Monday, February 13, 2012

WOLVES IMEMTIMUA KAZI KOCHA WAKE KUTOKANA NA KUPATA MATOKEO MABAYA!!!


Klabu ya Wolvehampton Wanderers ya nchini Uingereza imesitisha mkataba wake na Kocha aliyekuwa anakinoa kikosi hicho Mick McCarthy kutokana na timu hiyo kupata matokeo mabaya na hivyo kujiweka kwenye hatari ya kuweza kushuka daraja!!! Wolves imeshinda mchezo mmoja pekee kwenye michezo kumi na tatu iliyocheza na hivyo dhahiri imeanza kujichimia shimo la kushuka daraja msimu huu!!!

ZAMBIA MABINGWA WA AFRIKA WAICHAKAZA IVORY COAST!!!








Timu ya Taifa ya Zambia maarufu kama Chipolopolo imefanikiwa kutwa Ubingwa wa Mataifa ya Afrika kwa mara ya kwanza baada ya kufanikiwa kuifunga Ivory Coast kwa mikwaju ya penalty 8-7!! Mchezo huo ulipigwa dakika 120 lakini hakuna timu ambayo iliweza kupata goli ndipo mikwaju ya penalty ikalazimika kutumika. Kolo Toure na Gervihno ndiyo walikosa penalty za Ivory Coast wakati kwa Zambia Kabala ndiye alikosa mkwaju huo. Stoppila Sunzu alifunga penalty na mwisho na kuwapa ushindi Chipolipolo!!!

Thursday, February 9, 2012

ZAMBIA NA IVORY COAST USO KWA USO FAINALI AFCON!!!



Timu ya Taifa Zambia maarufu kama Chipolopolo inatarajiwa kupambana na Ivory Coast maarufu kama Tembo baada ya timu hizo kushinda michezo yake ya Nusu Fainali!! Zambia walifanikiwa kuiondosha Ghana maarufu kama Black Stars kwa goli moja kwa nunge goli la kwake Emmanuel Mayuka!! Ivory Coast wakawaondosha Mali maarufu kama Eagles kwa goli moja la kwake Gervais Yao Kouassi Gervinho!!! Mchezo wa kusaka nafasi ya Mshindi wa Tatu ni kati ya Mali dhidi ya Ghana siku ya jumamosi!! Fainali itapigwa siku ya jumapili!!!

FABIO CAPELLO AACHIA NGAZI UKOCHA WA ENGLAND!!!


Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Uingereza Fabio Capello ametangaza kujiuzlu wadhifa wake baada ya kufanya mazungumzo na Viongozi wa Chama Cha Soka nchini humo FA baada ya kupinga hatua na Nahodha John Terry kunyang'anywa unahodha!! Capello alionekana kuchukizwa na hatua hiyo na kutoa maneno ambayo yaliikera FA na sasa Harry Redknapp anatajwa huenda akachukua jukumu hilo!! Terry alinyang'anywa Unahodha baada ya kutoa maneno ya kibaguzi dhidi ya Anton Ferdinand na kumfanya afunguliwe kesi kitu kilichowafanya FA kumpora wadhifa huo!!!

WAZIRI MKUU PINDA AKUTANA NA MADAKTARI KUWASIHI WAMALIZE MGOMO!!!


Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Peter Pinda anaendelea kukutana na Uongozi wa Hospital ya taifa ya Muhimbili pamoja na Madaktari Bingwa kutoka Sekta ya Umma, Binafsi na Wastaafu ili kumaliza mgomo wa madakatari uliodumu kwa zaidi ya majuma mawili.

Mkutano huo ulianza saa tatu asubuhi ambapo pia Waziri Mkuu atakutana na Madaktari Bingwa, madaktari Waliosajili na Madaktari Waliopo Kwenye Mafunzo kwa Vitendokabla ya kukutana na Wafanyakazi wa Hispotali ya Muhimbili, Moi, Ocean Road na Wawikilishi kutoka Hospital za Mkowa wa Dar Es Salaam.

WANAHARAKATI WAFUNGA BARABARA WAKISHINIKIZA SERIKALI KUMALIZA MGOMO WA MADAKTARI!!!





Wanaharakati Jijini Dar Es Aalaam wakiwa wamepiga kambi katika Barabara ya Ally Hassan Mwinyi wakishinikiza serikali kuzungumza na Madaktari ambao wapo kwenye mgomo uliodumu kwa zaidi ya majuma mawili sasa huku wagonjwa wakiendelea kupoteza maisha!! Wanaharakati hao wametaka hilo lifanyike mara moja ili kunusuru maisha ya wagonjwa!!!