Friday, December 31, 2010

HAPPY NEW YEAR TO ALL!!


Nawatakia Heri ya Mwaka Mpya wadau wote wa Blogu hii na nawashukuru kwa kile ambacho imekifanya na kuchangia Blogu hii kufika hapa!! Kumbuka tarehe Moja ya kila mwezi January Nurdin Selemani mmiliki wa Blogu huu huwa anazaliwa!!

Thursday, December 30, 2010

LIVERPOOL KIMEO, CHELSEA IKIFUFUKA, ARSENAL NGUVU YA SODA!!







Waswahili husema mwaka wa hasara ni hasara tu hata ufanyaje na ng'ombe wa maskini hazai!! Klabu ya Liverpool imeendelea kudhihirisha hili baada ya kupata kichapo cha nyumbani kutoka kwa Wolverhampton kwa goli moja kwa nunge!! Matokeo ya michezo mingine ni kama inavyoonekana:
Chelsea 1-0 Bolton
Liverpool 0-1 Wolverhampton
Wigan 2-2 Arsenal

Monday, December 27, 2010

ANCELOTTI AKALIA KUTI KAVU CHELSEA!!



Kocha Mkuu wa Chelsea Carlo Ancelotti amekalia kuti kavu baada ya timu yake kupata kichapo cha magoli 3-1 kutoka kwa Arsenal!! Licha ya dalili kuonesha kibarua chake kipo mashakani kutokana na kutoshinda michezo sita mwenyewe amesisitiza ataendelea kuwepo na sasa anataka kusajili zaidi January!!

CHELSEA KIMEO KWA ARSENAL!!





Washika Magobole wa Jiji la London Arsenal wamefanikiwa kumaliza uteja mbele ya Chelsea baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 3-1!! Magoli ya Ale Song, Cecs Fabregas na Theo Walcott ndiyo yaliyomaliza uteja wa Arsenal!!

Sunday, December 26, 2010

LIGI KUU ENGLAND YAENDELEA KUCHANJA MBUGA KWA KASI!!








Ligi Kuu nchini England maarufu kama Barclays Premium League imeendelea siku ya Boxing Day na kushuhudia Manchester United ikiendelea kujichimia kileleni mwa Ligi. Matokeo yote yalikuwa hivi:
Aston Villa 1-2 Tottenham
Blackburn 0-2 Stoke
Bolton 2-0 West Brom
Fulham 1-3 West Ham
Man Utd 2-0 Sunderland
Newcastle 1-3 Man City
Wolverhampton 1-2 Wigan

Monday, December 20, 2010

GOLIKIPA BORA KWA UPANDE WANGU!!


Anaitwa Muteba Kidiaba Golikipa wa Klabu ya TP Mazembe ambaye style yake ya ushangiliaji imemzolea umaarufu mkubwa!! Lakini pia ni golikipa anayejua wajibu wake pindi anapokuwa golini kutetea Klabu na hata Timu yake ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC!!

TP MAZEMBE NA HISTORIA KWENYE SOKA!!


Klabu ya TP Mzembe hatimaye imeweza kuandika historia na kuudhihirishia ulimwengu kuwa hata Klabu za Bara la Afrika zinaweza kusakata soka la uhakika!! TP Mazembe ambao walishindwa kutwaa ubingwa wa Klabu Bingwa ya Dunia mbele ya Inter Milan watakumbukwa daima kwa kile ambacho wamekifanya!! Hii inawadhihirishia wale ambao walikuwa wanahoji jinsi ambavyo walitwaa Ubingwa wa Klabu Bingwa Barani Afrika!!

NAWEKA KUMBUKUMBU SAWA!!


Kwa kweli wanazi wa kabumbu wanasubiri kwa hamu mwezi February ufike ili washuhudie kile ambacho wenyewe wanakiita fainali ya mapema kati ya Barcelona na Arsenal!! Ngoja tusubiri ili tujue mambo yatakuwaje kwa kweli!!

CUF WAMSHUKIA MZEE MWINYI SAKATA LA KATIBA MPYA!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeshitushwa na kauli aliyoitoa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania wa awamu ya nne Mhe. Ali Hassan Mwinyi wiki iliyopita ya kutoona sababu ya kufanya mabadiliko ya Katiba kwa sasa.

Kwa mujibu wa vyombo vya Habari alidai kuwa haungi mkono wazo la kufanya mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kwa sasa, hii ni kwa maslahi ya nani?

CUF – Chama Cha Wananchi tunasisitiza tumeshitushwa na kauli hii iliyotolewa na mtu ambaye anaheshima kubwa katika nchi hii, tunaingia shaka kwamba hakubaliani na mabadiliko hayo kufanyika sasa hivi kwa sababu hana maslahi nayo hadi hapo dhamira yake ya matumizi ya Katiba hiyo itakapokamilika hasa ukizingatia miongoni mwa wanafamilia yake wana fursa kubwa ya kuwania urais katika nchi hii.

CUF – hatuanimi kuwa mapungufu yaliyomo katika Katiba hiyo yeye hayatambui, ila inatudhihirishia wazi kuwa kuna uwezekano mkubwa yeye akiwa Mwenyekiti mstaafu wa Chama cha Mapinduzi kuitumia au hata kushauri vifungu vyenye utata vya katiba hiyo, kutumika kwa maslahi ya CCM.

CUF – Tunahimiza mabadiliko ya katiba ni lazima, iwapo kama tunataka demokrasia ya kweli, hatuwezi kuwa na katiba yenye Tume isiyokuwa huru ambayo Rais aliyeiteua anaweza kuivunja wakati wowote hata kwa sababu nyingine yeyote au kwa sababu ya tabia mbaya lakini wakati huo huo chombo cha kisheria kama mahakama hakina uwezo wa kuchunguza lolote lililotendwa na tume hiyo ya uchaguzi (ibara ya 74).

CUF – Tunaendelea kuwasihi, watanzania wote waumini wa dini zote, vyama vyote vya siasa, Taasisi zote nchini, asasi za kiraia, wanaharakati wa aina zote, kuungana kwa pamoja kudai mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayokidhi mahitaji ya watanzania wote.

Wednesday, December 1, 2010

MAN UTD YAANGUKIA PUA, ARSENAL IKIUA CARLING CUP!!




Manchester United imekumbana na shubiri baada ya kupata kichapo cha kwanza msimu huu cha magoli manne kwa nunge wakati Arsenal wakitinga Nusu Faila ya Carling Cup kwa kuichabanga Wigan Athletics kwa magoli mawili kwa buyu!!

KIKWETE KUHUDHURIA MKUTANO WA EAST AFRICA!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete anatarajia kwenda Mkoani Arusha leo mchana, kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha kawaida cha Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kinachoanza kesho tarehe 2 Disemba.

Rais Kikwete anamaliza kipindi chake cha mwaka mmoja cha kuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kumkabidhi uenyekiti kiongozi mwingine katika kikao hicho kama ilivyo katika taratibu za Jumuiya ya Afrika Mashariki. Rais Kikwete alipokea uenyekiti kutoka kwa Rais Paul Kagame katika kikao cha Novemba mwaka jana , 2009.

Katika kikao cha wiki hii viongozi watapokea taarifa mbalimbali za Baraza la Mawaziri zinazohusu utekelezaji wa masuala yanayohusu Jumuiya na kujadili mambo mbalimbali.

Mapema leo asubuhi katika Ikulu ya Dar-Es-Salaam, Rais Kikwete amempokea Kijana wa Kitanzania Musa Lunyeka Dotto , mkazi wa kijiji cha Chabulongo, kata ya Kasamwa Wilaya ya Geita aliyeweka azma ya kusafiri kwa baiskeli kutoka Geita hadi Dar-Es-Salaam, kuja kumpongeza Rais Kikwete kwa kuchaguliwa tena kuiongoza nchi.

Hata hivyo, Musa alipofika Singida Katibu wa Vijana wa CCM, mkoani humo alimshauri apande basi hadi Dar-es-salaam, na ndipo alipofika na leo kutimiza azma yake ya kumsalimia na kumpongeza Rais Kikwete.

Rais Kikwete amemshukuru kijana huyo kwa moyo wake huo na kuahidi kumsaidia zaidi katika shughuli zake za kilimo ili apate manufaa na mafanikio zaidi.