Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo, Jumatatu, Januari 18, 2010, amewapatia wakazi wa eneo la Kamsamba, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Mbeya, gari la wagonjwa, ili kupunguza shida ya usafiri wa wagonjwa katika eneo hilo.
Katika shughuli fupi iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Mheshimiwa Kikwete amekabidhi gari hilo kwa Mkurugenzi wa Maendeleo wa Halmashauri ya Mbozi, Bwana Levison Jeremiah Chilewa.
Mheshimiwa Kikwete aliwaahidi wananchi wa Kamsamba gari hilo wakati alipotembelea eneo hilo mwishoni mwa mwaka jana.
Saturday, January 16, 2010
Friday, January 15, 2010
CAMPBELL ASAJILIWA TENA ARSENAL!!!

Klabu ya Arsenal haitimaye imemsajili tena beki wake wa zamani Mkongwe Sol Campbell mwenye umri wa miaka 35. Campbell ambaye almanusra ajiunge na Manchester United amekamilisha usajili wake na Kujiunga na Washika Bunduki wa Jiji la London. Campbell amekuwa hana klabu ya kuchezea tangu mwezi December baada ya kuachwa na Notts County
WAKALI WA MLIMANI TV WAKIWA KAZINI!!!!!


Hawa ni baadhi tu ya wale ambao wanakisimamisha kituo cha Mlimani Tv kwenye kazi. Anuary Mkama Mkuu wa kazi akifanya interview na Nahodha wa Malindi ya Zanzibar. Saleh Masoud maarufu kama Jecha akiwa amekamata Kamera yake. Juu ni Sylvia Mwehozi akiwa na Mama Nyerere. Ninavyomjua huyu binti hii picha itakuwa imebandikwa sebuleni kwao.
LIGI MZUNGUKO WA PILI KUANZA KESHO!!
Mabingwa watetezi Yanga wanatarajiwa kuanza mzunguko wa Pili wa ligi kesho kwa kucheza na wabaya wao African Lyon. Yanga watashuka dimbani wakiwa na kumbukumbu ya kutoka sare na African Lyon katika mzunguko wa kwanza. Vijana hao wanaonolewa na Kostadin Papic maarufu kama Clinton watakuwa na kibarua cha kuanza vizuri hatua hii ya lala kwa buriani.
MISAADA YAANZA KUWASILI NCHINI HAITI!!!!


Mashirika mbalimbali ya Misaada yameanza kupeleka misaada nchini Haiti kuwasaidia manusuru wa janga la Tetemeko la Ardhi ambalo limepiga nchi hiyo. Manusura wengi wanahitaji maji, chakula, malazi pamoja na msaada wa matibabu wa haraka.
Takwimu za Shirika la Msalaba Mwekundu zinaonesha watu zaidi ya elfu 50 wamepoteza maisha huku majeruhi wakiwa milioni 3.
Miili imeendelea kuzagaa katika mitaa ya nchi hiyo kutokana na zoezi la kuikosanya kwenda taratibu kutokana na kukosekana kwa vifaa vya kutosha na vya uhakika.
Thursday, January 14, 2010
ANGOLA YAWEKA HAI MATUMAINI YA KUTINGA ROBO FAINALI



Wenyeji wa Michuano ya AFCON Angola wameweka hai matumaini ya kutinga katika hatua ya Robo Fainali baada ya kushinda mchezo wake dhidi ya Malawi. Angola ambao katika mchezo wa kwanza waliambulia sare ya magoli 4-4 dhidi ya Mali wameshinda mchezo wao dhidi ya Malawi kwa 2-0. Magoli ya Angola yamefungwa na washambuliaji wake hatari Flavio na Manucho.
MALI HOI MBELE YA ALGERIA - AFCON!!!


Hatimaye Algeria inakuwa Timu ya kwanza miongoni mwa tano ambazo zitaiwakilisha Afrika kwenye Kombe la Dunia kupata ushindi. Algeria wamefanikiwa kuvuna ushindi baada ya kuifunga Mali kwa goli moja kwa buyu. Goli hilo la Wawakilishi hao wa Bara la Afrika kwenye Dimba la Kombe la Dunia limefungwa na Rafik Halliche akiunga mpira wa faulo uliopigwa na Karim Ziani
Subscribe to:
Posts (Atom)










































