Friday, March 12, 2010

DROGBA MCHEZAJI BORA WA AFRIKA!!!


Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tembo wa Afrika, Ivory Coast ambaye anakipiga katika klabu ya Chelsea, Didier Drogba ameibuka mchezaji bora wa mwaka na kuwabwaga Samuel Etoo (Cameroon) na Michael Essien (Ghana). TP Mazembe ni Klabu bora barani wakati Tresor Mputu naye akichukua tuzo ya uchezaji bora kwa wale ambao wanacheza ligi ya ndani. Algeria ni timu bora kwa ngazi ya timu ya Taifa wakati Masabiki wa Afrika Kusini, Bafana Bafana wakiwa na mavuvuzela yao wametajwa kama bora kwenye ushangiliaji.

No comments:

Post a Comment