Friday, August 13, 2010

UGONJWA WA AJABU WAWAKUMBA WANAFUNZI!!!


Baadhi ya wanafunzi wa darasa la Saba katika shule ya msingi ya Ilembula, wilaya mpya ya Wanging’ombe mkoa wa Njombe waliokumbwa na ugonjwa wa kuanguka na kupoteza fahamu wakiwa wamehifadhiwa katika moja ya darasa la shule hiyo kusubiri kurejea kwa fahamu zao baada ya kuanguka

Mwanafunzi wa darasa la saba katika shule ya msingi ya Ilembula, wilaya mpya ya Wanging’ombe mkoa wa Njombe aliyekumbwa na ugonjwa wa ajabu wa kuanguka na kupoteza fahamu akibebwa na wanafunzi wenzie kwa kushirikiana na Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Bi. Betty Simon (kulia) mara baada ya kuanguka na kumpeleka katika darasa lililotengwa kwa ajili ya kuwahifadhi waliokumbwa na ugonjwa huo.

Mwalimu mkuu wa shule ya Ilembula, wilaya mpya ya Wanging’ombe mkoa wa Njombe, Bi. Betty Simon (kushoto) akijaribu kumdaka mmoja wa wanafunzi wa darasa la Saba wa shule hiyo aliyekumbwa na ugonjwa wa kuanguka na kupoteza fahamu kabla hajaanguka chini.

Mmoja wa wanafunzi wa kike wa darasa la Saba katika shule ya msingi ya Ilembula, wilaya mpya ya Wanging’ombe mkoa wa Njombe aliyekumbwa na ugonjwa wa ajabu wa kuanguka na kupoteza fahamu akianguka mara baada ya kutoka chooni (kinachoonekena nyuma yake) kama alivyonaswa na mpiga picha wetu. (Picha kwa Hisani ya Emmanuel Msigwa)

No comments:

Post a Comment