Thursday, January 5, 2012

YAYA NA KOLO TOURE WATAKIWA KUJIUNGA NA KAMBI YA TIMU YA TAIFA!!


Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Ivory Coast Francois Zahoui ametaka wachezaji wawili wa timu hiyo wanaocheka katika Klabu ya Manchester City kujiunga mara moja na kikosi hicho kwa ajili ya maandailizi ya Kombe la Mataifa ya Afrika!! Yaya Toure na kakake Kolo Toure wanatakiwa wawe wamejiunga na kambi siku ya jumamosi huko Paris kabla ya kuelekea Abu Dhabi kwa Kambi!! Kocha wa Man City Roberto Mancini alikuwa anataka kuwatumia wacheza hao kwenye mchezo wa Kombe la FA siku ya jumapili dhidi ya Manchester United!!

No comments:

Post a Comment