Friday, April 23, 2010

LIVERPOOL YALALA WAKATI FULHAM IKILAZIMISHA SARE UEFA!!




Michezo miwili ya nusu fainali ya Mchuano wa Ligi ya Europa imepigwa na kushuhudia Atletico Madrid wakiwalaza Vijogoo vya Jiji Klabu ya Liverpool wakati Fulham wakipata sare tasa ya ugenini dhidi ya Hamburg!!!

Tuesday, April 20, 2010

NYUMBA YATEKETEA KWA MOTO SONGEA!!!











Nyumba moja yateketea kwa Moto Songea eneo la Mfaranyaki huku chanzo chake kikiwa bado hakijathibitishwa ( Picha kwa Hisani ya Emmanuel Msigwa)

SERIKALI YA AWAMU YA NNE NA ELIMU!!!

Serikali ya Awamu ya Nne imefanikiwa kuwezesha asilimia 96 ya watoto wenye umri wa kwenda shule kuwa darasani kutoka asilimia 35 miaka sita iliyopita.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo leo jioni (19.4.10) Jijini New York katika sherehe ya chakula maalum kilichoandaliwa kwa ajili ya kuzindua rasmi Mfuko wa Elimu Tanzania, Tanzania Education Fund.

“Mafanikio yetu ya kwanza yametokana na kuweza kuandikisha watoto kujiunga na elimu ya msingi na kuhakikisha kila mtoto anayetakiwa kuwa shule anakuwa darasani, miaka 6 iliyopita asilimia 35 ya watoto Tanzania ambao walitakiwa kuwa darasani walikuwa mitaani au wapo katika ajira”. Amewaambia waalikwa waliohudhuria chakula hicho cha jioni “sasa hivi ninapoongea nanyi, tumefanikiwa kuandikisha watoto shuleni kwa asilimia 96 na tumedhamiria kuwapeleka wote shuleni” Rais amesema.

Mfuko wa Elimu Tanzania, ni Shirika lisilo la Kiserikali(NGO) lililoanzishwa na marafiki wa Tanzania wa Kimarekani kwa kushirikiana na Serikali yaTanzania.

Kwa miaka minne sasa Serikali ya Awamu ya Nne imeweka kithara na kuelekeza nguvu zake katika kuhakikisha sekta ya elimu hapa nchini inaboreshwa na kuimarishwa. Kwa kuzingatia kithara hizo, bajeti ya sekta ya elimu imekuwa ikiongoza kwa ukubwa hapa nchini ili kuhakikisha kuwa malengo ya msingi ya Awamu ya Nne yanafanikiwa.

Malengo haya ya msingi ni “Kuhakikisha watoto wa kike na wa kiume nchini Tanzania anapata elimu bora kuanzia elimu ya msingi, sekondari na hadi elimu ya juu” Rais amewaeleza marafiki wa Tanzania waliohudhuria chakula hicho.

Rais ameelezea mafanikio makubwa yaliyofikiwa ambapo mwaka 2000, Tanzania ilikuwa na shule za sekondari 927 na hadi kufikia mwaka 2009 shule hizo zimeongezeka kwa asilimia mia nne na kufikia idadi ya shule 4,102. Hivyo hivyo kiwango cha uandikishaji wanafunzi katika shule hizi za sekondari kimeongezeka kutoka 261,896 hadi kufikia milioni 1.46 katika kipindi hicho hicho.

Mafanikio mengine ni kwamba kati ya mwaka 2006 na 2009, jumla ya shule za sekondari 2,377 zimejengwa na hivyo kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka 524,325 mwaka 2005, hadi kufikia wanafunzi milioni 1.6.

Hata hivyo Rais Kikwete amesema mafanikio yote haya yameleta changamoto mpya ambazo ni uhaba wa walimu, uhaba wa vitabu na vifaa vya kufundishia, uhaba wa vyumba vya maabara na nyumba za walimu.

Rais amewaambia waalikwa kuwa gharama za kutatua changamoto zote hizi zinazidi Dola za Kimarekani Bilioni 1.2 kwa miaka mitano, gharama ambazo kwa nchi maskini kama Tanzania ni mtihani ambao unahitaji ubunifu katika kuzitatua.

“Inahitajika ubunifu na ushirikiano katika kutatua changamoto hizi kutoka kwa marafiki na ndiyo maana tumekusanyika leo hapa”. Rais amewaambia waalikwa akiwemo mfanyibiashara Douglas Pitt ambaye amekuwa akisaidia Tanzania kimya kimya kwa zaidi ya miaka sita.

Katika sherehe hizo kabla ya chakula cha kuzindua mfuko wa Elimu Tanzania, Rais alimtangaza rasmi Bw. Douglas Pitt kuwa Balozi wa hiari wa Tanzania ambaye atakua na kazi ya kuitangaza Tanzania katika highly zake za kibiashara, utalii na elimu.

Bw. Douglas Pitt ni mdogo wake mcheza sinema maarufu wa Marekani Bw. Brad Pitt.

Rais Kikwete amekamilisha ziara yake ya kikazi nchini Marekani na anaondoka Jijini New York leo tarehe 20April, 2010 kurejea Dar-es-salaam.

VYETI VYA FORM FOUR KUWEKWA PICHA!!!

Serikali kupitia Baraza la Mitihani la Tanzania imeanza kuweka picha katika vyeti vya matokeo ya kidato cha nne na sita ili kudhibiti kutumiwa na watu wasio watainiwa kwa ajili ya kutafuta ajira au nafasi za masomo ya juu.

Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mheshimiwa Mwantumu Mahiza amesema hatua hiyo ya kuweka picha katika vyeti itawawezesha wadau kumtambua mmiliki halali wa cheti.

Aidha Mheshimiwa Maiza alisema zoezi la kuweka vyeti hivyo picha huwekwa kwa kompyuta hivyo picha hizo haziwezi kuondolewa.

Pia amesema zoezi la kuweka picha katika vyeti litaanza na vyeti vya watahini waliofanya Mtihani wa kidato cha nne mwaka 2008 ambavyo vitachapwa mwezi Mei 2010

Naibu Waziri amesema hati ya matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2009 zimetolewa zikiwa na picha

Akijibu swali la nyongeza Waziri Maiza amesema serikali haian taarifa ya kubadilishana vyeti kwa wahusika kwani jambo hilo huwa hufanyika kwa makubaliano maalumu kati ya mwenye cheti na nayetaka kupew cheti hicho.

Hata hivyo Naibu Waziri Mahiza aliongezea kuwa Serikali imewakamata na inaendelea kuwakamata wale wote waliofoji vyeti na kuwafikisha katika vyombo vya sheria kwa hatua zaidi za kisheria

Ametoa wito rai kwa wananchi wote kuacha mtindo wa kutumia vyeti visivyokuwa vyao kwani kwa kufanya hivyo kunawanyima haki wenye vyeti stahili zao na ni kutenda kosa la jinai.

Monday, April 19, 2010

CUF WALIA NA SHERIA YA WALEMAVU!!!

CUF – Chama cha Wananchi pamoja na kulipongeza Bunge la Jamhuri ya Muungano kupitisha muswada wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, tunamsihi Rais Jakaya Mrisho Kikwete kuharakisha kusaini muswada huo ili iwe sheria, lakini pia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Mwanasheria Mkuu kuhakikisha kanuni zinaandaliwa mapema kwa ajili ya utekelezaji.

Muswada huo uliopitishwa Bungeni wiki iliyopita, umeridhiwa na Wabunge wote bila kujali itikadi zao za kisiasa, na moja ya yaliyoridhiwa ni kuwepo kwa baraza la ushari litakalowashirikisha Watu wenye ulemavu na wadau wengine zikiwemo wizara za Serikali.

CUF – Chama cha Wananchi tunakila sababu ya kushinikiza kusainiwa muswada huo pia kuandaliwa kanuni zake haraka iwezekanavyo kama ilivyofanyika kwa muswada wa sheria ya gharama za uchaguzi, ili kuepusha yaliyotokea katika Sera ya Taifa ya Huduma ya Maendeleo kwa Watu wenye Ulemavu ambayo ilitolewa April 2004 na kuzinduliwa 2007 kwa kudandia maadhimisho ya Siku ya Watu wenye ulemavu duniani ambayo yameandaliwa na watu wenye ulemavu wenyewe.

Hiyo kama haitoshi hadi unaandaliwa muswada wa sheria ya haki za watu wenye ulemavu sera hiyo bado haijaandaliwa mkakati wa utekelezaji, jambo linalotia mashaka, hivyo ni budi maamuzi ya Bunge la Jamhuri ya kapewa thamani na uzito unaostahili kwa kutambua kwamba masuala ya watu wenye ulemavu yana gusa kila binadamu alie hai kwani inatambulika kuwa “Hujafa Hujaumbika”.

CUF – Halikadhalika tunamtanabaisha Rais Jakaya Kikwete kuwa masuala ya Watu wenye Ulemavu ni mtambuka, na yanahusisha karibuni wizara zote za Serikali, hivyo basi hana budi kulitambua hili na kuhamisha masuala ya Watu wenye ulemavu kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na kusimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ili iwe rahisi kusimiwa na kufuatilia utekelezaji wake.

CUF – Tunawahimiza watu wenye ulemavu kuzitumia vyema haki zao na fursa zilizomo katika vyama vya siasa hususan chama mbadala Chama cha Wananchi – CUF, kwa kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea, na chama kinaahidi kuwa hakuna ubaguzi wowote, tutaheshimu uwezo wa mtu bila ya kujali maumbile yake.

SIMBA YAKABIDHIWA KOMBE!!!


Wachezaji wa Simba wakinyanyua Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambalo wamekabidhiwa baada ya kuichakaza Yanga kwa magoli 4-3. Hongera Simba kwa Ubingwa!!!

Sunday, April 18, 2010

RAIS KIKWETE ALIVALIA NJUGA SUALA LA AFYA!!!

Changamoto Kubwa inayozikumba nchi zinazoendelea katika utoaji wa huduma za afya ni tatizo kuwa watu wa nchi hizi wanakabiliwa na maradhi mengi na wanaugua mara kwa mara.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo leo wakati alipokuwa anatoa mhadhara juu ya “Changamoto za Utoaji wa Huduma za Afya katika Nchi Zinazoendelea“ katika Chuo Kikuu cha Afya cha Weill Cornel Jijini New York.

“Afrika ina asilimia 11 tu ya idadi ya watu duniani lakini ina asilimia 24 ya mzigo wa maradhi duniani”, Rais amesema na kunukuu takwimu za shirika la Afya Duniani (WHO) ambazo zinaonesha kuwa kati ya vifo 10 vinavyotokea katika nchi tajiri, ni mtu mmoja tu ndiye anayekufa kutokana na magonjwa ya kuambukiza, wakati katika nchi maskini vifo sita kati ya kumi vinatokana na na maradhi ya kuambukiza.

Hii ni kutokana na ukweli kuwa nchi maskini bado zinakabiliwa na maradhi ambayo yalishatokomezwa katika nchi zilizoendelea na kutoa mfano wa magonjwa kama malaria, kipindupindu, maradhi ya kuhara, typhoid na mengine mengi.

Rais Kikwete amewaeleza wanafunzi, wahadhiri na wageni waalikwa katika mhadhara huo kuwa, changamoto ingine inayozikabili nchi maskini ni uhaba wa wataalamu na huduma za afya ambazo ni pamoja na madawa na vitendea kazi, suala ambalo husababisha uchunguzi na matibabu kuwa magumu.

“Hata hivyo haya yote yanasababishwa na umaskini ambao umesababisha magonjwa makubwa kuwa mzigo na uwezo mdogo wa kukabiliana na maradhi” Rais amefafanua, pato la taifa la nchi zote Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa mwaka 2008 lilikuwa dola za Kimarekani Bilioni 987.1, ambayo ni karibu na pato la taifa la nchi ya Korean ya Kusini ambalo lilikua Bilioni 992.0 na chini zaidi kuliko pato la Jiji la New York ambalo lilikua dola Trillion 1.4.

Hata hivyo pamoja na changamoto zote hizo Rais amesema, wananchi wa nchi zinazoendelea hawajakata tamaa na wanajitahidi kwa uwezo wao kuzikabili changamoto hizo na kujitahidi kuishi vyema, kwa kutengeneza sera, mipango na mazingira mazuri kulingana na hali halisi ya nchi zao.

Ameongeza kuwa kati ya jitihada hizo ni nchi hizi kutenga bajeti kubwa kwa ajili ya sekta ya Afya ingawa hata hivyo siyo kubwa sana ya kuweza kutatua matatizo ya sekta nzima ya afya kwa vile nchi hizi hazina uwezo mkubwa.

Ametoa mfano wa Tanzania ambayo ina mpango wa Afya wa miaka kumi ambao unalenga katika kuongeza na kuboresha huduma za afya ambapo serikali imeadhimia kujenga vituo vya Afya Tanzania nchi nzima katika umbali usiozidi km 5 kutoka makazi ya wananchi, kuongeza juhudi za kupambana na maradhi kama malaria, ukimwi, TB na maradhi ya kuambukiza.

Serikali pia inajidhatiti katika kujenga uwezo wa kubaini, kupima na kutibu magonjwa makubwa nchini ili wagonjwa watibiwe nchini, kuongeza idadi na uwezo wa wataalamu.

MCHUANO WA LANGALANGA WASHIKA KASI!!!!


Mchuano wa magari yaendayo kasi duniani maarufu kwa jina la Langalanga umemalizika nchini China na kushuhudia Jenson Button akiikwaa nafasi ya kwanza, huku nafari ya pili ikienda kwa Lewis Hamilton na nafasi ya tatu ikiangukia kwake Nico Rosberg. Mpangilio kwa nafasi kumi za juu ni kama ifuatavyo:
Driver Time
1 J Button 1:46:42.163
2 L Hamilton 1:46:43.693
3 N Rosberg 1:46:51.647
4 F Alonso 1:46:54.032
5 R Kubica 1:47:04.376
6 S Vettel 1:47:15.473
7 V Petrov 1:47:29.763
8 M Webber 1:47:34.335
9 F Massa 1:47:39.959
10 M Schumacher 1:47:43.912

DAKIKA CHACHE ZIMESALIA KABLA YA SIMBA NA YANGA KUUMANA!!!


Uwanja Mkuu wa Taifa ambapo dakika chache zijazo kutapigwa mchezo wa watani wa Jadi Simba na Yanga ukiwa mchezo wa mwisho katika Msimu huu ambapo tayari Wekundu wa Msimbazi wameshatwaa ubingwa!!!

LIGI KUU NCHINI ENGLAND YAFIKA PATAMU!!!



Michezo mitatu ikiwa imesalia kwa Chelsea na Manchester United kabla ya kumaliza Ligi Kuu Nchini England hatua tamu zaidi imefikia. Baada ya Man Utd kuifunga Man City wenzao Chelsea wamepoteza mchezo wao dhidi ya Tottenham Hotspurs na hivyo kufanya kibarua kuwa kigumu cha nani ataibuka Bingwa msimu huu.

BONGO YAWEZEKANA IKATOKEA KWELI??


Furaha ya Ushindi ambapo Beki wa Manchester United Gary Neville anaonekana akimbusu Paul Scholes ambaye alifunga goli la pekee kwenye mchezo dhidi ya Manchester City na kuweka hai matumaini ya kutwaa Ubingwa!!!

Monday, April 12, 2010

VAN PERSIE AREJEA!!!


Mshambuliaji wa Kimataifa wa Uholanzi ambaye anakipiga katika Klabu ya Arsenal Robin Van Persie anatarajiwa kurejea ugani katika mpambano wa London Derby katika ya Arsenal na Tottenham Hotspurs baada ya kupona matatizo ya mguu ambayo yalikuwa yanamkabili!!

CUF WAANZA MAMBO YAO!!!

CUF – Chama Cha Wanachi kimeshtushwa na kauli ya Mbunge wa Songea Mjini, ambaye ni Naibu wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Emmanuel Nchimbi ya kuchangia sekta ya elimu kwenye jimbo lake la Songea Mjini zaidi ya shilingi milioni 300. Hayo aliyasema wakati wa kukabidhi majengo ya Sekondari ya kidato cha tano na sita yalioyopo Mkuza katika Manispaa ya Songea aliyojenga kwa juhudi zake binafsi.

Kwa kuzingatia kiwango cha mishahara ya mawaziri hapa Tanzania kauli ya Nchimbi imeleta utata juu ya uhalali wa mchango wake huo wa Tshs milioni 300 kwa kipindi chote ambacho amekuwa Waziri katika Serikali hii ya awamu ya nne.

CUF- Chama Cha Wananchi kinatambua tabia ya viongozi wa CCM kila inapofikia kipindi hiki kuelekea uchaguzi Mkuu wao huanza kufanya kampeni kabla ya wakati na kutumia fedha ambazo hazilingani na vipato vyao halali kwa vipindi vyao vyote vya uongozi.

CUF – Chama Cha Wananchi kinamtaka msajili wa vyma ambae ndie msimamizi mkuu wa sheria za uchaguzi kwa kushirikiana na TAKUKURU kwa mujibu wa kauli yao kwa vyombo vya habari wamfuatilie Dr. Nchimbi kwani licha ya kutoa rushwa lakini pia ni ufisadi mkubwa.

KUMRADHI WADAU!!!

Niwaombe radhi wadau wote wa Blogu hii kuna kigugumizi sugu kilitokea na hivyo kusababisha mambo kushindwa kwenda kama kawaida! Lakini sasa mambo yametengamaa na kila siku nitaendelea kushusha mizigo mizito kazi kwenu!!