Friday, December 31, 2010

HAPPY NEW YEAR TO ALL!!


Nawatakia Heri ya Mwaka Mpya wadau wote wa Blogu hii na nawashukuru kwa kile ambacho imekifanya na kuchangia Blogu hii kufika hapa!! Kumbuka tarehe Moja ya kila mwezi January Nurdin Selemani mmiliki wa Blogu huu huwa anazaliwa!!

Thursday, December 30, 2010

LIVERPOOL KIMEO, CHELSEA IKIFUFUKA, ARSENAL NGUVU YA SODA!!







Waswahili husema mwaka wa hasara ni hasara tu hata ufanyaje na ng'ombe wa maskini hazai!! Klabu ya Liverpool imeendelea kudhihirisha hili baada ya kupata kichapo cha nyumbani kutoka kwa Wolverhampton kwa goli moja kwa nunge!! Matokeo ya michezo mingine ni kama inavyoonekana:
Chelsea 1-0 Bolton
Liverpool 0-1 Wolverhampton
Wigan 2-2 Arsenal

Monday, December 27, 2010

ANCELOTTI AKALIA KUTI KAVU CHELSEA!!



Kocha Mkuu wa Chelsea Carlo Ancelotti amekalia kuti kavu baada ya timu yake kupata kichapo cha magoli 3-1 kutoka kwa Arsenal!! Licha ya dalili kuonesha kibarua chake kipo mashakani kutokana na kutoshinda michezo sita mwenyewe amesisitiza ataendelea kuwepo na sasa anataka kusajili zaidi January!!

CHELSEA KIMEO KWA ARSENAL!!





Washika Magobole wa Jiji la London Arsenal wamefanikiwa kumaliza uteja mbele ya Chelsea baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-1!! Magoli ya Ale Song, Cecs Fabregas na Theo Walcott ndiyo yaliyomaliza uteja wa Arsenal!!

Sunday, December 26, 2010

LIGI KUU ENGLAND YAENDELEA KUCHANJA MBUGA KWA KASI!!








Ligi Kuu nchini England maarufu kama Barclays Premium League imeendelea siku ya Boxing Day na kushuhudia Manchester United ikiendelea kujichimia kileleni mwa Ligi. Matokeo yote yalikuwa hivi:
Aston Villa 1-2 Tottenham
Blackburn 0-2 Stoke
Bolton 2-0 West Brom
Fulham 1-3 West Ham
Man Utd 2-0 Sunderland
Newcastle 1-3 Man City
Wolverhampton 1-2 Wigan

Monday, December 20, 2010

GOLIKIPA BORA KWA UPANDE WANGU!!


Anaitwa Muteba Kidiaba Golikipa wa Klabu ya TP Mazembe ambaye style yake ya ushangiliaji imemzolea umaarufu mkubwa!! Lakini pia ni golikipa anayejua wajibu wake pindi anapokuwa golini kutetea Klabu na hata Timu yake ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC!!

TP MAZEMBE NA HISTORIA KWENYE SOKA!!


Klabu ya TP Mzembe hatimaye imeweza kuandika historia na kuudhihirishia ulimwengu kuwa hata Klabu za Bara la Afrika zinaweza kusakata soka la uhakika!! TP Mazembe ambao walishindwa kutwaa ubingwa wa Klabu Bingwa ya Dunia mbele ya Inter Milan watakumbukwa daima kwa kile ambacho wamekifanya!! Hii inawadhihirishia wale ambao walikuwa wanahoji jinsi ambavyo walitwaa Ubingwa wa Klabu Bingwa Barani Afrika!!

NAWEKA KUMBUKUMBU SAWA!!


Kwa kweli wanazi wa kabumbu wanasubiri kwa hamu mwezi February ufike ili washuhudie kile ambacho wenyewe wanakiita fainali ya mapema kati ya Barcelona na Arsenal!! Ngoja tusubiri ili tujue mambo yatakuwaje kwa kweli!!

CUF WAMSHUKIA MZEE MWINYI SAKATA LA KATIBA MPYA!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeshitushwa na kauli aliyoitoa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wa awamu ya nne Mhe. Ali Hassan Mwinyi wiki iliyopita ya kutoona sababu ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa sasa.

Kwa mujibu wa vyombo vya Habari alidai kuwa haungi mkono wazo la kufanya mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa sasa, hii ni kwa maslahi ya nani?

CUF – Chama Cha Wananchi tunasisitiza tumeshitushwa na kauli hii iliyotolewa na mtu ambaye anaheshima kubwa katika nchi hii, tunaingia shaka kwamba hakubaliani na mabadiliko hayo kufanyika sasa hivi kwa sababu hana maslahi nayo hadi hapo dhamira yake ya matumizi ya Katiba hiyo itakapokamilika hasa ukizingatia miongoni mwa wanafamilia yake wana fursa kubwa ya kuwania urais katika nchi hii.

CUF – hatuanimi kuwa mapungufu yaliyomo katika Katiba hiyo yeye hayatambui, ila inatudhihirishia wazi kuwa kuna uwezekano mkubwa yeye akiwa Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi kuitumia au hata kushauri vifungu vyenye utata vya katiba hiyo, kutumika kwa maslahi ya CCM.

CUF – Tunahimiza mabadiliko ya katiba ni lazima, iwapo kama tunataka demokrasia ya kweli, hatuwezi kuwa na katiba yenye Tume isiyokuwa huru ambayo Rais aliyeiteua anaweza kuivunja wakati wowote hata kwa sababu nyingine yeyote au kwa sababu ya tabia mbaya lakini wakati huo huo chombo cha kisheria kama mahakama hakina uwezo wa kuchunguza lolote lililotendwa na tume hiyo ya uchaguzi (ibara ya 74).

CUF – Tunaendelea kuwasihi, watanzania wote waumini wa dini zote, vyama vyote vya siasa, Taasisi zote nchini, asasi za kiraia, wanaharakati wa aina zote, kuungana kwa pamoja kudai mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayokidhi mahitaji ya watanzania wote.

Wednesday, December 1, 2010

MAN UTD YAANGUKIA PUA, ARSENAL IKIUA CARLING CUP!!




Manchester United imekumbana na shubiri baada ya kupata kichapo cha kwanza msimu huu cha magoli manne kwa nunge wakati Arsenal wakitinga Nusu Faila ya Carling Cup kwa kuichabanga Wigan Athletics kwa magoli mawili kwa buyu!!

KIKWETE KUHUDHURIA MKUTANO WA EAST AFRICA!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kwenda Mkoani Arusha leo mchana, kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha kawaida cha Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kinachoanza kesho tarehe 2 Disemba.

Rais Kikwete anamaliza kipindi chake cha mwaka mmoja cha kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kumkabidhi uenyekiti kiongozi mwingine katika kikao hicho kama ilivyo katika taratibu za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Rais Kikwete alipokea uenyekiti kutoka kwa Rais Paul Kagame katika kikao cha Novemba mwaka jana , 2009.

Katika kikao cha wiki hii viongozi watapokea taarifa mbalimbali za Baraza la Mawaziri zinazohusu utekelezaji wa masuala yanayohusu Jumuiya na kujadili mambo mbalimbali.

Mapema leo asubuhi katika Ikulu ya Dar-Es-Salaam, Rais Kikwete amempokea Kijana wa Kitanzania Musa Lunyeka Dotto , mkazi wa kijiji cha Chabulongo, kata ya Kasamwa Wilaya ya Geita aliyeweka azma ya kusafiri kwa baiskeli kutoka Geita hadi Dar-Es-Salaam, kuja kumpongeza Rais Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuiongoza nchi.

Hata hivyo, Musa alipofika Singida Katibu wa Vijana wa CCM, mkoani humo alimshauri apande basi hadi Dar-es-salaam, na ndipo alipofika na leo kutimiza azma yake ya kumsalimia na kumpongeza Rais Kikwete.

Rais Kikwete amemshukuru kijana huyo kwa moyo wake huo na kuahidi kumsaidia zaidi katika shughuli zake za kilimo ili apate manufaa na mafanikio zaidi.

Tuesday, November 30, 2010

KIKWETE AKETI KIKAO CHA KWANZA NA BARAZA LA MAWAZIRI!!

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete, Jumatatu, Novemba 29, 2010, amekutana rasmi kwa mara ya kwanza na Baraza la Mawaziri lake jipya pamoja na Naibu Mawaziri na kuwapa maelekezo ya awali ya nini anakitarajia kutoka kwa wateule wake hao.

Mawaziri wote 29 na Naibu Mawaziri wote 21 ambao Rais Kikwete aliwaapisha rasmi kushika nyadhifa zao katika sherehe iliyofanyika Jumamosi iliyopita, Novemba 27, 2010, wamehudhuria mkutano huo kwenye Chumba cha Baraza la Mawaziri, Ikulu, Dar es Salaam.

Katika mkutano huo uliochukua kiasi cha saa tatu, Rais alianza kwa kuwaeleza mawaziri kuwa katika kipindi hiki cha pili cha uongozi wake hakutakuwepo na muda wa kupoteza, na wala hatakuwa tayari kukubali maelezo ya kwa nini utekelezaji wa majukumu ya msingi umeshindikana.

Kwa mara nyingine amewapongeza Mawaziri na Naibu Mawaziri hao akisisitiza: “Mnastahili pongezi hasa ukizingatia ukweli kwamba nyinyi mmebahatika kuteuliwa kutoka kwenye orodha ndefu ya wabunge wengi wenye sifa za kushika nafasi mlizo nazo. Nimewateua kwa imani kuwa pamoja nanyi, tutatimiza matumaini ya wananchi wa Tanzania waliokichagua Chama cha Mapinduzi kiendelee kuongoza nchi yetu.”

Ameongeza: “Ni imani yangu kuwa kwa mshikamano na ushirikiano wetu kama timu moja ya ushindi, tutatekeleza majukumu yote kwa uadilifu, uaminifu na ufanisi wa hali ya juu. Ufanisi wa Waziri ama Naibu Waziri katika utekelezaji wa majukumu yake unategemea sana ufahamu na uelewa wake wa masuala muhimu yanayohusu Nchi, Serikali na Wizara anayoiongoza.”

Katika mkutano huo ambao ameuelezea kama wa Utangulizi wakati inaandaliwa Semina Elekezi, Rais Kikwete amewaelezea wateule wake maana ya Baraza la Mawaziri na majukumu yake, na kutaka kila Waziri ahakikishe anatayarisha kalenda yake ya masuala muhimu ambayo anataka yajadiliwe na Baraza la Mawaziri kwa mwaka.

Rais Kikwete pia amewaeleza wateule wake kuhusu wajibu wa Mawaziri katika Bunge akisisitiza kuwa ni wajibu wa kila waziri kuhudhuria vikao vyote vya Bunge, na kuwa ndani ya Bunge mawaziri wote wa Serikali lazima wawajibike kwa pamoja.

“Ni muhimu ieleweke kuwa kama ilivyo kwa maamuzi ya Baraza la Mawaziri, uwajibikaji wa Mawaziri Bungeni ni wa Pamoja. Kwa hiyo, Hoja ya Serikali Bungeni ni Hoja ya Mawaziri Wote na siyo Waziri anayewasilisha hoja tu,” amesema Rais Kikwete.

Rais pia amewakumbusha wateule wake kuhusu uwajibikaji wa pamoja (collective responsibility) katika kuongoza nchi, akisisitiza kuwa uwajibikaji huo unaelezwa kwa ufasaha katika Hati Maalum (Instrument) ya Majukumu ya kila Wizara.

Kuhusu uhusiano kati ya Waziri na Rais, na kati ya Waziri na Waziri Mkuu, Rais amesema kuwa pamoja na kwamba shughuli zote za utendaji Serikalini hutekelezwa kwa niaba ya Rais, lazima mawaziri wakumbuke kuwa Waziri Mkuu ndiye msimamizi wa shughuli za kila siku za Serikali.

Rais Kikwete pia ametaka kujengeka mahusiano mazuri kati ya Waziri na Naibu Waziri wake akisisitiza: “Jambo la msingi la kuzingatia ni kwamba uhusiano mzuri baina ya viongozi hawa ni nguzo muhimu katika mafanikio ya Wizara. Kwa hiyo, ili kuepuka migongano katika utekelezaji ni muhimu mipaka ya kazi za Waziri na Naibu Waziri ikaheshimika na pia ni wajibu wa Waziri kumpangia kazi Naibu Waziri katika Wizara husika.

Katika mkutano huo, Rais Kikwete pia amezungumzia uhusiano kati ya Waziri na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Waziri wa Nchi Asiyekuwa na Portfolio na Katibu Mkuu; uhusiano kati ya Naibu Waziri na Katibu Mkuu, na uhusiano kati ya Waziri na Waziri wa Sekta Nyingine.

Rais Kikwete pia amefafanua kuhusu uhusiano kati ya Wizara na Wadau Wengine; uhusiano baina ya Wizara, Mikoa na Halmashauri; uhusiano na Taasisi Zilizo Chini ya Wizara; uhusiano na Wasaidizi wa Mawaziri pamoja na utekelezaji wa Maagizo ya Viongozi wa Kitaifa.
Rais Kikwete pia amewaeleza Mawaziri na Naibu Mawaziri kuhusu nyaraka muhimu ambazo wanapaswa kukabidhiwa na kuzipitia watakapofika kwenye nafasi zao mpya za kazi. Nyaraka hizo ni pamoja na Taarifa ya Makabidhiano ya Ofisi, Katiba, Ilani ya Chama Tawala, Dira ya Taifa, na Mpango wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umasikini (MKUKUTA).

Aidha, Rais Kikwete amewaeleza wateule wake kuhusu umuhimu wao kufahamu Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu, Mikakati, Mipangomkakati, Mpango na Bajeti ya Wizara, Mpango wa Kazi wa Wizara na Masharti ya Kazi ya Waziri.

Rais Kikwete vile vile amekumbusha Mawaziri na Naibu Mawaziri wake kuwa suala la vita dhidi ya rushwa ni suala la kikatiba na kuwataka kuhakikisha kuwa Mpango wa Pili wa Mkakati wa Kitaifa wa Kupambana na Rushwa (NACSAP-11) unatekelezwa.

Pia amewataka Mawaziri kusimamia mapato ya Serikali yasiyotokana na kodi na kudhibiti matumizi ya Serikali.
Rais Kikwete pia amewataka viongozi hao kuzingatia maadili ya uongozi ikiwa ni pamoja na kusimamia sheria za nchi, kuheshimu sheria katika shughuli na mambo yao binafsi na pia kutunza siri za Serikali kwa mujibu wa kiapo chao.

Rais Kikwete pia amesisitiza umuhimu wa Mawaziri na Naibu Mawaziri kuwasiliana na wananchi kwa maana ya kueleza mafanikio ya Serikali na mipango ya Serikali katika kushughulikia matatizo ya wananchi.

Amewataka kuvitumia kikamilifu Vitengo vya Mawasiliano ya Serikali katika wizara zao ambavyo ndivyo vyenye jukumu la kutoa taarifa kuhusu Wizara inavyotelekeza majukumu yake.

“Uzoefu unaonyesha kuwa Mawaziri wengi ni wazito kufanya mawasiliano na wananchi hata pale ambako Wizara imefanya mambo mengi mazuri. Hivyo, Mawaziri muwe mstari wa mbele kuelezea mafanikio ya utendaji wa Serikali katika Wizara zetu,” ameelekeza Rais Kikwete na kuongeza:

“Lazima ujengwe utamaduni wa kudumu wa kuwasiliana na wananchi wote ambao ndio waajiri wetu kupitia kura zao. Mawaziri wote tumieni Vitengo vyenu vya Mawasiliano na vyombo vya habari kwa ustadi ipasavyo,” amefafanua Rais Kikwete.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

BARCELONA YAISHUSHIA MAAFA REAL MADRID!!







Barcelona hatimaye wamekaa kileleni mwa Ligi Kuu nchini Spain maarufu kama La Liga baada ya kuvuna ushindi wa magoli matano kwa nunge dhidi ya wapinzani wao Real Madrid!!

Monday, October 11, 2010

MATOKEO YA SYNOVATE YASHUKIWA!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumesikitishwa na taarifa ya utafiti wa taasisi ya Synovate iliyotolewa jana Oktoba 10, jijini Dar es Salaam na kuripotiwa na vyombo vya habari leo hii namna inavyojichanganya, kwani idadi ya wanaomkubali Mgombea Urais wa Chama cha Mapinduzi Jakaya Kikwete ni wengi kuliko vyama vingine, wakati huo huo wanaokiri kutoridhishwa na huduma zake ni wengi.

Kwa mujibu wa vyombo vya Habari, ripoti hiyo inaonyesha Dkt. Jakaya Kikwete anakubalika kwa asilimia 61, Dkt. Willbrod Slaa ana asilimia 16 na Prof. Ibrahim Lipumba ana asilimia 5, lakini wakati huo huo inaeleza ripoti hiyo kuwa katika utendaji wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete watu wengi waliohojiwa hawakuridhika na huduma zinazotolewa katika upatikanaji wa ajira (84%), bei za vyakula (72%), maji safi ya kunywa (49%), afya(48%), mapambano dhidi ya rushwa(61%) na mapambano dhidi ya kuondoa umasikini(86%).

Katika ripoti hiyo hiyo, pamoja na kuonyesha wananchi wasivyoridhishwa na utendaji wa serikali hiyo ya Jakaya Kikwete, lakini bado wana imani na Rais Kikwete kwa asilimia 84, Baraza la Mawaziri (68%), Jeshi la Polisi (45%), Baraza la Mitihani (50%), mahakama (52), taasisi za huduma za afya (50%), TAKUKURU (46%) na vyama vya upinzani (48%).

Kwa upande wa elimu ya msingi ripoti inaonyesha kuwa wanaoridhika na utolewaji bora wa elimu ni asilimia 82, na kwa elimu ya sekondari wanaoridhika na utolewaji wa elimu bora ni asilimia 77.

CUF – Chama cha Wananchi tunasema iwapo kama ni kweli taarifa iliyoripotiwa ndivyo ilivyo tunasikitishwa namna taaluma ya utafiti inavyotumika vibaya, kwani hayamkiniki mtu mwenye akili timamu hata kama hakwenda shule, hata awe mtoto wako nyumbani, wakati akijua fika, tena kwa uhakika kwamba wewe umeshindwa kumpatia huduma muhimu (kama ripoti inavyoonyesha) na akawa bado eti ana imani na wewe na watendaji wako, huu ni uzushi mtupu.

CUF – Chama cha Wananchi tunaitaka taasisi ya Syonovate iwaombe radhi watanzania, kwani ripoti yao inaonyesha kuwa, wananchi wa nchi hii bado ni mbumbumbu wa kumpenda mtu kwa sura yake na wakaendelea kuwa na imani nae hata kama wanatambua fika ameshindwa kuwapatia huduma muhimu, huku ni kuwadhalilisha Watanzania na kazi kubwa inayofanywa na vyama vya upinzani, taasisi zisizo za kiserikali na vyombo vya habari juu ya kuelimisha umma.

CUF – Tunawatahadharisha Watanzania kuwa makini katika kipindi hiki cha uchaguzi, kwani taasisi mamluki zitatumia taaluma zao kuwapotosha na kuwavunja moyo mliokuwa nao wakukataa ufisadi na dhuluma inayofanywa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi dhidi ya mali asili na mapato ya nchi, ili siku ya uchaguzi Oktoba 31, wananchi msijitokeze kwa wingi kwa kudhani kuwa CCM bado inakubalika, TUNAWASIHI WANANCHI WA TANZANIA WALIOJIANDIKISHA KUPIGA KURA, JITOKEZENI KWA WINGI SIKU YA KUPIGA KURA NA MFANYE MAAMUZI SAHIHI YA KULETA MABADILIKO.

Saturday, September 18, 2010

MHANGA WA UBUNGE AUKWAA UKUU WA WILAYA!!!


Kada wa Chama Cha Mapinduzi CCM Nape Moses Nnauye ameteuliwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuwa Mkuu wa Wilaya ya Masasi. Hii inaweza kuwa njia moja wapo ya kumfuta "JASHO" baada ya kushindwa kupata nafasi ya kuwa mgombea Ubunge katika Jimbo la Ubungo!!!

Thursday, September 16, 2010

TAKUKURU YATAKIWA KUUNGWA MKONO KWENYE SHUGHULI ZAKE!!!

Katibu Mkuu Ikulu, Bwana Michael Mwanda amewahimiza wananchi wa Mkoa wa Lindi, viongozi, Asasi Zisizo za Kiserikali pamoja na viongozi wa madhehebu ya dini mkoani humo, kuunga mkono jitihada zinazofanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kwa vile jukumu la kupambana na rushwa ni la Watanzania wote.

“Jukumu la kupambana na rushwa ni letu sote na ndiyo maana kwa kutambua hilo, nipo hapa leo kuwaunga mkono katika mapambano dhidi ya rushwa. Napenda nitumie nafasi hii pia kuwahamasisha wananchi wote wa Mkoa wa Lindi pamoja na viongozi wenzangu kuwaunga mkono TAKUKURU katika mapambano haya mazito”, amesema.

Bwana Mwanda amebainisha hayo mjini Lindi 16 Septemba, 2010 akiwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa jengo la ofisi za TAKUKURU mkoani humo, iliyohudhuriwa pia na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Asasi Zisizo za Kiserikali.

Katika hotuba yake, Bwana Mwanda amesema hatua ya TAKUKURU kujenga jengo la ofisi katika Mkoa wa Lindi, inatokana na dhamira thabiti ya Serikali ya Awamu ya Nne katika kuimarisha utawala bora na kuboresha utendaji wa kazi wa taasisi hiyo, kwa vile siku zote lengo la Serikali ni kupeleka huduma karibu na wananchi.

“…lengo la Serikali yetu siku zote limekuwa ni kupeleka huduma karibu na wananchi ili waweze kufanya shughuli zao za kimaendeleo kwa ufanisi na kuhakikisha kwamba kero ya rushwa inadhibitiwa vilivyo katika kila kona ya nchi yetu”, amebainisha Bwana Mwanda.

Amesema vita ya kuzuia na kupambana na rushwa ni kubwa inayohitaji umakini, moyo wa kujitolea na kujituma, na wakati mwingine kukubali lawama, hivyo Serikali imeona umuhimu wa kuboresha mazingira ya kazi ya watumishi wa TAKUKURU ili waweze kutoa huduma zilizo bora zaidi.

Bwana Mwanda amewatanabaisha viongozi wa madhehebu ya dini kuendelea kuwaelimisha waumini wao na hasa vijana kuhusu ubaya wa rushwa, na amewashauri kutumia nafasi waliyo nayo kutoa elimu ya maadili mema kwa waumini ili waepukane na maovu, hivyo kusaidia kwa kiwango kikubwa kujenga jamii adilifu na inayochukia vitendo vya rushwa.

Katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani Oktoba 31, 2010, Bwana Mwanda amewahimiza wananchi kuzingatia matakwa ya sheria zinazosimamia masuala ya rushwa katika uchaguzi, ili kuhakikisha kuwa uchaguzi huo haugubikwi na vitendo vya rushwa.

Ili kuhakikisha kuwa TAKUKURU inapata mafanikio zaidi, Bwana Mwanda ameitaka Taasisi hiyo kuimarisha Kamati za Uadilifu zilizopo katika Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa, Wilaya na Halmashauri za Wilaya, kuzishirikisha Asasi Zisizo za Kiserikali katika vita dhidi ya rushwa katika ngazi hizo, kuendelea kujenga uwezo wa watumishi wake, na kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu rushwa.

SIMBA YAZOA POINTI TATU WAKATI YANGA IKICHECHEMEA!!!




Ligi Kuu Tanzania Bara imeendelea ambapo Bingwa Mtetezi Simba amefanikiwa kupata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Ruvu Shooting, Wakati Mtibwa wakiwalazimisha sare Yanga ya goli moja kwa moja huku Azam wakipata kichapo cha goli moja kwa nunge kutoka kwa Kagera Sugar!!!

CUF WALAANI KUPIGWA KWA MWANDISHI KWENYE KAMPENI!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumesikitishwa na kitendo cha mwandishi wa gazeti la Mwananchi Fredrick Katulanda, kuvamiwa na kushambuliwa na kikosi cha “janjaweed” wa Chama cha Mapinduzi wanatambulika kama “Green Guard” na kumjeruhi, katika kampeni za Ubunge katika jimbo la Sumve, Kijiji cha Nyambiti.

Walinzi hao walimshambulia mwandishi huyo na kumjeruhi sehemu za puani na mdomoni wakati wakimtaka yeye na wanataaluma wengine wa fani ya uandishi waondoke kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge wa Jimbo hilo la Sumve, wilayani Kwimba.

CUF – Chama cha Wananchi tunalaani, kitendo hicho kuwa siyo cha kiungwana hata kidogo, licha ya kuhatarisha amani ya nchi lakini pia ni ukiukwaji mkubwa wa maadili na haki za binadamu cha kuwapiga waandishi wakiwa kazini.

CUF – Chama cha Wananchi tunatambua kuwa, vitendo hivi vimefanywa na Chama cha Mapinduzi, kutokana na mazoea ya kubebwa kwa kuripotiwa habari zao kwa kupambwa zaidi kuliko uhalisia, hivyo pindi waandishi wanapofuata maadili ya taaluma yao na kuripoti habari kama zilivyo, inakuwa nongwa kwa CCM, na kupanda jazba hatimaye kujichukulia sheria mikononi mwao.

CUF – Tunaviomba vyombo vyote vinavyohusika, kuwachukulia hatua kali Chama cha Mapinduzi, kwa uvunjifu huu wa amani, ukiukwaji wa maadili wakati wa kampeni na kwa vile ni vitendo vya jinai, tunalisihi jeshi la Polisi kuhakikisha wale wote waliohusika wanapatikana na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa Chama hicho.

CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa makini na chama hiki kinachoashiria uvunjivu wa amani iliyoasisiwa na wazee wetu, kwani hata ukiangalia baadhi ya mabango yao ya kampeni yanatoa vitisho kwenu wapiga kura ili msichague chama kingine iwapo kama mnataka amani, hii ina maana kuwa wapo tayari kuvunja amani iliyopo iwapo hawatachaguliwa.

HAKI SAWA KWA WOTE

RAFAEL NADAL AENDELEA KUSHEREHEKEA TAJI LA US OPEN!!!


Mchezaji ambaye anaorodheshwa katika nafasi ya kwanza upande wa wanaume kwa Mchezo wa Tennis na Bingwa wa US Open Rafael Nadal ameendelea kusherehekea ubingwa wake na hapa ilikuwa katika Uwanja wa Sabtiago Bernabeu kabla ya kuchezwa kwa mchezo wa Ligi ya Mabingwa kati ya Real Madrid na Ajax Amsterdam.

MAUAJI YAFANYIKA LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA!!!










Uefa Champions League
AC Milan 2-0 Auxerre
Arsenal 6-0 Braga
Bayern Munich 2-0 Roma
CFR 1907 Cluj-Napoca 2-1 Basle
Marseille 0-1 Spartak Moscow
MSK Zilina 1-4 Chelsea
Real Madrid 2-0 Ajax
Shakhtar Donetsk 1-0 Partizan Belgrade

CUF NA MATOKEO YA UTAFITI YA SYNOVTE!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumefarijika kwa taarifa iliyosahihi inayoelezea hali halisi ya utolewaji wa Habari za kampeni katika vyombo vya Habari, iliyoripotiwa na Meneja taasisi ya Synovate Bi. Jane Meela jana Jumanne, Septemba 14, jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo ambayo imeripotiwa katika vyombo vya Habari imebainisha kwamba, katika utafiti wao wa pili Taasisi ya Synovate imegundua kuwa katika kampeni zinazoendelea Magazeti yameegemea kuripoti zaidi Chama cha Mapinduzi (CCM) na kufuatiwa na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA) na kuviacha vyama vingine pasipo kupewa kipaumbele.

Taarifa hiyo imesema kuwa vyombo vya televisheni havikulalia upande wowote, taarifa zao wanazozitoa zinatoa kipaumbele kwa vyama mbalimbali (neutral) tofauti na vyombo vya magazeti, na isitoshe suala la amani limekuwa likizungumziwa zaidi katika kampeni zilizoripotiwa, halikadhalika Chama cha CHADEMA kilimepata kipaumbele mara baada ya kumtangaza mgombea wake wa Urais.

CUF – Chama cha Wananchi pamoja na kufarijika kwa ripoti hii ya Synovate ambayo inausahihi ndani yake, lakini pia tunamasikitiko kwa vyombo hivyo vya habari kwani pamoja na nia nzuri ya kuongozana na baadhi ya waandishi wao katika ziara za kampeni zetu za mgombea Urais na mgombea mwenza, lakini bado kipaumbele kimeelekezwa zaidi kwa wagombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Demokrasia Makini (CHADEMA).

CUF – Tunawatanabaisha Watanzania kuwa dhamira ya makusudi inayofanywa na vyombo vingi vya habari (ukiacha vichache), hususani magazeti ni kujaribu kuonyesha kuwa upinzani uliopo katika uchaguzi mwaka huu kwa Tanzania Bara, ni baina ya CCM na CHADEMA, na kwa upande wa Zanzibar ni baina ya CCM na CUF, jambo ambalo halina ukweli kabisa.

CUF – Tunatambua kuwa harakati hizi hazikuanza leo, kwani waandishi walidiriki kulitamka hili bayana katika mikutano yetu na waandishi wa habari mapema mwaka jana 2009, kabla ya kuumbuliwa na matokeo ya uchaguzi wa Serikali za mitaa, vitongoji na vijiji zilizofanyika mwishoni mwa Oktoba mwaka jana, ambapo pamoja na taarifa halisi za matokeo hayo kutotangazwa na wizara ya TAMISEMI (kwa kuchelea kuumbuka), bado chama chetu kilifanya zizuri kuliko chama kingine chochote cha upinzani.

Ikiwa hata mwaka haujatimia tangu uchaguzi huo kufanyika, hayamkiniki kigezo kinachotumika na baadhi ya vyombo hivi vya habari kukipa kipaumbele chama ambacho kiliambulia mitaa saba tu, katika jiji hili la Dar es Salaam, na chama chetu kufanikiwa kuchukua mitaa 34, ambapo maeneo yaliyokuwa ni ngome zetu kuu ambayo ni wastani wa robo tatu wa wagombea wetu walienguliwa.

CUF – Tunavisihi vyombo vya Habari pamoja na kuifanyia kazi kamilifu ripoti ya Synovate, wazingatie maadili ya uandishi wa habari, jambo ambalo wamekuwa wakiliahidi na kujivuna nalo, hatupendi matukio ya mwaka 2005 ya wananchi wenye hasira kali kukosa imani na vyombo hivyo, yakajirudia katika uchaguzi huu.

HAKI SAWA KWA WOTE

Wednesday, September 15, 2010

MAMBO YALIVYOKUWA CHAMPIONS LEAGUE!!!












Uefa Champions League
Barcelona 5-1 Panathinaikos
Benfica 2-0 Hapoel Tel-Aviv
Bursaspor 0-4 Valencia
FC Copenhagen 1-0 Rubin Kazan
FC Twente 2-2 Inter Milan
Lyon 1-0 Schalke 04
Man Utd 0-0 Rangers
Werder Bremen 2-2 Tottenham