Wednesday, March 3, 2010

TTC SONGEA MAMBO SI SHWARI!!!

Kikao cha Bodi ya Chuo cha Ualimu SONGEA kilichofanyika jumatano kwa siku nzima kimeshindwa kutoa hatma ya Mawaziri 10 wa serikali ya wananchuo waliosimamishwa masomo tangu mwishoni mwa mwezi NOVEMBER mwaka jana kwa madai ya kuchochea mgomo wa wachuo waliokuwa wakimpinga mwalimu wa maadili wa chuo hicho kuwavua madaraka mawaziri waliowachagua na kuwateua anaowataka yeye.

Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Chuo hicho ambaye ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa RUVUMA DR ANSERM TARIMO, ameonekana kugongana kimaelezo na Mkuu wa Chuo hicho MPELI MBOSA juu ya Sakata wakati wakihojiwa na waandishi wa habari.

DR TARIMO amesema Hatma ya wananchuo hao bado haijapatikana na kusisitiza ni lazima itafutwe haki kwanza, wakati Mkuu wa Chuo MPELI MBOSA amedai hatambui chochote kilichotokea wala Mkutano wa Maridhiano uliofanyika Octoba 27 mwaka jana na kutoa suluhu ambapo Mwalimu wa maadili wa Chuo hicho VALENTINE MAYAYA aliomba radhi kwa kuwa chanzo cha tatizo.

Kuhusu hatma ya wanafunzi waliosimamishwa ambao wanaendelea kuhangaika mjini SONGEA wakisubiri hatma yao Bw MBOSA amesema hilo halimhusu. (Taarifa kwa hisani ya Gerson Msigwa)

No comments:

Post a Comment