Wednesday, March 9, 2011

ARSENE WENGER ALIA NA MASSIMO BUSACCA!!



Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ameibuka mbogo na kumlaumu vikali Mwamuzi wa mchezo wao dhidi ya Barcelona, Massimo Busacca!! Kwa kifupi tu wale wasiomfahamu Busacca ni mwamuzi wa Uswiss tangu mwaka 1990 na alipata Beji ya FIFA mwaka 1999!! Lakini huyu ndiye aliyechezesha mchezo wa Fainali wa Ligi ya Mabingwa kati ya Barcelona na Manchester United!! Wenger na Rob Van Persie ambaye alizawadiwa kadi nyekundu kila mmoja amemlaumu Mwamuzi huyo kwa kusema alibadili mchezo baada ya kutoka kadi ya njano ya pili!!

No comments:

Post a Comment