Sunday, March 21, 2010

MBINGA WAPATA NEEMA!!!

Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii NSSF katika Mkoa wa RUVUMA umekiri kukumbana na ugumu katika uongezaji wa idadi ya waajiri na wanachama wa hiari unaosababisha kupunguza makusanyo ya fedha.

Meneja wa NSSF Mkoani humo WAZIRI NDONDE amesema kumekuwa na mwitikio mdogo hasa kwa wananchi wa hiari licha ya juhudi kubwa zinazofanywa kutangaza manufaa ya wananchi kujiunga katika Mifumo ya Hifadhi za Jamii.

Akizungumza katika Hafla ya kihitimisha Juma la NSSF iliyohudhuriwa na wafanyakazi wa NSSF na Baadhi ya wateja wa Shirika hilo, Bw NDONDE amesema pamoja na kuwepo Changamoto hiyo, katika kipindi cha nusu mwaka zaidi ya shilingi milioni 560 kati ya lengo la shilingi bilioni 1 na milioni 200 zinazotarajiwa kukusanywa Mkoani RUVUMA.

Kuhusu malalamiko ya wanachama wa NSSF kuwa Mfuko huo umekuwa ukitoa mafao kidogo ikilinganishwa na mifuko mingine ya Hifadhi ya Jamii Meneja huyo amesema Serikali inaunda Chombo kitakachodhibiti viwango vya mafao ya mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Aidha amewaondoa shaka wanachama wa NSSF, kuwa Taarifa za shirika la wafanyakazi la kimataifa ILO zinaonesha kuwa viwango vianvyolipwa na NSSF vitaliwezesha shirika hilo kutoa mafao kwa miaka 50 baadaye ikilinganishwa na mashirika mengine ambayo yanakabiliwa na madeni makubwa (Habari kwa Hisani ya Gerson Msigwa)

No comments:

Post a Comment