Tuesday, August 17, 2010

CUF YABADILI TAREHE YA KUMSINDIKIZA MGOMBEA WAO WA URAIS!!

CUF - Chama Cha Wananchi kinawatangazia Wananchi wote kuwa kutokana na mabadiliko yaliyofanywa na Tume ya Uchaguzi ya Taifa ya tarehe ya kurudisha fomu ya Urais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, hivyo basi Mgombea wa Urais Profesa Ibrahim Haruna Lipumba atarudisha fomu tarehe 19/08/2010.

Msafara huo utaanzia Ofisi ya Wilaya ya Ilala iliyopo Buguruni Shell saa 4.00 asubuhi na msafara huo utapitia barabara za Uhuru hadi Mnazi mmoja, Bibi Titi, Ohio, Ghana na kuingia Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Taifa.

CUF - Chama Cha Wananchi tunawaomba wanachama wote wanaopenda mabadiliko kujitokeza kwa wingi kumsindikiza Prof. Ibrahim Lipumba.

Aidha tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza kutokana na mabadiliko haya na hii imekuwa nje ya uwezo wetu.

No comments:

Post a Comment