Monday, January 3, 2011

CUF NA HARAKATI ZAO ZA KISIASA!!!

CUF – Chama cha Wananchi tumeamua kujipanga na kujizatiti upya ili kuboresha zaidi mafanikio yaliyopatikana 2010 na kuzitafutia ufumbuzi changamoto zote tulizozipata mwaka 2010 ili kuleta mafanikio mazuri yatakayoweza kutimiza malengo yetu ya miaka mitano (2011 – 2015).

Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana;

1.Uwepo wa mshikamano ndani ya chama ambapo viongozi na wanachama awamekuwa hawahitilafiani katika masuala ya msingi

2.Utaratibu wa shughuli za chama umefanywa kwa kufuata katiba ya chama na misingi mikuu ya uendeshaji wa chama bila kugongana kitarataibu na kiutendaji.

3.Mafanikio ya uteuzi wa wagombea wa urais jamhuri ya muungano na Zanzibar ambapo tulisimamisha wagombea wanaokidhi sifa za kuongoza chi kwa mafanikio makubwa.

4.Kushiriki katika uchaguzi mkuu na kupata mafanikio;

·Wabunge 0 mwaka 2005 hadi 2 mwaka 2010 upande wa Tanganyika .

·Wabunge 19 mwaka 2005 hadi 22 mwaka 2010 upande wa Zanzibar.

·Madiwani 96 mwaka 2005 hadi 152 mwaka 2010 upande wa Tanganyika.

5.CUF kimezidi kuimarisha utaifa mwaka 2010,kwa kuwa chama cha kipekee cha kitaifa ambapo tumeafanikiwa kupata wawakilishi na wabunge kutoka katika kila upande wa muungano.

·Kwa mfano,tumepata wabunge Bara,unguja na Pemba .

·CCM wamepata wabunge bara na unguja peke yake.

·CHADEMA wamepata wabunge bara peke yake.

6.Tumefanikiwa kuendelea kupata wabunge wengi wa kuchaguliwa kuliko vyama vingine vyote vya upinzani,mwaka huu 2010 tumepata wabunge 24 waliochaguliwa kwa kura na wananchi.

7.Kuwepo kwa serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar kulikotokana na kura za maoni ya wananchi wa Zanzibar walipoamua kuwa kuanzia uchaguzi wa 2010 chama kitakachoshinda uchaguzi kwa upande wa Zanzibar kitatoa rais na kitakachokuwakuwa cha pili kitatoa makamu wa kwanza wa rais,na kwa mafanikio makubwa baada ya uchaguzi CUF ikawa ya pili Zanzibar na hivyo maamuzi ya wananchi ya kuwa na serikali ya umoja wa kitaifa yakatekelezwa na sasa CUF imekuwa chama cha kwanza cha upinzani Tanzania kuingia serikalini kwa mujibu wa katiba upande wa Zanzibar.

8.Kufanikiwa kuwasilisha rasimu ya mapendekezo ya katiba mpya kwa waziri wa sheria na katiba japokuwa Polisi walitumia nguvu kubwa kuzuia CUF imeonesha ukomavu mkubwa sana kuwa wakitetea jambo la kidemokrasia la kudai haki za watu hawaogopi dola,kwa hiyo CUF inabaki kuwa chama cha kipekee katika kuwapigania watanzania.

CHANGAMOTO;
Nafasi ya urais tumerudi nyuma kutoka nafasi ya 2 mwaka 2005 hadi nafasi ya tatu mwaka 2010.

MALENGO YA CUF 2011 – 2015

1.Kushika hatamu za dola bara na Zanzibar kupitia michakato yote ya uchaguzi itakayojitokeza

2.Kuendeleza na kuimarisha umoja ndani ya chama.

3.Kutoa elimu ya uraia kupitia michakato ya kisiasa na kijamii.

4.Kuingiza wanachama wengi wapya ndani ya chama.

5.Kuendeleza madai ya katiba mpya na siyo marekebisho ya katiba hadi tupate katiba mpya itakayokuwa na maoni ya watanzania wote.

6.Kuendeleza michakato ya kuviweka pamoja vyama vya upinzani ili sote kwa pamoja kama wapinzani tuwe na dira ya pamoja na hii isaidie kutowayumbisha watanzania wanapoenda kuchagua viongozi.

No comments:

Post a Comment