Monday, December 19, 2011

RAIS KIKWETE AWAAPISHA MABALOZI WAPYA IKULU LEO!!


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaapisha Mabalozi wapya ambao amewateua kwenda kuiwakilisha nchi kwenye mataifa ya ughaibuni. Miongoni wa walioapishwa ni pamoja na Philip Marmo ambaye anakwenda nchini China, Daktari Batlida Salha Burian ambaye anakwenda nchini Kenya. Dokta Deodorus Kamala yeye anachukua nafasi ya kuwa Balozi nchini Ubelgiji. naye Dokta Ladislaus Komba anakwenda kuhudumu nchini Uganda. Mabalozi wengine ni pamoja na Bi Shamim Nyanguga ambaye amepelekwa nchini Msumbiji, Bi Grace J.E. Mujuma ambaye anakwenda nchini Zambia, Mohamed Hamza ambaye anakwenda kuiwakilisha nchi huko Misri na Ali Saleh ambaye amepelekwa Omani.

No comments:

Post a Comment