Monday, April 12, 2010

CUF WAANZA MAMBO YAO!!!

CUF – Chama Cha Wanachi kimeshtushwa na kauli ya Mbunge wa Songea Mjini, ambaye ni Naibu wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emmanuel Nchimbi ya kuchangia sekta ya elimu kwenye jimbo lake la Songea Mjini zaidi ya shilingi milioni 300. Hayo aliyasema wakati wa kukabidhi majengo ya Sekondari ya kidato cha tano na sita yalioyopo Mkuza katika Manispaa ya Songea aliyojenga kwa juhudi zake binafsi.

Kwa kuzingatia kiwango cha mishahara ya mawaziri hapa Tanzania kauli ya Nchimbi imeleta utata juu ya uhalali wa mchango wake huo wa Tshs milioni 300 kwa kipindi chote ambacho amekuwa Waziri katika Serikali hii ya awamu ya nne.

CUF- Chama Cha Wananchi kinatambua tabia ya viongozi wa CCM kila inapofikia kipindi hiki kuelekea uchaguzi Mkuu wao huanza kufanya kampeni kabla ya wakati na kutumia fedha ambazo hazilingani na vipato vyao halali kwa vipindi vyao vyote vya uongozi.

CUF – Chama Cha Wananchi kinamtaka msajili wa vyma ambae ndie msimamizi mkuu wa sheria za uchaguzi kwa kushirikiana na TAKUKURU kwa mujibu wa kauli yao kwa vyombo vya habari wamfuatilie Dr. Nchimbi kwani licha ya kutoa rushwa lakini pia ni ufisadi mkubwa.

No comments:

Post a Comment