Tuesday, April 20, 2010

VYETI VYA FORM FOUR KUWEKWA PICHA!!!

Serikali kupitia Baraza la Mitihani la Tanzania imeanza kuweka picha katika vyeti vya matokeo ya kidato cha nne na sita ili kudhibiti kutumiwa na watu wasio watainiwa kwa ajili ya kutafuta ajira au nafasi za masomo ya juu.

Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mheshimiwa Mwantumu Mahiza amesema hatua hiyo ya kuweka picha katika vyeti itawawezesha wadau kumtambua mmiliki halali wa cheti.

Aidha Mheshimiwa Maiza alisema zoezi la kuweka vyeti hivyo picha huwekwa kwa kompyuta hivyo picha hizo haziwezi kuondolewa.

Pia amesema zoezi la kuweka picha katika vyeti litaanza na vyeti vya watahini waliofanya Mtihani wa kidato cha nne mwaka 2008 ambavyo vitachapwa mwezi Mei 2010

Naibu Waziri amesema hati ya matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2009 zimetolewa zikiwa na picha

Akijibu swali la nyongeza Waziri Maiza amesema serikali haian taarifa ya kubadilishana vyeti kwa wahusika kwani jambo hilo huwa hufanyika kwa makubaliano maalumu kati ya mwenye cheti na nayetaka kupew cheti hicho.

Hata hivyo Naibu Waziri Mahiza aliongezea kuwa Serikali imewakamata na inaendelea kuwakamata wale wote waliofoji vyeti na kuwafikisha katika vyombo vya sheria kwa hatua zaidi za kisheria

Ametoa wito rai kwa wananchi wote kuacha mtindo wa kutumia vyeti visivyokuwa vyao kwani kwa kufanya hivyo kunawanyima haki wenye vyeti stahili zao na ni kutenda kosa la jinai.

No comments:

Post a Comment