday, May 5, 2011

MANCHESTER UNITED YAKAMILISHA SAFARI YA WEMBLEY!!!




Klabu ya Manchester United imefanikiwa kutinga katika Fainal ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya baada ya kuifunga Schalke 04 kwa magoli 4-1!! Kwa matokeo hayo Manchester United imefanikiwa kuiondosha Schalke 04 kwa magoli 6-1!! Kocha Mkuu wa Man Utd Sir Alex Ferguson amekitaka kikosi chake kutowahofia wapinzani wao Barcelona ambao watakumbana nao huko Wembley tarehe 28 May!!

Wednesday, May 4, 2011

RAIS KIKWETE KWENYE MKUTANO WA KIUCHUMI HUKO SAUZI!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atakuwa mgeni maalum katika mjadala wa kimataifa kuhusu Visheni Mpya ya Kilimo katika Afrika (Achieving Africa’s New Vision for Agriculture) utakaofanyika mjini Cape Town, Afrika Kusini, Jumatano, Mei 4, 2011.

Rais Kikwete pia atatembelea Kituo cha Kimataifa cha Biashara (World Trade Centre) mjini humo humo kuona maandalizi yanayofanywa kwa ajili ya kuanzisha kituo kama hicho nchini Tanzania.

Aidha, kesho hiyo hiyo, Rais Kikwete atashiriki katika mjadala maalum wa maandalizi ya kuanzishwa kwa Soko la Mazao nchini (Commodity Exchange) ambalo maandalizi yake yanafanywa kwa pamoja kati ya Serikali ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB).

Rais Kikwete atashiriki katika shughuli hizo muhimu kwa uchumi na maendeleo ya Tanzania ikiwa sehemu ya ushiriki wake katika Mkutano wa Uchumi Duniani – Kanda ya Afrika (World Economic Forum-Africa) unaofanyika mjini Cape Town, Afrika Kusini.

Mwaka jana, mkutano huo ulifanyika mjini Dar es Salaam, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mkutano huo kufanyika nje ya mji wa Cape Town katika historia yake.

Rais Kikwete ameondoka nchini Jumanne, Mei 3, 2011, kwenda Cape Town kwa ajili ya mkutano huo wa siku mbili ambako pia atashiriki katika shughuli nyingine tatu kuhusu uchumi na maendeleo.

Washiriki wengine wa mkutano wa Visheni Mpya ya Kilimo katika Afrika, ambako Rais Kikwete atakuwa mgeni maalum, ni pamoja na viongozi mbalimbali duniani wa serikali, biashara na uchumi, mashirika ya kimataifa, mashirika yasiyokuwa ya kimataifa, wasomi na vyama vya wakulima duniani.

BARCELONA WATANGULIA WEMBLEY!!







Klabu ya Barcelona imefanikiwa kutinga hatua ya Fainal ya Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya baada ya kuoondoa kwenye mashindano Real Madrid kwa kwenda sare ya 1-1. Mchezo huo umetawaliwa na lwama lukuki kutoka kwa wachezaji wa Real Madrid ambao wanashutumu maamuzi!!

Monday, May 2, 2011

MAREKANI YATANGAZA KIFO CHA OSAMA BIN LADEN!!!




Rais wa Marekani, Barack Hussein Obama ametangaza kifo cha Kiongozi wa mtandao wa Al Qaeda Osama Bin Laden ambacho kimetokea nchini Pakistan!! Rais wa Marekani ametangaza kuwa Haki imepatikana kutokana na kifo hicho!! Taarifa kutoka Vyombo vya Habari vya Marekani zinaeleza kuwa tayari Mwili wa Osama Bin Ladeba ameshazikwa Baharini!!