Sunday, August 15, 2010

JIONEE MWENYEWE MAMBO YALIVYO!!!


Kutokana na miundombinu ya stendi kuu ya mabasi Songea kuwa mibovu imekuwa vigumu kwa magari makubwa kuingia na kutoka katika stendi hiyo kama inavyoonekana gari lenye namba za usajiri T 439 AJQ mali ya kampuni ya CocaCola likishindwa kutoka katika stendi hiyo na kusababisha adha kubwa kwa wengine.

Uuzaji wa mafuta ya kula wa mtindo huu umekuwa ukifananishwa na uchakachuaji wa mafuta ya Dizeli na Petroli ulioshamiri katika siku za hivi usoni kwani wananchi wengi wamekuwa wakilalamikia ubora wa mafuta hayo kupungua kutokana na kuuziwa ndani ya makopo

Watoto kutoka Shirika la Masista wa Maria Immaculata kutoka India (DMI) mkoa wa Ruvuma wakionesha umahili wa kucheza ngoma ya ukakamavu ya mganda katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa DMI iliyofanyika katika viwanja vya makumbusho ya Vita vya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea mwishoni mwa wiki.

Askofu mkuu jimbo Katoliki la Songea, Mhashamu Norbert Mtega akicheza na watoto wimbo wa kuliombea Taifa katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa DMI iliyofanyika katika viwanja vya makumbusho ya Vita vya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea mwishoni mwa wiki.

Mama mkuu wa Shirika la Masista wa Maria Immaculata kutoka India (DMI) Afrika, Sista Thianes (kushoto) akiteta jambo na Askofu mkuu jimbo Katoliki la Songea, Mhashamu Norbert Mtega katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa DMI iliyofanyika katika viwanja vya makumbusho ya Vita vya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea mwishoni mwa wiki.(Picha zote na Emmanuel Msigwa, Songea)

No comments:

Post a Comment