Monday, December 20, 2010

CUF WAMSHUKIA MZEE MWINYI SAKATA LA KATIBA MPYA!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeshitushwa na kauli aliyoitoa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wa awamu ya nne Mhe. Ali Hassan Mwinyi wiki iliyopita ya kutoona sababu ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa sasa.

Kwa mujibu wa vyombo vya Habari alidai kuwa haungi mkono wazo la kufanya mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa sasa, hii ni kwa maslahi ya nani?

CUF – Chama Cha Wananchi tunasisitiza tumeshitushwa na kauli hii iliyotolewa na mtu ambaye anaheshima kubwa katika nchi hii, tunaingia shaka kwamba hakubaliani na mabadiliko hayo kufanyika sasa hivi kwa sababu hana maslahi nayo hadi hapo dhamira yake ya matumizi ya Katiba hiyo itakapokamilika hasa ukizingatia miongoni mwa wanafamilia yake wana fursa kubwa ya kuwania urais katika nchi hii.

CUF – hatuanimi kuwa mapungufu yaliyomo katika Katiba hiyo yeye hayatambui, ila inatudhihirishia wazi kuwa kuna uwezekano mkubwa yeye akiwa Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi kuitumia au hata kushauri vifungu vyenye utata vya katiba hiyo, kutumika kwa maslahi ya CCM.

CUF – Tunahimiza mabadiliko ya katiba ni lazima, iwapo kama tunataka demokrasia ya kweli, hatuwezi kuwa na katiba yenye Tume isiyokuwa huru ambayo Rais aliyeiteua anaweza kuivunja wakati wowote hata kwa sababu nyingine yeyote au kwa sababu ya tabia mbaya lakini wakati huo huo chombo cha kisheria kama mahakama hakina uwezo wa kuchunguza lolote lililotendwa na tume hiyo ya uchaguzi (ibara ya 74).

CUF – Tunaendelea kuwasihi, watanzania wote waumini wa dini zote, vyama vyote vya siasa, Taasisi zote nchini, asasi za kiraia, wanaharakati wa aina zote, kuungana kwa pamoja kudai mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayokidhi mahitaji ya watanzania wote.

No comments:

Post a Comment