RAIS Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatatu, Novemba 29, 2010, amekutana rasmi kwa mara ya kwanza na Baraza la Mawaziri lake jipya pamoja na Naibu Mawaziri na kuwapa maelekezo ya awali ya nini anakitarajia kutoka kwa wateule wake hao.
Mawaziri wote 29 na Naibu Mawaziri wote 21 ambao Rais Kikwete aliwaapisha rasmi kushika nyadhifa zao katika sherehe iliyofanyika Jumamosi iliyopita, Novemba 27, 2010, wamehudhuria mkutano huo kwenye Chumba cha Baraza la Mawaziri, Ikulu, Dar es Salaam.
Katika mkutano huo uliochukua kiasi cha saa tatu, Rais alianza kwa kuwaeleza mawaziri kuwa katika kipindi hiki cha pili cha uongozi wake hakutakuwepo na muda wa kupoteza, na wala hatakuwa tayari kukubali maelezo ya kwa nini utekelezaji wa majukumu ya msingi umeshindikana.
Kwa mara nyingine amewapongeza Mawaziri na Naibu Mawaziri hao akisisitiza: “Mnastahili pongezi hasa ukizingatia ukweli kwamba nyinyi mmebahatika kuteuliwa kutoka kwenye orodha ndefu ya wabunge wengi wenye sifa za kushika nafasi mlizo nazo. Nimewateua kwa imani kuwa pamoja nanyi, tutatimiza matumaini ya wananchi wa Tanzania waliokichagua Chama cha Mapinduzi kiendelee kuongoza nchi yetu.”
Ameongeza: “Ni imani yangu kuwa kwa mshikamano na ushirikiano wetu kama timu moja ya ushindi, tutatekeleza majukumu yote kwa uadilifu, uaminifu na ufanisi wa hali ya juu. Ufanisi wa Waziri ama Naibu Waziri katika utekelezaji wa majukumu yake unategemea sana ufahamu na uelewa wake wa masuala muhimu yanayohusu Nchi, Serikali na Wizara anayoiongoza.”
Katika mkutano huo ambao ameuelezea kama wa Utangulizi wakati inaandaliwa Semina Elekezi, Rais Kikwete amewaelezea wateule wake maana ya Baraza la Mawaziri na majukumu yake, na kutaka kila Waziri ahakikishe anatayarisha kalenda yake ya masuala muhimu ambayo anataka yajadiliwe na Baraza la Mawaziri kwa mwaka.
Rais Kikwete pia amewaeleza wateule wake kuhusu wajibu wa Mawaziri katika Bunge akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila waziri kuhudhuria vikao vyote vya Bunge, na kuwa ndani ya Bunge mawaziri wote wa Serikali lazima wawajibike kwa pamoja.
“Ni muhimu ieleweke kuwa kama ilivyo kwa maamuzi ya Baraza la Mawaziri, uwajibikaji wa Mawaziri Bungeni ni wa Pamoja. Kwa hiyo, Hoja ya Serikali Bungeni ni Hoja ya Mawaziri Wote na siyo Waziri anayewasilisha hoja tu,” amesema Rais Kikwete.
Rais pia amewakumbusha wateule wake kuhusu uwajibikaji wa pamoja (collective responsibility) katika kuongoza nchi, akisisitiza kuwa uwajibikaji huo unaelezwa kwa ufasaha katika Hati Maalum (Instrument) ya Majukumu ya kila Wizara.
Kuhusu uhusiano kati ya Waziri na Rais, na kati ya Waziri na Waziri Mkuu, Rais amesema kuwa pamoja na kwamba shughuli zote za utendaji Serikalini hutekelezwa kwa niaba ya Rais, lazima mawaziri wakumbuke kuwa Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa shughuli za kila siku za Serikali.
Rais Kikwete pia ametaka kujengeka mahusiano mazuri kati ya Waziri na Naibu Waziri wake akisisitiza: “Jambo la msingi la kuzingatia ni kwamba uhusiano mzuri baina ya viongozi hawa ni nguzo muhimu katika mafanikio ya Wizara. Kwa hiyo, ili kuepuka migongano katika utekelezaji ni muhimu mipaka ya kazi za Waziri na Naibu Waziri ikaheshimika na pia ni wajibu wa Waziri kumpangia kazi Naibu Waziri katika Wizara husika.
Katika mkutano huo, Rais Kikwete pia amezungumzia uhusiano kati ya Waziri na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Waziri wa Nchi Asiyekuwa na Portfolio na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Naibu Waziri na Katibu Mkuu, na uhusiano kati ya Waziri na Waziri wa Sekta Nyingine.
Rais Kikwete pia amefafanua kuhusu uhusiano kati ya Wizara na Wadau Wengine; uhusiano baina ya Wizara, Mikoa na Halmashauri; uhusiano na Taasisi Zilizo Chini ya Wizara; uhusiano na Wasaidizi wa Mawaziri pamoja na utekelezaji wa Maagizo ya Viongozi wa Kitaifa.
Rais Kikwete pia amewaeleza Mawaziri na Naibu Mawaziri kuhusu nyaraka muhimu ambazo wanapaswa kukabidhiwa na kuzipitia watakapofika kwenye nafasi zao mpya za kazi. Nyaraka hizo ni pamoja na Taarifa ya Makabidhiano ya Ofisi, Katiba, Ilani ya Chama Tawala, Dira ya Taifa, na Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA).
Aidha, Rais Kikwete amewaeleza wateule wake kuhusu umuhimu wao kufahamu Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu, Mikakati, Mipangomkakati, Mpango na Bajeti ya Wizara, Mpango wa Kazi wa Wizara na Masharti ya Kazi ya Waziri.
Rais Kikwete vile vile amekumbusha Mawaziri na Naibu Mawaziri wake kuwa suala la vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.
Pia amewataka Mawaziri kusimamia mapato ya Serikali yasiyotokana na kodi na kudhibiti matumizi ya Serikali.
Rais Kikwete pia amewataka viongozi hao kuzingatia maadili ya uongozi ikiwa ni pamoja na kusimamia sheria za nchi, kuheshimu sheria katika shughuli na mambo yao binafsi na pia kutunza siri za Serikali kwa mujibu wa kiapo chao.
Rais Kikwete pia amesisitiza umuhimu wa Mawaziri na Naibu Mawaziri kuwasiliana na wananchi kwa maana ya kueleza mafanikio ya Serikali na mipango ya Serikali katika kushughulikia matatizo ya wananchi.
Amewataka kuvitumia kikamilifu Vitengo vya Mawasiliano ya Serikali katika wizara zao ambavyo ndivyo vyenye jukumu la kutoa taarifa kuhusu Wizara inavyotelekeza majukumu yake.
“Uzoefu unaonyesha kuwa Mawaziri wengi ni wazito kufanya mawasiliano na wananchi hata pale ambako Wizara imefanya mambo mengi mazuri. Hivyo, Mawaziri muwe mstari wa mbele kuelezea mafanikio ya utendaji wa Serikali katika Wizara zetu,” ameelekeza Rais Kikwete na kuongeza:
“Lazima ujengwe utamaduni wa kudumu wa kuwasiliana na wananchi wote ambao ndio waajiri wetu kupitia kura zao. Mawaziri wote tumieni Vitengo vyenu vya Mawasiliano na vyombo vya habari kwa ustadi ipasavyo,” amefafanua Rais Kikwete.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
Tuesday, November 30, 2010
BARCELONA YAISHUSHIA MAAFA REAL MADRID!!
Monday, October 11, 2010
MATOKEO YA SYNOVATE YASHUKIWA!!!
CUF – Chama cha Wananchi tumesikitishwa na taarifa ya utafiti wa taasisi ya Synovate iliyotolewa jana Oktoba 10, jijini Dar es Salaam na kuripotiwa na vyombo vya habari leo hii namna inavyojichanganya, kwani idadi ya wanaomkubali Mgombea Urais wa Chama cha Mapinduzi Jakaya Kikwete ni wengi kuliko vyama vingine, wakati huo huo wanaokiri kutoridhishwa na huduma zake ni wengi.
Kwa mujibu wa vyombo vya Habari, ripoti hiyo inaonyesha Dkt. Jakaya Kikwete anakubalika kwa asilimia 61, Dkt. Willbrod Slaa ana asilimia 16 na Prof. Ibrahim Lipumba ana asilimia 5, lakini wakati huo huo inaeleza ripoti hiyo kuwa katika utendaji wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete watu wengi waliohojiwa hawakuridhika na huduma zinazotolewa katika upatikanaji wa ajira (84%), bei za vyakula (72%), maji safi ya kunywa (49%), afya(48%), mapambano dhidi ya rushwa(61%) na mapambano dhidi ya kuondoa umasikini(86%).
Katika ripoti hiyo hiyo, pamoja na kuonyesha wananchi wasivyoridhishwa na utendaji wa serikali hiyo ya Jakaya Kikwete, lakini bado wana imani na Rais Kikwete kwa asilimia 84, Baraza la Mawaziri (68%), Jeshi la Polisi (45%), Baraza la Mitihani (50%), mahakama (52), taasisi za huduma za afya (50%), TAKUKURU (46%) na vyama vya upinzani (48%).
Kwa upande wa elimu ya msingi ripoti inaonyesha kuwa wanaoridhika na utolewaji bora wa elimu ni asilimia 82, na kwa elimu ya sekondari wanaoridhika na utolewaji wa elimu bora ni asilimia 77.
CUF – Chama cha Wananchi tunasema iwapo kama ni kweli taarifa iliyoripotiwa ndivyo ilivyo tunasikitishwa namna taaluma ya utafiti inavyotumika vibaya, kwani hayamkiniki mtu mwenye akili timamu hata kama hakwenda shule, hata awe mtoto wako nyumbani, wakati akijua fika, tena kwa uhakika kwamba wewe umeshindwa kumpatia huduma muhimu (kama ripoti inavyoonyesha) na akawa bado eti ana imani na wewe na watendaji wako, huu ni uzushi mtupu.
CUF – Chama cha Wananchi tunaitaka taasisi ya Syonovate iwaombe radhi watanzania, kwani ripoti yao inaonyesha kuwa, wananchi wa nchi hii bado ni mbumbumbu wa kumpenda mtu kwa sura yake na wakaendelea kuwa na imani nae hata kama wanatambua fika ameshindwa kuwapatia huduma muhimu, huku ni kuwadhalilisha Watanzania na kazi kubwa inayofanywa na vyama vya upinzani, taasisi zisizo za kiserikali na vyombo vya habari juu ya kuelimisha umma.
CUF – Tunawatahadharisha Watanzania kuwa makini katika kipindi hiki cha uchaguzi, kwani taasisi mamluki zitatumia taaluma zao kuwapotosha na kuwavunja moyo mliokuwa nao wakukataa ufisadi na dhuluma inayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi dhidi ya mali asili na mapato ya nchi, ili siku ya uchaguzi Oktoba 31, wananchi msijitokeze kwa wingi kwa kudhani kuwa CCM bado inakubalika, TUNAWASIHI WANANCHI WA TANZANIA WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA, JITOKEZENI KWA WINGI SIKU YA KUPIGA KURA NA MFANYE MAAMUZI SAHIHI YA KULETA MABADILIKO.
Kwa mujibu wa vyombo vya Habari, ripoti hiyo inaonyesha Dkt. Jakaya Kikwete anakubalika kwa asilimia 61, Dkt. Willbrod Slaa ana asilimia 16 na Prof. Ibrahim Lipumba ana asilimia 5, lakini wakati huo huo inaeleza ripoti hiyo kuwa katika utendaji wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete watu wengi waliohojiwa hawakuridhika na huduma zinazotolewa katika upatikanaji wa ajira (84%), bei za vyakula (72%), maji safi ya kunywa (49%), afya(48%), mapambano dhidi ya rushwa(61%) na mapambano dhidi ya kuondoa umasikini(86%).
Katika ripoti hiyo hiyo, pamoja na kuonyesha wananchi wasivyoridhishwa na utendaji wa serikali hiyo ya Jakaya Kikwete, lakini bado wana imani na Rais Kikwete kwa asilimia 84, Baraza la Mawaziri (68%), Jeshi la Polisi (45%), Baraza la Mitihani (50%), mahakama (52), taasisi za huduma za afya (50%), TAKUKURU (46%) na vyama vya upinzani (48%).
Kwa upande wa elimu ya msingi ripoti inaonyesha kuwa wanaoridhika na utolewaji bora wa elimu ni asilimia 82, na kwa elimu ya sekondari wanaoridhika na utolewaji wa elimu bora ni asilimia 77.
CUF – Chama cha Wananchi tunasema iwapo kama ni kweli taarifa iliyoripotiwa ndivyo ilivyo tunasikitishwa namna taaluma ya utafiti inavyotumika vibaya, kwani hayamkiniki mtu mwenye akili timamu hata kama hakwenda shule, hata awe mtoto wako nyumbani, wakati akijua fika, tena kwa uhakika kwamba wewe umeshindwa kumpatia huduma muhimu (kama ripoti inavyoonyesha) na akawa bado eti ana imani na wewe na watendaji wako, huu ni uzushi mtupu.
CUF – Chama cha Wananchi tunaitaka taasisi ya Syonovate iwaombe radhi watanzania, kwani ripoti yao inaonyesha kuwa, wananchi wa nchi hii bado ni mbumbumbu wa kumpenda mtu kwa sura yake na wakaendelea kuwa na imani nae hata kama wanatambua fika ameshindwa kuwapatia huduma muhimu, huku ni kuwadhalilisha Watanzania na kazi kubwa inayofanywa na vyama vya upinzani, taasisi zisizo za kiserikali na vyombo vya habari juu ya kuelimisha umma.
CUF – Tunawatahadharisha Watanzania kuwa makini katika kipindi hiki cha uchaguzi, kwani taasisi mamluki zitatumia taaluma zao kuwapotosha na kuwavunja moyo mliokuwa nao wakukataa ufisadi na dhuluma inayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi dhidi ya mali asili na mapato ya nchi, ili siku ya uchaguzi Oktoba 31, wananchi msijitokeze kwa wingi kwa kudhani kuwa CCM bado inakubalika, TUNAWASIHI WANANCHI WA TANZANIA WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA, JITOKEZENI KWA WINGI SIKU YA KUPIGA KURA NA MFANYE MAAMUZI SAHIHI YA KULETA MABADILIKO.
Saturday, September 18, 2010
MHANGA WA UBUNGE AUKWAA UKUU WA WILAYA!!!
Thursday, September 16, 2010
TAKUKURU YATAKIWA KUUNGWA MKONO KWENYE SHUGHULI ZAKE!!!
Katibu Mkuu Ikulu, Bwana Michael Mwanda amewahimiza wananchi wa Mkoa wa Lindi, viongozi, Asasi Zisizo za Kiserikali pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini mkoani humo, kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa vile jukumu la kupambana na rushwa ni la Watanzania wote.
“Jukumu la kupambana na rushwa ni letu sote na ndiyo maana kwa kutambua hilo, nipo hapa leo kuwaunga mkono katika mapambano dhidi ya rushwa. Napenda nitumie nafasi hii pia kuwahamasisha wananchi wote wa Mkoa wa Lindi pamoja na viongozi wenzangu kuwaunga mkono TAKUKURU katika mapambano haya mazito”, amesema.
Bwana Mwanda amebainisha hayo mjini Lindi 16 Septemba, 2010 akiwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la ofisi za TAKUKURU mkoani humo, iliyohudhuriwa pia na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Asasi Zisizo za Kiserikali.
Katika hotuba yake, Bwana Mwanda amesema hatua ya TAKUKURU kujenga jengo la ofisi katika Mkoa wa Lindi, inatokana na dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kuimarisha utawala bora na kuboresha utendaji wa kazi wa taasisi hiyo, kwa vile siku zote lengo la Serikali ni kupeleka huduma karibu na wananchi.
“…lengo la Serikali yetu siku zote limekuwa ni kupeleka huduma karibu na wananchi ili waweze kufanya shughuli zao za kimaendeleo kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba kero ya rushwa inadhibitiwa vilivyo katika kila kona ya nchi yetu”, amebainisha Bwana Mwanda.
Amesema vita ya kuzuia na kupambana na rushwa ni kubwa inayohitaji umakini, moyo wa kujitolea na kujituma, na wakati mwingine kukubali lawama, hivyo Serikali imeona umuhimu wa kuboresha mazingira ya kazi ya watumishi wa TAKUKURU ili waweze kutoa huduma zilizo bora zaidi.
Bwana Mwanda amewatanabaisha viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kuwaelimisha waumini wao na hasa vijana kuhusu ubaya wa rushwa, na amewashauri kutumia nafasi waliyo nayo kutoa elimu ya maadili mema kwa waumini ili waepukane na maovu, hivyo kusaidia kwa kiwango kikubwa kujenga jamii adilifu na inayochukia vitendo vya rushwa.
Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 31, 2010, Bwana Mwanda amewahimiza wananchi kuzingatia matakwa ya sheria zinazosimamia masuala ya rushwa katika uchaguzi, ili kuhakikisha kuwa uchaguzi huo haugubikwi na vitendo vya rushwa.
Ili kuhakikisha kuwa TAKUKURU inapata mafanikio zaidi, Bwana Mwanda ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha Kamati za Uadilifu zilizopo katika Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri za Wilaya, kuzishirikisha Asasi Zisizo za Kiserikali katika vita dhidi ya rushwa katika ngazi hizo, kuendelea kujenga uwezo wa watumishi wake, na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu rushwa.
“Jukumu la kupambana na rushwa ni letu sote na ndiyo maana kwa kutambua hilo, nipo hapa leo kuwaunga mkono katika mapambano dhidi ya rushwa. Napenda nitumie nafasi hii pia kuwahamasisha wananchi wote wa Mkoa wa Lindi pamoja na viongozi wenzangu kuwaunga mkono TAKUKURU katika mapambano haya mazito”, amesema.
Bwana Mwanda amebainisha hayo mjini Lindi 16 Septemba, 2010 akiwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la ofisi za TAKUKURU mkoani humo, iliyohudhuriwa pia na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Asasi Zisizo za Kiserikali.
Katika hotuba yake, Bwana Mwanda amesema hatua ya TAKUKURU kujenga jengo la ofisi katika Mkoa wa Lindi, inatokana na dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kuimarisha utawala bora na kuboresha utendaji wa kazi wa taasisi hiyo, kwa vile siku zote lengo la Serikali ni kupeleka huduma karibu na wananchi.
“…lengo la Serikali yetu siku zote limekuwa ni kupeleka huduma karibu na wananchi ili waweze kufanya shughuli zao za kimaendeleo kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba kero ya rushwa inadhibitiwa vilivyo katika kila kona ya nchi yetu”, amebainisha Bwana Mwanda.
Amesema vita ya kuzuia na kupambana na rushwa ni kubwa inayohitaji umakini, moyo wa kujitolea na kujituma, na wakati mwingine kukubali lawama, hivyo Serikali imeona umuhimu wa kuboresha mazingira ya kazi ya watumishi wa TAKUKURU ili waweze kutoa huduma zilizo bora zaidi.
Bwana Mwanda amewatanabaisha viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kuwaelimisha waumini wao na hasa vijana kuhusu ubaya wa rushwa, na amewashauri kutumia nafasi waliyo nayo kutoa elimu ya maadili mema kwa waumini ili waepukane na maovu, hivyo kusaidia kwa kiwango kikubwa kujenga jamii adilifu na inayochukia vitendo vya rushwa.
Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 31, 2010, Bwana Mwanda amewahimiza wananchi kuzingatia matakwa ya sheria zinazosimamia masuala ya rushwa katika uchaguzi, ili kuhakikisha kuwa uchaguzi huo haugubikwi na vitendo vya rushwa.
Ili kuhakikisha kuwa TAKUKURU inapata mafanikio zaidi, Bwana Mwanda ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha Kamati za Uadilifu zilizopo katika Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri za Wilaya, kuzishirikisha Asasi Zisizo za Kiserikali katika vita dhidi ya rushwa katika ngazi hizo, kuendelea kujenga uwezo wa watumishi wake, na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu rushwa.
SIMBA YAZOA POINTI TATU WAKATI YANGA IKICHECHEMEA!!!
CUF WALAANI KUPIGWA KWA MWANDISHI KWENYE KAMPENI!!!
CUF – Chama cha Wananchi tumesikitishwa na kitendo cha mwandishi wa gazeti la Mwananchi Fredrick Katulanda, kuvamiwa na kushambuliwa na kikosi cha “janjaweed” wa Chama cha Mapinduzi wanatambulika kama “Green Guard” na kumjeruhi, katika kampeni za Ubunge katika jimbo la Sumve, Kijiji cha Nyambiti.
Walinzi hao walimshambulia mwandishi huyo na kumjeruhi sehemu za puani na mdomoni wakati wakimtaka yeye na wanataaluma wengine wa fani ya uandishi waondoke kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge wa Jimbo hilo la Sumve, wilayani Kwimba.
CUF – Chama cha Wananchi tunalaani, kitendo hicho kuwa siyo cha kiungwana hata kidogo, licha ya kuhatarisha amani ya nchi lakini pia ni ukiukwaji mkubwa wa maadili na haki za binadamu cha kuwapiga waandishi wakiwa kazini.
CUF – Chama cha Wananchi tunatambua kuwa, vitendo hivi vimefanywa na Chama cha Mapinduzi, kutokana na mazoea ya kubebwa kwa kuripotiwa habari zao kwa kupambwa zaidi kuliko uhalisia, hivyo pindi waandishi wanapofuata maadili ya taaluma yao na kuripoti habari kama zilivyo, inakuwa nongwa kwa CCM, na kupanda jazba hatimaye kujichukulia sheria mikononi mwao.
CUF – Tunaviomba vyombo vyote vinavyohusika, kuwachukulia hatua kali Chama cha Mapinduzi, kwa uvunjifu huu wa amani, ukiukwaji wa maadili wakati wa kampeni na kwa vile ni vitendo vya jinai, tunalisihi jeshi la Polisi kuhakikisha wale wote waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa Chama hicho.
CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa makini na chama hiki kinachoashiria uvunjivu wa amani iliyoasisiwa na wazee wetu, kwani hata ukiangalia baadhi ya mabango yao ya kampeni yanatoa vitisho kwenu wapiga kura ili msichague chama kingine iwapo kama mnataka amani, hii ina maana kuwa wapo tayari kuvunja amani iliyopo iwapo hawatachaguliwa.
HAKI SAWA KWA WOTE
Walinzi hao walimshambulia mwandishi huyo na kumjeruhi sehemu za puani na mdomoni wakati wakimtaka yeye na wanataaluma wengine wa fani ya uandishi waondoke kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge wa Jimbo hilo la Sumve, wilayani Kwimba.
CUF – Chama cha Wananchi tunalaani, kitendo hicho kuwa siyo cha kiungwana hata kidogo, licha ya kuhatarisha amani ya nchi lakini pia ni ukiukwaji mkubwa wa maadili na haki za binadamu cha kuwapiga waandishi wakiwa kazini.
CUF – Chama cha Wananchi tunatambua kuwa, vitendo hivi vimefanywa na Chama cha Mapinduzi, kutokana na mazoea ya kubebwa kwa kuripotiwa habari zao kwa kupambwa zaidi kuliko uhalisia, hivyo pindi waandishi wanapofuata maadili ya taaluma yao na kuripoti habari kama zilivyo, inakuwa nongwa kwa CCM, na kupanda jazba hatimaye kujichukulia sheria mikononi mwao.
CUF – Tunaviomba vyombo vyote vinavyohusika, kuwachukulia hatua kali Chama cha Mapinduzi, kwa uvunjifu huu wa amani, ukiukwaji wa maadili wakati wa kampeni na kwa vile ni vitendo vya jinai, tunalisihi jeshi la Polisi kuhakikisha wale wote waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa Chama hicho.
CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa makini na chama hiki kinachoashiria uvunjivu wa amani iliyoasisiwa na wazee wetu, kwani hata ukiangalia baadhi ya mabango yao ya kampeni yanatoa vitisho kwenu wapiga kura ili msichague chama kingine iwapo kama mnataka amani, hii ina maana kuwa wapo tayari kuvunja amani iliyopo iwapo hawatachaguliwa.
HAKI SAWA KWA WOTE
RAFAEL NADAL AENDELEA KUSHEREHEKEA TAJI LA US OPEN!!!

Mchezaji ambaye anaorodheshwa katika nafasi ya kwanza upande wa wanaume kwa Mchezo wa Tennis na Bingwa wa US Open Rafael Nadal ameendelea kusherehekea ubingwa wake na hapa ilikuwa katika Uwanja wa Sabtiago Bernabeu kabla ya kuchezwa kwa mchezo wa Ligi ya Mabingwa kati ya Real Madrid na Ajax Amsterdam.
MAUAJI YAFANYIKA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA!!!
CUF NA MATOKEO YA UTAFITI YA SYNOVTE!!!
CUF – Chama cha Wananchi tumefarijika kwa taarifa iliyosahihi inayoelezea hali halisi ya utolewaji wa Habari za kampeni katika vyombo vya Habari, iliyoripotiwa na Meneja taasisi ya Synovate Bi. Jane Meela jana Jumanne, Septemba 14, jijini Dar es Salaam.
Taarifa hiyo ambayo imeripotiwa katika vyombo vya Habari imebainisha kwamba, katika utafiti wao wa pili Taasisi ya Synovate imegundua kuwa katika kampeni zinazoendelea Magazeti yameegemea kuripoti zaidi Chama cha Mapinduzi (CCM) na kufuatiwa na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA) na kuviacha vyama vingine pasipo kupewa kipaumbele.
Taarifa hiyo imesema kuwa vyombo vya televisheni havikulalia upande wowote, taarifa zao wanazozitoa zinatoa kipaumbele kwa vyama mbalimbali (neutral) tofauti na vyombo vya magazeti, na isitoshe suala la amani limekuwa likizungumziwa zaidi katika kampeni zilizoripotiwa, halikadhalika Chama cha CHADEMA kilimepata kipaumbele mara baada ya kumtangaza mgombea wake wa Urais.
CUF – Chama cha Wananchi pamoja na kufarijika kwa ripoti hii ya Synovate ambayo inausahihi ndani yake, lakini pia tunamasikitiko kwa vyombo hivyo vya habari kwani pamoja na nia nzuri ya kuongozana na baadhi ya waandishi wao katika ziara za kampeni zetu za mgombea Urais na mgombea mwenza, lakini bado kipaumbele kimeelekezwa zaidi kwa wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA).
CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa dhamira ya makusudi inayofanywa na vyombo vingi vya habari (ukiacha vichache), hususani magazeti ni kujaribu kuonyesha kuwa upinzani uliopo katika uchaguzi mwaka huu kwa Tanzania Bara, ni baina ya CCM na CHADEMA, na kwa upande wa Zanzibar ni baina ya CCM na CUF, jambo ambalo halina ukweli kabisa.
CUF – Tunatambua kuwa harakati hizi hazikuanza leo, kwani waandishi walidiriki kulitamka hili bayana katika mikutano yetu na waandishi wa habari mapema mwaka jana 2009, kabla ya kuumbuliwa na matokeo ya uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji zilizofanyika mwishoni mwa Oktoba mwaka jana, ambapo pamoja na taarifa halisi za matokeo hayo kutotangazwa na wizara ya TAMISEMI (kwa kuchelea kuumbuka), bado chama chetu kilifanya zizuri kuliko chama kingine chochote cha upinzani.
Ikiwa hata mwaka haujatimia tangu uchaguzi huo kufanyika, hayamkiniki kigezo kinachotumika na baadhi ya vyombo hivi vya habari kukipa kipaumbele chama ambacho kiliambulia mitaa saba tu, katika jiji hili la Dar es Salaam, na chama chetu kufanikiwa kuchukua mitaa 34, ambapo maeneo yaliyokuwa ni ngome zetu kuu ambayo ni wastani wa robo tatu wa wagombea wetu walienguliwa.
CUF – Tunavisihi vyombo vya Habari pamoja na kuifanyia kazi kamilifu ripoti ya Synovate, wazingatie maadili ya uandishi wa habari, jambo ambalo wamekuwa wakiliahidi na kujivuna nalo, hatupendi matukio ya mwaka 2005 ya wananchi wenye hasira kali kukosa imani na vyombo hivyo, yakajirudia katika uchaguzi huu.
HAKI SAWA KWA WOTE
Taarifa hiyo ambayo imeripotiwa katika vyombo vya Habari imebainisha kwamba, katika utafiti wao wa pili Taasisi ya Synovate imegundua kuwa katika kampeni zinazoendelea Magazeti yameegemea kuripoti zaidi Chama cha Mapinduzi (CCM) na kufuatiwa na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA) na kuviacha vyama vingine pasipo kupewa kipaumbele.
Taarifa hiyo imesema kuwa vyombo vya televisheni havikulalia upande wowote, taarifa zao wanazozitoa zinatoa kipaumbele kwa vyama mbalimbali (neutral) tofauti na vyombo vya magazeti, na isitoshe suala la amani limekuwa likizungumziwa zaidi katika kampeni zilizoripotiwa, halikadhalika Chama cha CHADEMA kilimepata kipaumbele mara baada ya kumtangaza mgombea wake wa Urais.
CUF – Chama cha Wananchi pamoja na kufarijika kwa ripoti hii ya Synovate ambayo inausahihi ndani yake, lakini pia tunamasikitiko kwa vyombo hivyo vya habari kwani pamoja na nia nzuri ya kuongozana na baadhi ya waandishi wao katika ziara za kampeni zetu za mgombea Urais na mgombea mwenza, lakini bado kipaumbele kimeelekezwa zaidi kwa wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA).
CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa dhamira ya makusudi inayofanywa na vyombo vingi vya habari (ukiacha vichache), hususani magazeti ni kujaribu kuonyesha kuwa upinzani uliopo katika uchaguzi mwaka huu kwa Tanzania Bara, ni baina ya CCM na CHADEMA, na kwa upande wa Zanzibar ni baina ya CCM na CUF, jambo ambalo halina ukweli kabisa.
CUF – Tunatambua kuwa harakati hizi hazikuanza leo, kwani waandishi walidiriki kulitamka hili bayana katika mikutano yetu na waandishi wa habari mapema mwaka jana 2009, kabla ya kuumbuliwa na matokeo ya uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji zilizofanyika mwishoni mwa Oktoba mwaka jana, ambapo pamoja na taarifa halisi za matokeo hayo kutotangazwa na wizara ya TAMISEMI (kwa kuchelea kuumbuka), bado chama chetu kilifanya zizuri kuliko chama kingine chochote cha upinzani.
Ikiwa hata mwaka haujatimia tangu uchaguzi huo kufanyika, hayamkiniki kigezo kinachotumika na baadhi ya vyombo hivi vya habari kukipa kipaumbele chama ambacho kiliambulia mitaa saba tu, katika jiji hili la Dar es Salaam, na chama chetu kufanikiwa kuchukua mitaa 34, ambapo maeneo yaliyokuwa ni ngome zetu kuu ambayo ni wastani wa robo tatu wa wagombea wetu walienguliwa.
CUF – Tunavisihi vyombo vya Habari pamoja na kuifanyia kazi kamilifu ripoti ya Synovate, wazingatie maadili ya uandishi wa habari, jambo ambalo wamekuwa wakiliahidi na kujivuna nalo, hatupendi matukio ya mwaka 2005 ya wananchi wenye hasira kali kukosa imani na vyombo hivyo, yakajirudia katika uchaguzi huu.
HAKI SAWA KWA WOTE
Wednesday, September 15, 2010
MAMBO YALIVYOKUWA CHAMPIONS LEAGUE!!!
VALENCIA NJE MSIMU WOTE!!



Kiungo wa Pembeni wa Klabu ya Manchester United Antonio Valnecia huenda akawa nje ya Dimba kwa kipindi chote cha msimu kutokana na kuumia kifundo cha mguu kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Barani Ulaya dhidi ya Rangers uliopigwa kwenye Dimba la Old Trafford. Kocha Mkuu wa Man Utd Sir Alex Ferguson amethibitisha huenda mchezji huyo asipatikane hadi mwishoni mwa msimu!!!
Wednesday, September 1, 2010
AJALI ZA BARABARANI BADO NI TATIZO SUGU!!!!
Askari wa kikosi cha usalama barabarani wakipima ajali ya gari aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajiri T 544 AFY inayofanya safari zake kati ya Mtyangimbole na mjini Songea mara baada kufeli breki na dereva kulazimika kukata kona ya ghafla na kisha kuparamia ukuta wa hotel ya kufikia wageni ya Safina Lodge mjini Songea. Zaidi ya abiria 20 wamenusurika kifo katika ajali hiyo
Crista Komba mkazi wa mjini Songea mkoa wa Ruvuma, akipata matibabu katika hospitali ya mkoa mjini Songea baada ya kugongwa na gari aina ya Toyota Hiace yenye namba za usajiri T 544 AFY inayofanya safari zake kati ya Mtyangimbole na mjini Songea mara baada gari hilo kufeli breki na dereva kulazimika kukata kona ya ghafla na kisha kumgonga. Zaidi ya abiria 20 wamenusurika kifo katika ajali hiyo. (Picha zote na Emmanuel Msigwa, Songea)
Friday, August 20, 2010
WALIMU WATAKIWA KUACHA TABIA YA UMAMLUKI!!
NAIBU katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bw. Ezekiel Oluoch, akiongea na walimu wa shule za msingi na sekondari katika ukumbi wa Songea Club mjini hapa huku akiwataka walimu hao kuacha mara moja kuwa vibaraka wa wanasiasa kama wengi wao walivyogeuka kuwa makampeni meneja wa wagombea katika mchakato wa upigaji kura za maoni uliofanyika hivi karibuni. (Picha zote na Emmanuel Msigwa, Songea)
BALOTELLI AIBEBA MAN CITY, COLE AKIKOSA PENALTY!!


Michezo ya kusaka nafasi ya kushiriki katika hatua ya Makundi ya Mashindano ya Europa imeendelea na kushuhudia Manchester City ikichomoza na ushindi wa goli moja kwa nunge dhidi ya FC Timisoara kwa goli la Super Mario Balotelli. Vijogoo vya Jiji, Liverpool vimevuna ushindi wa goli moja kwa buyu mbele ya Trabzonspor huku Joe Cole akikosa mkwaju wa penalty!!!
GALLAS ATUA TOTTENHAM!!
Thursday, August 19, 2010
MAN CITY KUUZA WACHEZAJI WATATU!!




Kocha Mkuu wa Klabu ya Manchester City, Roberto Mancini ametangaza kuwa tayari kuwauza wachezaji watatu wa timu hiyo. Golikipa Shay Given baada ya Joe Hart kuonesha uwezo mkubwa, Mshambuliaji Roque Santa Cruz ambaye hana uhakika wa namba pamoja na Robinho ambaye kwa sasa anakipiga kwa mkopo katika Klabu ya Santos!!!
MASCHERANO KUONDOKA KWA ADA KUBWA YA UHAMISHO!!

Kocha wa Vijogoo vya Jiji Klabu ya Liverpool, Roy Hodgson amesema atamuuza kiungo ambaye hajatulia wa timu hiyo Javier Mascherano iwapo klabu ambazo zinamtaka zitatoa fungu kubwa kuweza kumnunua. Mascherano amemwambia Hodgson anataka kuondoka Anfield kwa sababu zake binafsi huku Inter Milan na Barcelona zikimwania!!!
Wednesday, August 18, 2010
JAMES MILNER AKAMILISHA USAJILI WAKE MAN CITY!!!
YANGA YATWAA NGAO YA HISANI!!!
ANELKA AUDHIKI UAMUZI WA FFF KUMFUNGIA!!!

Mshambuliaji wa Klabu ya Chelsea, Nicolas Anelka ameudhiaki uamuzi wa Kamati ya nidhamu ya Shirikisho la Kabumbu nchini Ufaransa FFF kumfungia michezo kumi na nane ya kimataifa baada ya kuwa chanzo cha kuzuka mtafaruku wakati wa fainali za Kombe la Dunia nchini Afrika Kusini. Anelka amesema vyote vinavyofanyika havina maana na vimekuja kwa sababu Kocha Mpya Laurent Blanc aweze kufanya kazi zake kwa amani!!!
ANELKA, EVRA, RIBERY NA TOULALAN WAFUNGIWA TIMU YA TAIFA!!!
Subscribe to:
Posts (Atom)






































