Monday, December 19, 2011

MBUNGE WA KIGOMA KUSINI DAVID KAFULILA AVULIWA UANACHAMA NCCR-MAGEUZI!!


Halmashauri Kuu ya Chama Cha NCCR-Mageuzi imemtimua uanachama Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila kwa madai ya kutaka kukiharibu chama hicho huku wanachama wengine sita wakiingia kwenye mkumbo huo.

Mgombea wa Urais kwenye uchaguzi uliopita Hashim Rungwe ni miongoni mwa waliotimuliwa kwa kosa linalofanana na Kafulila wakitajwa kutaka kukivuruga Chama.

Wanachama hao wanasiku kumi na nne za kukataa rufaa kupinga adhabu ambayo imetolewa na iwapo watashindwa kwenye rufaa yao ni wazi Kafulila atakuwa amepoteza uhalali wa kuwa Mbunge na hivyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulazimika kuitisha Uchaguzi Mdogo.

No comments:

Post a Comment