Thursday, January 5, 2012

ZITTO KABWE ATOA WARAKA KWA JUSSA RADU BAADA YA KUFUKUZWA KWA HAMAD RASHID!!!


Ndugu Jussa, Kama rafiki yako mkubwa na unajua ninavyomheshimu Maalim Seif Kama kiongozi thabiti. Leo nakwambia usilolipenda. Sio sahihi katika demokrasia Kama yetu kumfukuza Mbunge Hamad Rashid au hata wanachama wengine wa chama chenu cha CUF.

Kama Maalim aliweza kumsamehe Salmin, aliweza kumsamehe Karume, aliweza kukubali kutangazwa kushindwa ilhali hata wewe unajua alishinda Urais wa Zanzibar iweje iwe muhali kumaliza tatizo hili dogo la Hamad Rashid? Hamad ana makosa lukuki. Nimefanya naye kazi Bungeni.

Hamad pia ana mazuri mengi kafanya. Hamad amejitoa muhanga. Uamuzi wa Baraza Kuu la CUF kumfukuza uanachama ufikiriwe upya. That is my appeal to you as a friend and a fine politician.

No comments:

Post a Comment