Friday, December 30, 2011

BALOZI OMBENI YOHANA SEFUE ATEULIWA KUWA KATIBU MKUU KIONGOZI!!!


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Balozi Ombeni Yohana Sefue kuwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Balozi Sefue anachukua nafasi inayoachwa wazi na Bwana Phillemon Luhanjo ambaye anahitimisha mkataba wake wa utumishi wa umma kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011.

Kabla ya uteuzi wake, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, New York, Marekani. Kabla ya hapo, Balozi Sefue alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani na kabla ya hapo alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Canada tokea Oktoba 2005.

Balozi Sefue ataapishwa kesho, Jumamosi, Desemba 31, 2011 saa nne asubuhi, Ikulu, Dar es Salaam.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
30 Desemba, 2011

Thursday, December 29, 2011

PIGO KWA TASNIA YA HABARI TANZANIA JOHN NGAYHOMA AFARIKI DUNIA!!!


Mtangazaji wa zamani wa ITV/Radio One na Shirika la Utanagazaji la Uingereza BBC Kiswahili John Ngahyoma amefariki dunia mapema asubuhi ya leo!! Ngahyoma amefikwa na mauti akiwa Hospital ambako alikuwa anapatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefuna hata kulazimika kupekwa nchini India kwa matibabu lakini haikusaidia!! Kifo cha Ngahyoma kimekuja wakati Tasnia ya Habari ikiwa imepata pigo kubwa la kuondokewa na mwandishi wa Tbc Halima Mchuka!! Blogu hii imepokea kwa masikitiko makubwa sana kifo hicho!! Mwenyezimungu aiweke roho yake mahali panapostahili!! Ameen!!

RAIS KIKWETE ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA KIFO CHA HALIMA MCHUKA!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bwana Clement Mshana, kuomboleza kifo cha mtangazaji maarufu wa shirika hilo, Bi Halima Mohammed Mchuka ambaye alifariki dunia usiku wa kuamkia leo, Alhamisi, Desemba 29, 2011 kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.

“Nimepokea kwa huzuni habari za kifo cha Halima Mohammed Mchuka. Nakutumia wewe Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) salamu za dhati ya moyo wangu kuomboleza kifo chake. Nakuomba, kupitia kwako, uniwasilishie salamu zangu kwa wafanyakazi wenzake katika TBC ambao wamempoteza mwenzao na rafiki yao.”

Ameongeza Mheshimiwa Rais katika salamu zake, “Aidha, nataka kupitia kwako niwatumie salamu zangu za rambirambi wana-familia, ndugu na jamaa wote za marehemu. Wajulishe kuwa niko nao katika wakati huu wa maombolezo na kwamba msiba wao ni msiba wangu pia. Nawaomba wawe na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu kwa sababu yote ni mapenzi ya Mungu. Naungana nao kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, ailaze pema peponi roho ya marehemu. Amen.”

Mheshimiwa Rais pia amesema kuwa Bi. Mchuka ametoa mchango mkubwa katika nyanja ya utangazaji nchini. “Sote tutaendelea kukumbuka weledi wake, uzalendo wake na ujasiri wake katika utangazaji uliomsukuma kuwa Mwanamke wa Kwanza katika Tanzania kutangaza mechi za mpira wa miguu”.

Ameongeza Rais Kikwete: “Ni dhahiri kuwa nyanja ya utangazaji imeondokewa na mtu muhimu na namna nzuri zaidi ya kumuenzi Bi. Mchuka ni kwa watangazaji waliobakia kuendelea kuiga mfano wake katika ubora wa utangazaji nchini mwetu.”

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
29 Desemba, 2011

NGOMA MPYA YA TID INAITWA HANITAKI!!

MATUKIO YALIYOTOKEA KWENYE MAHAKAMA YA ICTR-ARUSHA!!!

Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) inaweza kusherehekea mwisho wa mwaka 2011 kwa kujivuna kutokana na hukumu nzito na nyingi zilizotolewa katika mwaka huo.

Mahakama hiyo imetoa jumla ya hukumu 10 katika ngazi zote mbili za mahakama ya awali na mahakama yake ya Rufaa zenye kuhusisha watu 21, akiwemo mwanamke pekee kuwahi kushitakiwa na mahakama hiyo, Pauline Nyiramasuhuko na mtu anayesadikiwa kuwa mpangaji mkuu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994,Kanali Theoneste Bagosora.

Hukumu za ICTR 2011

Gatete ahukumiwa kifungo cha maisha: Machi 29, 2011, ICTR ilianza mwaka mpya kwa kutoa hukumu yake ya kwanza katika kesi inayomkabili aliyekuwa afisa mwandamizi wa serikali ya Rwanda, Jean-Baptiste Gatete ambaye alitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari na kuteketeza kizazi. Alipewa adhabu ya kifungo cha maisha jela na kesi hiyo sasa iko mahakama ya Rufaa.

Aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi ahukumiwa kifungo cha miaka 30: Mei 17, 2011, Mahakama hiyo ya Umoja wa Mataifa ilitoa hukumu nyingine nzito katika kesi inayohusisha maafisa wanne wa zamani wa jeshi la Rwanda wakiwemo Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi hilo , Jenerali Augustin Bizimungu na Afisa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Polisi, Jenerali Augustin Ndindiliyimana.Majenerali hao walitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Bizimungu alihukumiwa kifungo cha miaka 30 jela huku mwenzake, Ndindiliyimana alipewa adhabu ya muda aliokwisha tumikia akiwa kizuizini tangu mwaka 2000.Aliachiwa huru mara moja.

Maafisa wengine waliotiwa hatiani ni pamoja na Mkuu wa Bataliani ya Usalama Jesheni, Meja Francois-Xavier Nzuwonemeye na Kapteni Innocent Sagahutu pia wa Bataliani hiyo ambao walipewa kila mmoja wao adhabu za vifungo vya miaka 20 jela baada ya kutiwa hatiani kwa uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Pande zote mbili za mwendesha mashitaka na utetezi zimekata rufaa.

Mwanamke pekee na wengine watano watiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari: Juni 24, 2011 ilikuwa siku ya pekee katika historia ya ICTR kwa kutoa hukumu ya kesi iliyokuwa na watuhumiwa wengi zaidi kuliko kesi yoyote katika mahakama hiyo.Kesi hiyo maarufu kwa jina la Kesi ya Butare, inajumuisha watuhumiwa sita akiwemo mwanamke pekee, Pauline Nyiramasuhuko, Waziri wa zamani wa Familia na Masuala ya Wanawake na mtoto wake wa kiume, Arsene Shalom Ntahobali. Wawili hao walihukumiwa vifungo vya maisha jela baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu ukiwemo ubakaji na kuteketeza kizazi na uhalifu wa kivita.

Wengine waliotiwa hatiani katika kesi hiyo ni pamoja na Eli Ndayambaje, aliyehukumiwa pia kifungo cha maisha jela, Alphonse Nteziryayo, alipewa adhabu ya kifungo cha miaka 30, Sylvain Nsabimana atatumikia miaka 25 jela ambapo Joseph Kanyabashi alipewa adhabu ya miaka 35 jela. Wote sita wanasubiri tarehe ya kusikilizwa kwa rufaa zao.

Mawaziri wawili waachiwa huru na wengine wawili watiwa hatiani: Septemba 30, 2011, hukumu nyingine ilitolewa katika kesi inayohusisha mawaziri wanne wa zamani wa Rwanda katika serikali ya mpito ya mwaka 1994. Mahakama iliwaachia huru mawaziri wawili ikiwa ni pamoja na Casimir Bizimungu (Afya) na Jerome Bicamumpka (Mambo ya Nje). Waliotiwa hatiani ni Justin Mugenzi (Biashara) na Prosper Mugiraneza (Utumishi wa Umma) ambao kila mmoja wao alipewa adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka 30 jela baada ya kutiwa hatiani kwa kula njama za kufanya mauaji ya kimbari na uchohezi.Kama ilivyokuwa kwa wote waliotiwa hatiani nao wamekata rufaa kupinga hukumu hiyo.

Meya wa zamani ahukumiwa kifungo cha miaka 15 jela: Novemba 17, 2011 Mahakama pia ilitoa hukumu nyingine katika kesi ya meya wa zamani nchini Rwanda, Gregoire Ndahimana. Alitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari na ukatili dhidi ya binadamu na kuhukumiwa adhabu ya kifungio cha miaka 15.Anasubiri kupangiwa tarehe ya kusikilizwa rufaa yake.

Wanasiasa vigogo wawili wa Rwanda kutumikia jela maisha: Desemba 21, 2011 ICTR ilitoa hukumu ya mwisho kwa mwaka huu katika kesi ya wanasiasa wawili wa kilichokuwa chama tawala cha MRND wakati wa mauaji ya kimbari ikiwa ni pamoja na Rais wa chama hicho Mathieu Ngirumpatse na Makamu wake, Edouard Karemera.Walitiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita. Walipatikana na hatia hususa ni kwa sababu ya nafasi yao kama viongozi wa juu wa chama hicho kwa kushindwa kuwazuia wala kuwaadhibu wanamgambo wa chama chao maarufu kama Interahamwe waliokuwa wanashiriki katika mauaji ya kimbari.

Hukumu za Mahakama ya Rufaa

Luteni Kanali Muvunyi kuendelea kutumikia miaka 15 jela: Aprili 1, 2011, Mahakama ya Rufaa ya Mahakama ya ICTR, ilithibitisha adhabu ya kifungo cha miaka 15 jela aliyopewa afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda Luteni Kanali Tharcisse Muvunyi. Afisa huyo aliyekuwa katika Chuo cha Maafisa wa Jeshi Wasiokuwa na Kamisheni (ESO) alitiwa hatiani kwa uchochezi wa mauaji ya kimbari katika hotuba yake aliyoitoa Kusini mwa Rwanda wakati wa mauaji ya kimbari mwaka 1994.

Luteni Kanali Setako kuendelea kutumikia miaka 25 jela: Septemba 28, 2011 Mahakama ya Rufaa pia ilithitisha adhabu ya kifungo cha miaka 25 jela aliyopewa aliyekuwa afisa wa zamani wa jeshi la Rwanda, Luteni Kanali Ephrem Setako baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari, uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.

Maafisa wawili waandamizi wa zamani wa jeshi wanusurika vifungo vya maisha: Desemba 14, 2011, Mahakama ya Rufaa ilipunguza hadi miaka 35 jela adhabu ya kifungo cha maisha aliyopewa mtu anayesadikiwa kuwa alikuwa mpangaji mkuu wa mauaji ya kimbari ya Rwanda Kanali Theoneste Bagosora baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya kimbari,uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.Katika mahakama hiyo pia tarehe hiyohiyo ilimpunguzia afisa mwingine adhabu kama hiyo ya kifungo cha maisha jela hadi miaka 15, afisa mwingine wa jeshi, Luteni Kanali Anatole Nsengiyumva. Kwa kuzingatia muda aliokwishatumikia akiwa kizuizini tangu atiwe mbaroni, mahakama iliamuru kuachiwa huru mara moja.

Kesi ya mtuhumiwa wa ICTR kusikilizwa Rwanda kwa mara ya kwanza: Desemba 16, 2011, Mahakama ya Rufaa ilitoa uamuzi wa kihistoria kwa kuruhusu kesi ya mchungaji Jean Uwikinkindi kwenda kusikilizwa nchini Rwanda.Mahakama mapema ilitupilia mbali rufaa ya mtuhumiwa huyo kupinga uamuzi wa mahakama ya awali ulioamuru kesi hiyo kwenda kusikilizwa nchini Rwanda Juni 28, 2011. Umuazi huo unafungua njia kwa kesi nyingine za watuhumiwa wa ICTR kupelekwa kusikilizwa nchini Rwanda.

Matukio mengine muhimu ICTR

Uchaguzi wa Rais na Makamu wake ICTR: Jaji mwanamke, raia wa Pakistani, Khalida Rachid Khan alichanguliwa kuwa Rais wa ICTR,kuanzia Mei 27, 2011 kwa kipindi cha miaka miwili. Jaji Khan ambaye alikuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama namba III alikuwa Makamu wa Rais wa ICTR tangu Mei 29, 2007. Wakati hohuo, Rais huyo alitangaza Agosti 24, 2011 kwamba Jaji Vagn Joenson kutoka Denmark aliteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa ICTR. Jaji huyo alianza rasmi kazi hiyo Agosti 26, 2011.

Kuachiwa mapema mfungwa wa mauaji ya kimbari: Mfungwa wa mauaji ya kimbari, Michel Bagaragaza, aliachiwa toka gerezani nchini Sweden alikokuwa anatumikia adhabu ya kifungo cha miaka nane jela baada ya kutumikia tayari theluthi mbili ya adhabu hiyo iliyotolewa na ICTR kwa kula njama za kufanya mauaji ya kimbari.Hii ni mara ya kwanza kwa Mahakama hiyo ya Umoja wa Mtaifa kuruhusu mmoja wa wafungwa wake kutoka jela kabla ya muda wa adhabu uliotolewa kumalizika. Bagaragaza alikuwa Mkuu wa Mamlaka ya Chai nchini Rwanda.

Wito kwa mataifa kupokea wanaoachiwa huru ICTR: Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limezitaka nchi wanachama wa umoja huo kuwapokea watuhumiwa wanaoachiwa huru na Mahakama ya Kimataifa ya Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (ICTR) na kuendelea kubaki chini ya uangalizi wa mahakama hiyo. Wapo watuhumiwa watano waliokwishaachiwa huru lakini bado wanatafuta nchi za kuwapokea.

TFF YATOA RAMBIRAMBI MSIBA WA MCHEZAJI WA ZAMANI WA TAIFA STARS RASHID MOYO!!!

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 29, 2011

RAMBIRAMBI MSIBA WA RASHID MOYO

Shrikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa, Rashid Moyo kilichotokea usiku wa Desemba 25 mwaka huu kwao Msambweni, Tanga.

Moyo ambaye aliichezea timu ya Taifa kwenye miaka ya 70 alizikwa Desemba 26 mwaka huu kwenye makaburi ya Mabawa mkoani Tanga. Pia alikuwa mchezaji wa timu ya Coastal Union ya mkoa wa Tanga.

Msiba huo ni pigo kwa familia ya Moyo, TFF na familia ya mpira wa miguu kwa ujumla nchini kutokana na mchango alioutoa kwa Tanzania hasa wakati akiwa mchezaji.

TFF inatoa pole kwa familia ya marehemu Moyo, Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Tanga (TRFA) na kuwataka kuwa na uvumilivu katika kipindi hiki cha msiba huo mzito. Pia TFF itatoa ubani wa sh. 100,000 kwa familia ya marehemu kama rambirambi zake.

Mungu aiweke roho ya marehemu Rashid Moyo mahali pema peponi. Amina

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

MTANGAZAJI WA TBC HALIMA MCHUKA AFARIKI DUNIA!!


Mtangazaji Mahiri wa Mpira katika Eneo la Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na Mwanamke wa Kwanza Halima Mchuka amefariki Dunia akiwa anahudumu katika Redio Tanzania Dar es Salaam RTD na baadae Shirika la Utangazaji Tanzania (SHIUTA) amefariki Dunia.

Mchuka amefariki usiku wa kumkia leo kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi kwa muda ambapo kwa sasa inaelezwa alikuwa anaanza kupata nafuu baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Mtangazaji Halima Mchuka alijiunga na Radio Tanzania Dar es Salaam mwaka 1994 ambapo alifanya kazi katika Idara ya Habari na Idara ya mipango.

Mungu ailaze Roho ya BI Halima Mchuka pahala pema peponi Amina

Wednesday, December 28, 2011

KIONGOZI WA KOREA KASKAZINI KIM JONG IL AZIKWA!!


Kiongozi wa zamani wa Korea Kaskazini Kim Jong Il amezikwa leo kwenye mazishi ambayo yameongozwa na mwanaye Kim Jong Un huku kukiwa hakuna kiongozi yoyote kutoka mataifa mengine ambaye amehudhuria maziko hayo!! Maelfu ya wananchi wa Korea Kaskazini wameshiriki kwenye shughuli hizo huku weni wao wakiomboleza kwa kilio!!

Tuesday, December 27, 2011

ARSENAL YABANWA MBAVU EMIRATES NA KUAMBULIA SARE!!



Klabu ya Arsenal maarufu kama Washika Magobole waJiji la London wamebanwa mbavu katika mchezo wa Ligi Kuu Nchini England baada ya kuambulia sare ya bao 1-1 mbele ya Wolves!! Kutokana na matokeo hayo Klabu ya Arsenal imeendelea kujiweka mbali na mbio za Ubingwa msimu huu!!

JONNY EVANS KUKAA NJE KWA MAJUMA MAWILI!!


Kocha Mkuu wa Manachester United Sir Alex Ferguson amesema watamkosa Beki wao wa kati Jonny Evans kwa majuma mawili hadi matatu na hivyo kumfanya kuwa na majeruhi kumi na moja wa kikosi chake!! Evans aliumia kwenye mchezo dhidi ya Wigan Athletic uliopigwa hiyo jana!! Wachezaji wengine ambao ni majeruhi kwa sasa ni Nemanja Vidic, Darren Fletcher, Rio Ferdinand, Michael Owen, Anderson, Tom Cleverley, Fabio Da Silva, Phil Jones, Ashley Young na Chris Smalling!!

TAHADHARI YA KUIBUKA KWA MAFURIKO TENA KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM!!

Monday, December 26, 2011

MAN UTD YASHINDA HUKU LIVERPOOL, CHELSEA NA MAN CITY ZIKIBANWA MBAVU!!






Ligi Kuu nchini Uingereza imeendelea na kushuhudia Manchester United ikifanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 5-0 na kuikaribia Manchester City kilele baada ya timu hiyo kulazimishwa sare ya bila kufungana na Wes Bromwich Albion!! Chelsea walikwenda sare ya goli 1-1 mbele ya Fulham wakati Liverpool walibanwa mbavu na Blackburn Rovers baada ya kutoka sare ya goli 1-1!!

Wednesday, December 21, 2011

MANCHESTER UNITED NA CITY WAKABANA KOO LIGI KUU NCHINI UINGEREZA!!





Manchester Unite imevuna ushidni wa magoli 5-0 mbele ya Fulham wakati Manchester City wakiisambaratisha Stoke City kwa magoli 3-0!! Arsenal nayo iliendelea kuvuna ushindi baada ya kuifunga Aston Villa kwa magoli 2-1!! Newcastle United imeendelea na wakati mgumu baada ya kufunga magoli 3-2 na West Bromwich Albion!! Everton ilishinda kwa goli 1-0 mbele ya Swansea huku Wigan wakitoka sare tasa na Liverpool huku QPR wakipata kichapo cha nyumbani mbele ya Sunderland!!

RAIS KIKWETE ATOA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA WALIOFIKWA NA VIFO KUTOKANA NA MAFURIKO DSM!!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Said Meck Sadiq kuomboleza vifo vya watu 13 ambao wamepoteza maisha katika mafuriko makubwa yaliyotokana na mvua ambazo zimekuwa zinanyesha tokea Jumanne, Desemba 20, 2011.

Aidha, Rais Kikwete amempa pole Mkuu huyo wa Mkoa kutokana na uharibifu mkubwa wa nyumba, makazi na mali nyingine za wananchi uliosababishwa na mvua hizo ambazo pia zimesababisha uharibifu wa miundombinu.

Rais Kikwete pia ameuelekeza uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa kusaidiana na taasisi na vyombo vyenye uzoefu wa maafa kushirikiana katika kuendelea kuokoa maisha ya watu, kusaidia waliozingirwa na mafuriko na kuwahifadhi na kuwasaidia wale wote waliopoteza nyumba na makazi kutokana na mafuriko hayo.

Katika salamu zake, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Sadiq: “Nimepokea kwa masikitiko habari za vifo vya wenzetu 13 vilivyotokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa ambayo sote tumeishuhudia katika Mkoa wa Dar es Salaam tokea jana. Nakutumia wewe rambirambi zangu kutokana na vifo hivyo, na kupitia kwako kwa familia, ndugu na jamaa waliopoteza wapendwa wao katika balaa hili la mafuriko. Wajulishe kuwa msiba wao ni msiba wangu, naelewa machungu yao na niko nao katika hali ya sasa ya maombolezo. Mungu aziweke pema peponi roho za marehemu wote.”

Ameongeza Rais Kikwete: “Napenda pia kupitia kwako kutoa pole zangu nyingi kwa wote walioumia ama kupoteza mali zao katika mafuriko haya. Wajulishe kuwa moyo wangu uko nao wakati huu wa mazingira magumu.”

“Chini ya usimamizi wako, ningependa kuona uongozi wa Mkoa kwa kushirikiana na taasisi na vyombo vyenye ujuzi na uzoefu wa kupambana na majanga na dharura za namna hii, kuhakikisha kuwa tunaendelea kuokoa watu ambao bado wamezingirwa na mafuriko, tunawapa matibabu wale walioumia katika mafuriko hayo, na tunawahifadhi na kuwapa huduma za kibinadamu wote waliopoteza nyumba na makazi yao katika mafurikio hayo.”

WATU 13 WAPOTEZA MAISHA JIJINI DAR ES SALAAM KUTOKANA NA MVUA!!



Boti zikitumika kuwaokoa wananchi ambao walikumbwa na mafuriko katika Jiji la Dar Es Salaam. Boti hiyo ilitumika kuwaokoa wakazi wa Jangwani na hata Kigogo ambao walikuwa wamechukuliwa na mafuriko hayo. Mamia ya wananchi hawana makazi kutokana na mvua hizo zilizochangia kuzuka kwa mafuriko huku watu 13 wakipoteza maisha na uharibifu mwingine wa miundombinu ukishuhudiwa!!

MAFURIKO YAENDELEA KUTESA WAKAZI WA DAR ES SALAAM KWA SIKU YA PILI SASA!!





Hali ilivyo katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam baada ya mvua kali ikiambatana na radi kuendelea kutikisa Jiji hilo. Mvua hiyo imenyesha kwa saa zaidi ya nne sasa huku mawasiliano ya barabara yakikatizwa na kuchangia watu kushindwa kufika maeneo wanayokwenda!! Jeshi la Polisi nalo linaendelea na zoez la uokozi kwa wale ambao wamekwama kwenye maeneo ya mabondeni!!

Monday, December 19, 2011

RAIS KIKWETE AWAAPISHA MABALOZI WAPYA IKULU LEO!!


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewaapisha Mabalozi wapya ambao amewateua kwenda kuiwakilisha nchi kwenye mataifa ya ughaibuni. Miongoni wa walioapishwa ni pamoja na Philip Marmo ambaye anakwenda nchini China, Daktari Batlida Salha Burian ambaye anakwenda nchini Kenya. Dokta Deodorus Kamala yeye anachukua nafasi ya kuwa Balozi nchini Ubelgiji. naye Dokta Ladislaus Komba anakwenda kuhudumu nchini Uganda. Mabalozi wengine ni pamoja na Bi Shamim Nyanguga ambaye amepelekwa nchini Msumbiji, Bi Grace J.E. Mujuma ambaye anakwenda nchini Zambia, Mohamed Hamza ambaye anakwenda kuiwakilisha nchi huko Misri na Ali Saleh ambaye amepelekwa Omani.

MBUNGE WA KIGOMA KUSINI DAVID KAFULILA AVULIWA UANACHAMA NCCR-MAGEUZI!!


Halmashauri Kuu ya Chama Cha NCCR-Mageuzi imemtimua uanachama Mbunge wa Kigoma Kusini David Kafulila kwa madai ya kutaka kukiharibu chama hicho huku wanachama wengine sita wakiingia kwenye mkumbo huo.

Mgombea wa Urais kwenye uchaguzi uliopita Hashim Rungwe ni miongoni mwa waliotimuliwa kwa kosa linalofanana na Kafulila wakitajwa kutaka kukivuruga Chama.

Wanachama hao wanasiku kumi na nne za kukataa rufaa kupinga adhabu ambayo imetolewa na iwapo watashindwa kwenye rufaa yao ni wazi Kafulila atakuwa amepoteza uhalali wa kuwa Mbunge na hivyo Tume ya Taifa ya Uchaguzi kulazimika kuitisha Uchaguzi Mdogo.

MAN CITY YAREJEA KILELENI WAKATI MAN UTD IKISHINDA DHIDI YA QPR!!




Klabu ya Manchester City imefanikiwa kurudi kileleni mwa Ligi Kuu Nchini Uingereza baada ya kuifunga Arsenal kwa goli moja kwa nunge!! Goli la David Silva ndiyo lilipeleka kilio kwa Washika Bunduki wa Jiji la London!! Manchester United ilifanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-0 mbele ya Queens Park Rangers!!

BARCELONA YATWAA UBINGWA WA KLABU BINGWA DUNIANI!!


Klabu ya FC Barcelona imefanikiwa kutetea Ubingwa wake wa Klabu Bingwa ya Dunia baada ya kuifunga Santos kwa magoli 4-0!! Katika mchezo wa fainal uliopigwa nchini Japan katika Jiji la Yokohama ulishuhudia Lionel Messi akifanikiwa kufunga magoli mawili huku mengine yakifungwa na Xavi Hanandez na Cesc Fabregas!!

KIONGOZI WA KOREA KASKAZINI KIM JONG IL AFARIKI DUNIA!!


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Il amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 69 baada kuugua ugonjwa wa moyo. Kiongozi huyo ambaye aliingia madarakani mwaka 1994 baada ya kifo cha Baba yake Kim Jong Sung. Nafasi yake itachukuliwa na mwanae Kim Jong Un!! Mazishi yake yatafanyika tarehe 28 December 2011!!