Thursday, December 29, 2011

MTANGAZAJI WA TBC HALIMA MCHUKA AFARIKI DUNIA!!


Mtangazaji Mahiri wa Mpira katika Eneo la Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Mwanamke wa Kwanza Halima Mchuka amefariki Dunia akiwa anahudumu katika Redio Tanzania Dar es Salaam RTD na baadae Shirika la Utangazaji Tanzania (SHIUTA) amefariki Dunia.

Mchuka amefariki usiku wa kumkia leo kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda ambapo kwa sasa inaelezwa alikuwa anaanza kupata nafuu baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mtangazaji Halima Mchuka alijiunga na Radio Tanzania Dar es Salaam mwaka 1994 ambapo alifanya kazi katika Idara ya Habari na Idara ya mipango.

Mungu ailaze Roho ya BI Halima Mchuka pahala pema peponi Amina

No comments:

Post a Comment