Wednesday, January 4, 2012

MASHAHIDI 3,200 WAHOJIWA NA MAHAKAMA YA ICTR!!

Zaidi ya mashahidi 3,200 wameshatoa ushahidi katika kesi mbalimbali mbele ya Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) tangu mahakama hiyo ianze rasmi kusikiliza kesi za mauaji ya kimbari mwaka 1997.

Rais wa Mahakama hiyo Jaji Khalida Rachid Khan alieleza katika ripoti yake kwamba usikilizaji wa ushahidi wa mashahidi hao ulichukukua jumla ya masaa 26,000.

Chombo Maalum kitakachorithi kazi zitakazoachwa na ICTR kitaanza kazi rasmi Julai mosi, mwaka huu, na kitakuwa pamoja na mambo mengine na jukumu la kuhifadhi nyaraka lukuki ikiwa ni pamoja na kurasa 900,000 za kumbukumbu za maandishi za mahakama na rekodi za kaseti na video za zaidi ya siku za kusikiliza kesi 6,000. Chombo hicho pia kitatunza maamuzi na hukumu zaidi ya 10,000.

Akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa Desemba 7, 2011, juu ya maendeleo ya mkakati wa kuhitimisha kazi za ICTR, Jaji Khan aliahidi kwamba kesi katika ngazi ya mahakama ya awali yaani ICTR zitakamilika ifikapo Juni, 2012 ambapo kesi katika ngazi ya Mahakama ya Rufaa zitakamilika mwishoni mwa 2014.

No comments:

Post a Comment