Wednesday, March 16, 2011

CUF WAANZA KUWASHUKURU WAPIGA KURA!!

Waheshimiwa waandishi wa Habari, CUF- Chama Cha Wananchi kitafanya ziara ya awali ya kuwashukuru wapigakura katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, kisiwa cha Unguja, Lindi, Mtwara na Pwani kuanzia tarehe 19/03/2011 hadi tarehe 02/04/2011.

Ziara itaongozwa na Mwenyekiti wa CUF - Taifa, Prof. Ibrahimu Haruna Lipumba akifuatana na Kaimu Naibu Katibu Mkuu - Bara, Mhe. Julius Mtatiro, Wajumbe wa Baraza kuu la Uongozi - Taifa, Kiongozi wa wabunge wanaotokana na CUF ( Mh. Hamad Rashidi) na baadhi ya wabunge wanaotokana na CUF.



Malengo

· Kuwashukuru wabiga kura kwa kukipigia Chama Cha Wananchi (CUF) katika uchaguzi mkuu wa 31, Oktoba, 2010

· Kuishitaki kwa wananchi serikali ya CCM kwa kushindwa kuboresha maisha ya wananchi wake na kusababisha:-

o Kukosekana kwa umeme wa uhakika,

o Kupanda kwa gharama za maisha mfano bidhaa, nauli, na nk,

o Matatizo makubwa katika sekta ya afya,

o Uhaba wa maji , ukosefu wa ajira

o Miundombinu mibovu ya barabara, reli na nk

o Matatizo katika sekta ya Elimu na pia:-

Kuitaka Serikali ya CCM kuhakikisha kuwa mchakato wa Tume Huru ya Uchaguzi unafanyika mapema bila kusubiri mchakato wa kupata Katiba Mpya ya nchi.

CUF- Chama Cha Wananchi tunaamini kuwa ziara hii ni muhimu kwa wananchi wote,na tutatumia fursa hii kuwahakikishia wananchi kwamba CUF iko bega kwa bega na wananchi wote bila kujali itikadi zao za rangi, dini au kabila ili kuwaletea ukombozi wa kweli wa kiuchumi na kijamii.

No comments:

Post a Comment